Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii
SURAT AT-TAKAATHUR
Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Imam Bukhari anaeleza ya kuwa ilishuka Madina. Lakini sahaba mmoja, Ibni Abbas, anasema ya kuwa ilishuka Makka. Neno Takaathur anasema Ibn Abbas maana yake ni tamaa nyingi ya mali na watoto (Bukhari). Abu Huraira anasimulia ya kuwa Mtume s.a.w. aliposoma sura hii alisema, "Mwanadamu anasema, hii ni mali yangu, hii ni mali yangu. Kumbe aliyokula na kuvaa ameichakaza, aliyotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, ndiyo kaiweka akiba na iliyobaki si yake ni mali ya watu."
Sababu za kushuka sura hii:-
Muqatil na Al-Kalb wamesema “sura hii ilishuka kutokana na makabila mawili ya Kikurayshi, ambayo ni Banu Abd Manafi na Banu Sahm. Kila kabila lilikuwa likijisifu na kujigamba juu ya lingine. Hivyo ikafikia hadi wakaanza kuheabu ni kabila lipi lina machifu wengi na viongozi wengi kuliko lingine. Banu Abd Manafi walikuwa wakisema “sisi tuna machifu wengi, viongozi wengi na hata kabila letu lina watu wengi”. pia banu Sahm walikuwa wakisema hivyohivyo. Basi baada ya kuhesabu ikaonekana kweli Banu Abd Manafi wana watu wengi kwenye kabila lao. Baada ha yapo wakasema “twendeni tukahesabu makaburi ya watu wetu waliokufa. Hivyo wakayaendea makaburi hapo wakaata jibu kuwa Banu Saham ni wengi waliokufa kuliko Banu Abd Manafi.
Qatada amesema kuwa sura hii ilishuka kuwahusu Mayahudi waliosema “sisi ni wengi ssana kuliko wakina fulani na fulani ….., hivyo walikuwa wakiendelea na madai yao haya na kujisahau, kumuasi mungu hadi mauti anawafikia.
‹ Nyuma
› Endelea
‹ Books
‹ Apps ››
Umeionaje Makala hii.. ?
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid
Soma Zaidi...Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet
Soma Zaidi...Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain
Soma Zaidi...Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?
Soma Zaidi...FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.
Soma Zaidi...Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani
Soma Zaidi...