picha

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti

3.

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti

Namna ya kuiswali sala ya maiti

3. Kumswalia Maiti.

Masharti ya Swala ya Maiti.
- Kwa wenye kumswalia maiti, watekeleze masharti ya kawaida ya swala.
- Masharti ya maiti anayeswaliwa:
1. Maiti awe muislamu
2. Maiti iwe imeoshwa na kukafiniwa
3. Maiti iwekwe mbele ya wanaoisalia.


- Inajuzu kusalia maiti iliyo masafa ya mbali (swala ya ghaibu).
- Maiti zikiwa nyingi zipangwe mbele, za kiume zikiwa karibu na imamu kisha kusaliwa zote kwa pamoja.
oMaiti isiwe ya shihidi.
- Kwa mujibu ya Hadith ya Mtume (s.a.w), mashahidi hawaoshwi wala kusaliwa.



Nguzo za Swala ya maiti.
- Swala ya maiti inaswaliwa wima; haina rukuu, sijda wala kikao.
- Nguzo za swala ya maiti ni;
i.Nia
ii.Takbira ya kuhirimia
iii.Kusoma Suratul-Faatiha.
iv.Takbira ya Pili.
v.Kumswalia Mtume (s.a.w) kama tufanyavyo kwenye Tahiyyatu.
vi.Takbira ya Tatu.
vii.Kumuombea dua maiti.
viii.Takbira ya Nne.
ix.Kuombea dua waislamu wote, kisha kutoa Salaam.



Namna ya kutekeleza swala ya Maiti hatua kwa hatua.
Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo;
a)Maiti iwekwe mbele.
b)Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti ikiwa maiti ni ya kike, na usawa wa mabega kama maiti ni ya kiume.
c)Maamuma watasimama kwenye mistari (safu) kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, n.k.
d)Baada ya hapo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
i.Nia - ambayo ni kukusudia moyoni.
ii.Kuleta takbira ya kwanza; kwa kusema, “Allaah Akbar”
iii.Imamu na maamuma watasoma suratul-Faatiha – kimya kimya.
iv.Imamu ataleta Takbira ya Pili kisha maamuma – kimya kimya kwa maamuma na si lazima kuinua mikono wao.
v.Kumswalia Mtume (s.a.w) kama ilivyo katika Tahiyyatu, wote – kimya kimya.
vi.Imamu ataleta takbira ya Tatu kisha maamuma- kama walivyofanya awali.
vii.Wote kumuombea maiti dua kimya kimya, ikiwemo:


“Allaahumma ghfir lihayyinaa wamaayyitinaa washaahidinaa waghaaibinaa waswaaghirinaa wakaabirinaa wadhakirnaa waunthaanaa. Allaahumma man ahyaytahuu minnaa faahyi ‘alal Islaam. Waman tawaffaytahuu minnaa tawaffahuu ‘alal Imaani. Allaahumma laa tahirimnaa ajirahuu walaa taftinaa ba’adahuu”


Tafsiri:
“Ewe Allah tusamehe sisi, na maiti wetu, na mashahidi, na wasiokuwepo miongoni wetu, vijana wadogo miongoni mwetu na wakubwa miongoni mwetu, wanamume wetu, na wanawake wetu. Ewe Allah, yeyote yule miongoni mwetu utakayemewezesha kuishi, mjaalie aishi katika Kiislamu na yeyote miongoni mwetu utakayemfisha, mfishe katika Imani (ya Kiislamu). Ewe Allah, usitukatishe ujira kutoka kwake na wala usitufitinishe baada yake.”



- Au kwa kifupi tuweza kumuombea maiti kama ifuatavyo;
“Allaahumma ghfir lahuu warhamhuu wa-afihii wa-afu-anhu”
Tafsiri:
“Ewe Allah, Mghufirilie na Umrehemu”.



viii.Imamu ataleta Takbira ya nne na maamuma kufuatihia kama awali.
ix.Wote watawaombea waislamu dua – (pia si lazima kuleta dua hii).
Rejea Qur’an (59:10).



x.Imamu kutoa salaam na maamuma kufuatishia bila kutoa sauti kama ilivyo kwenye swala ya kawaida kwa kusema;
“Assalaamu ‘alaykum Warahmatullaah (Wabarakaatuh)”
Tafsiri:
“Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake”.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 5993

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo.

Soma Zaidi...
Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Soma Zaidi...