picha

Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani

Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani

(c) Mashariki ya kati



Uarabuni kabla ya Ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w) mwanamke alionekana kitu duni na nuksi kwa jamii. Baba akipewa habari ya kuzaliwa mtoto wa kike alijinyonga nyonga na kuhuzunika sana. Wanaume walikuwa wakitafuta kila njia ya kujiokoa na aibu hiyo ya kupata mtoto wa kike. Ilikuwa kuchagua moja katika njia mbili: Ama amzike binti huyo mzima mzima akiwa hai au aendelee kuishi maisha ya aibu na fedheha kwa kumbakisha hai.


Mara nyingine wanaume walikuwa wakiwalazimisha wake zao wanapoanza mwezi wa tisa wa ujauzito wa kuchimba shimo uvungni mwa kitanda. Shimo likiwa tayari mume anamuagiza mkewe: "Ukimzaa mtoto mwanake basi haraka sana mfukie mwenyewe katika shimo hii kabla sijaja." Qur'an inatufahamisha tabia ya Waarabu dhidi ya watoto wa kike katika aya zifuatazo:


Na mmoja wao anapopewa habari ya (kuzaliwa) mtoto wa kike, husawajika uso wake, akajaa sikitiko (akawa) anajflcha na watu kwa sababu ya ha bar mbaya ile aliyoambiwa (anafanya shauri) Je, akae nayejuu yafedheha hiyo au amfukie udongoni (akiwa hai). Sikilizeni! Ni mbaya mno hukumu yao hiyo. (1 6:58-59).



Wanawake baada ya kufiwa na waume zao, walirithiwa na wanawe wa kambo au shemeji zao. Walikuwa hawaruhusiwi kuolewa tena. Qur'an inakataza tabia hii kama ifuatavyo:


Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazuie (kuolewa na wanaume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhiya vile mlivyo wapa... (4:19).




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 1180

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 web hosting     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Soma Zaidi...
tarekh 02

FAMILIA YA MTUME (S.

Soma Zaidi...