Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.

Download Post hii hapa

Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti Uzazi
Miongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya. Viwanda vilihitaji wafanyakazi kwa maelfu ambao japo walifanyishwa kazi sana, sehemu kubwa ilikwenda kwa wenye viwanda, hivyo wafanyakazi hawakuweza kuzikimu familia zao. Bidhaa za viwandani pia zikabadili mahitaji ya watu. Vitu ambavyo hapo awali havikuwepo sasa vikawa ni mahitaji ya lazima.



Pili, kwa kuwa pato Ia mfanyakazi halikumwezesha kuihudumia familia yake, mke na watoto walilazimika pia kufanya kazi viwandani ili kupata riziki zao. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwa familia ziliparaganyika na yale malezi muhimu ambayo mtoto aliyapata kwa wazazi wake sasa yakakosekana. Kwa kuwa mke asingeweza kuishi bila kuajiriwa kiwandani na asingeweza kumudu zile kazi ngumu za kiwandani akiwa mjamzito au akiwa na mtoto mchanga, kuzaa kukaanza kuwa nuksi kubwa. Kwani kipindi chote ambacho mwanamke alishindwa kufanya kazi kwa sababu ya udhaifu wa afya hakulipwa kitu. Ndio maana kampeni hii ya kudhibiti uzazi ilianzishwa na kupiganiwa sana na wanawake. Kujiepusha na kuzaa kukaonekana kuwa ni ukombozi wa ama yake.



Tatu, mapinduzi hayo yaliambatana na utamaduni wake. Utamaduni ambao ulihimiza sana maendeleo na ustawi wa mtu binafsi. Ustawi kwa maana yakuwa na vitu vingi vya anasa na fahari. Matokeo yake yakawa watu walijiepusha sana na kila kitu ambacho walidhani kingeliweza kwa namna fulani kuathiri ustawi wao wa binafsi. Moyo wa ukarimu na kuhurumiana ukafa. Ikafikia hadi mtu akawaona wazazi wake kuwa ni mzigo mkubwa kuishi nao watampunguzia anasa zake. Kwa hoja hiyo kuzaa watoto kukawa balaa kubwa. Na aliyezaa akaishia mtoto mmoja au wawili.



Nne, kuparaganyika kwa familia kukapelekea kuondoka kwa uadilifu. Na hivyo uadilifu wa ndoa ukaonekana ni hekaya za watu wa kale. Badala yake falsafa za uhuru wa mtu binafsi zikapata nguvu. Kwa mujibu wa falsafa hiyo mtu anao uhuru wa kufanya analotaka na kazi ya serikali ni kuusimamia na kuudumisha uhuru huo. Hivyo kwa upande wa mahusiano ya ndoa falsafa hiyo iliona kuwa hilo ni suala Ia watu binafsi wanahiari ya kufanya lolote wapendalo. Na kampeni zote za kudhibiti uzazi katu hazijishughulishi kabisa na suala zima Ia uadilifu katika ndoa. Bali hujishughulisha tu na kuwasaidia watu wasipate mimba. Na kama tutakavyoona baadaye hii ni dosari mojawapo kubwa ya kampeni hii.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 725

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

 Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Waislamu wanaolazimika kufunga
Waislamu wanaolazimika kufunga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kusimamisha swala za Sunnah
Kusimamisha swala za Sunnah

Nguzo za uislamu, kusimamisha swala za Sunnah (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu
Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu

Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga.

Soma Zaidi...
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...