haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Download Post hii hapa

haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya Kutaliki
Katika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Kalika sheria ya Klislamu haki ya kutoa talaka iko kwa wote, mume na mke.


(a)Haki ya Mume kutoa talaka
Ilivyo katika kawaida ya maumbile mwanamume ndiye anayeanza kutoa posa au pendekezo Ia kuoana. Katika sheria ya Kiislamu, mwanamume pia ndiye anayepaswa kutoa mahari kumpa anayemtaka waoane, ndiye mwenye jukumu Ia kumlisha mkewe na kukidhi haja zake zote, na ndiye kiongozi wa familia. Kwa kuzingatia ukweli huu. Uislamu umempa haki ya kutoa talaka lakini iwe inapokuwa hapana budi na iwe ni kwa wema na kwa kutekeleza masharti yaliyowekwa na sheria.



(b)Haki ya mke kumwacha mumewe
Ndoa katika Qur-an imeelezwa kuwa lengo lake ni kuleta upendo na huruma kati ya mume na mke - (Rejea Qur-an, 30:21). Endapo mwanamke ataona sababu za msingi ambazo, zinaifanya ndoa yao isifikie lengo hili, mwanamke anapewa uhuru wa kudai talaka kwa mumewe. Mumewe akimkatalia, anaruhusiwa mwanamke kwenda mbele ya vyombo vya Sheria ya Kiislamu na kudai talaka. Itabidi mume alazimishwe kutoa talaka iwapo vyombo hivi vya sheria vitashindwa kuwasuluhisha. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kumtaliki mumewe bila hata ya kukubaliana naye au kupitia mahakamani. Inawezekana hivi kwa namna mbili:



(i)Kama tangu mwanzo, katika kufunga mkataba wa ndoa mume alikubaliana na mkewe kuwa atakuwa na uhuru wa kuvunja ndoa, endapo mume atamfanyia au atafanya jambo fulani asilolipenda; basi atakapovunja ahadi hiyo, mkewe atakuwa na uhuru wa kumwacha bila ya kudai talaka kwake au mahakamani. Kwa maana nyingine mwanamume tangu mwanzo katika mkataba wao wa ndoa, amempa mkewe haki ya kumtalakisha, endapo atafanya au atamfanyia jambo fulani asilolipenda. Talaka ya ama hii huitwa "Khul".



(ii)Kama katika mkataba wa ndoa, mwanamume alitoa haki yake ya "kutamka" talaka na kumpa mkewe ili kumpa uhuru na uwezo zaidi wa kuvunja mkataba wa ndoa endapo ataona haifikii lengo lake.



(c)Kuvunja ndoa kwa makubaliano ya mume na mke:
Wakati mwingine, mume na mke wote baada ya kuona kuwa hawaishi kwa maelewano kama ilivyotarajiwa, wana uhuru wa kukubaliana kuachana kwa wema. Mahakama ya Kiislamu haitaingilia kati, labda itokee kuvunjwa kwa sheria nyingine kutokana na kuachana kwao huko. Ama hii ya Talaka huitwa "Mubarat".



(d)Haki ya Mahakama ya Kiislamu katika kuvunja Ndoa
Wakati mwingine, hata bila ya makubaliano ya mume na mke, mahakama ya Kiislamu ma uwezo wa kuvunja ndoa. Kwa mfano talaka ya ama ya "Li'aan" husimamiwa na serikali.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1209

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...
Sunnah za udhu
Sunnah za udhu

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu sunah za udhu

Soma Zaidi...
maana ya Eda na aina zake
maana ya Eda na aina zake

Ni kipindi au muda wa kungojea mwanamke aliyepewa talaka (aliyeachwa) au kufiwa na mumewe kabla ya kuolewa na mume mwingine.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi

Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.

Soma Zaidi...
Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani
Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani

Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...