malezi ya mtoto mchanga baada ya talaka
Malezi ya Mtoto Mchanga baada ya Talaka
Mtoto mchanga hataachanishwa na mama yake mpaka awe na umri wa miaka miwili - umri wa kuacha kunyonya. Matumizi ya mama na mtoto katika kipindi hiki cha kunyonya mtoto yatakuwa juu ya mume japo mkewe aliyemtaliki atakuwa kwa wazazi wake au penginepo nje ya nyumbani kwake. Lakini mume na mke walioachana, wakiridhiana wanaweza kumwachisha kunyonya kabla ya miaka miwili au wanaweza kumkodisha mwanamke mwingine amnyonyeshe. Hukumu hii ya malezi ya mtoto baada ya mume na mke kuachana inabainishwa vyema katika Qur-an:
Na wanawake waliozaa wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili; kwa anayetaka kukamilisha kunyonyesha; na ni juu ya baba (yake) chakula chao (hao watoto na mama) na nguo zao kwa sheria. Wala haikalflshwi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya wasaa wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake, wala baba (asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake).
Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa (kabla ya miaka miwili), kwa kuridhiana na kushauriana, basi sio kosa juu yao. Na kama mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha (wengine wasiokuwa mama zao) basi haitakuwa dhambi juu yenu kama mkitoa (kuwapa hao wanyonyeshaji) mlichowaahidi kwa sharia. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyatenda. (2:233)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 ai web app 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.
Soma Zaidi...Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.
Soma Zaidi...Makosa Yanayofanywa Wakati wa Swala
Swala ni nguzo ya pili ya Uislamu baada ya Shahada na ni ibada ya kwanza ambayo mja atahisabiwa nayo Siku ya Kiyama. Kwa sababu ya umuhimu wake mkubwa, Muislamu anatakiwa kuiswali kwa usahihi kulingana na mafundisho ya Mtume Muhammad (Swalla Allahu Alayhi Wasallam). Hata hivyo, watu wengi hufanya makosa mbalimbali wakati wa swala, mengine kwa kutokujua na mengine kutokana na uzembe. Makosa haya yanaweza kupunguza thawabu za swala au hata kuifanya swala kuwa batili. Katika makala hii tutajifunza makosa ya kawaida yanayofanywa wakati wa swala, madhara yake, na namna ya kuyarekebisha.
Soma Zaidi...Milki ya raslimali katika uislamu
Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo.
Soma Zaidi...