HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU
Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu.
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU
Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu. Sumu inaweza kuwa katika vidonge, kimiminika, katika hali ya hewa ama kwenye sindano. Hapa nitazungumzia tu sumu inayoliwa na kuingia kwenye tumbo kwa njia ya mdomo. Sumu hii inawez akuwa ya panya am vidonge vya dawa.
Ukimuona mtu amekunywa ama kula sumu usimkimbie, na tambua kuwa anahitaji msaada wako. Kwanza angalia vyema hali yake na ukiwezekana ita msaada kwa haraka. Baad ya kufanya maamuzi kulingana na hali ya mgonwa unaweza kuanza kumpa huduma ya kwanza:
1.Mtapishe mgonjwa: kumtapisha mgonjwa ni katika njia nzuri na za haraka sana katika kupunguza athari za sumu. Unaweza kumtapisha mgonjwa kwa kumuingiza vidole mdomoni. Kama sumu ni ya kemikali mathalani amekunywa tindikali, njia ya kumtapisha sio njia sahihi.
2.Mpe maji mengi sana anywe. Kunywa maji mengi kutasaidia kupunguza makali ya sumu na kuiyeyusha kwenye maji.
3.Mpatie mgonjwa maziwa anywe. Unywaji wa maziwa uje baada ya kumtapisha. Usije mtapisha baada ya kumpa maziwa. Pia kama maziwa yapo usimpe maji mgonjwa.
4.Kama hali ya mgonjwa haijatengemaa, awahishe kituo cha afya kilicho karibu kwa haraka zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Utaratibu wa lishe kwa vijana
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana
Soma Zaidi...Madhara ya kunywa pombe kiafya
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kunywa pombe kiafya, ni madhara ambayo utokea kwa watu wanaokumywa pombe kwa kupita kiasi kwa hiyo wanapaswa kupunguza kunywa pombe baada ya kujua madhara yake.
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na minyoo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo
Soma Zaidi...Faida za seli
Posti hii inahusu zaidi faida za seli. Seli ni chembechembe hai za mwili ambazo hufanya kazi mbalimbali katika mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.
Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Soma Zaidi...