Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.w). Vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume mbali mbali.
“Kwa hakika tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha Vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu...” (57:25).
Vitabu vya Allah (s.w) ni vingi lakini tunavyovifahamu ni vile vilivyotajwa katika Qur-an kama ifuatavyo:
Suhufi kwa Ibrahimu (a.s)
Taurati kwa Mussa (a.s)
Zaburi kwa Daud (a.s)
Injili kwa Issa (a.s)
Qur-an kwa Muhammad (s.a.w)
Lengo la kushushwa Vitabu vya Allah (s.w)Iimebainishwa wazi katika Qur-an kuwa vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume wake ili kuwaongoza wanaadamu katika njia iliyonyooka. Njia iliyonyooka ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake kwa kipindi chote cha uhai wake hapa ulimwenguni. Allah (s.w) amechukua ahadi ya kuwaletea watu mwongozo tangu awali pale alipowashusha wazazi wetu, Adamu (a.s) na mkewe (Hawwah) hapa ardhini kama tunavyojifunza katika Qur-an:
“Tukasema, shukeni humo nyote, na kama ukikufikieni uw ongozi utokao kw angu, basi w atakaoufuata uw ongozi wangu huo haitakuwa hofu juu yao wala haw atahuzunika.
Lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa Motoni, humo watakaa milele”. (2:38-39).
Ahadi hii ameitekeleza Allah (s.w) kwa kuwaleta Mitume mbali mbali baada ya Adamu (a.s) na kuwashushia vitabu vyenye Uongozi na nuru. Qur-an inasisitiza:
“Hakika tuliteremsha Taurat yenye Uongozi na Nuru..” (5:44)
“Na tukawafuatishia (Mitume hao) Issa bin Maryam kuyahakikisha yaliyokuwa kabla yake katika Taurat, na tukampa Injili iliyomo ndani yake Uongozi na nuru.” (5:46 )
“Ni mw ezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa katika (mwezi) huo (hii) Qur-an ili iwe Uongozi kwa watu na hoja zilizo wazi za Uongozi wa upambanui
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)
Soma Zaidi...Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.
Soma Zaidi...(v)Kuwaombea dua wazazi.
Soma Zaidi...Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.
Soma Zaidi..."Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu
Soma Zaidi...