Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Semeni nyinyi (Waislamu kuwaambia Mayahudi na Wakristo kuw a): “Tumemw amini Mw enyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu, na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutafautishi baina ya yoyote katika hao.
(Wote tunawaamini), na sisi tumenyenyekea kwake.” (2:136)Kuamini baadhi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu na kuwakanusha wengine kama walivyo fanya mayahudi na Wakristo ni Ukafiri kama tunavyojifunza katika Qur-an:
“Hakika wale wanaomkanusha Mwenyezi Mungu na Mitume yake, na wanataka kutenga baina ya Mwenyezi Mungu na Mitume yake, kwa kusema: “Wengine tunawaamini na wengine tunawakataa, ” na wanataka kushika njia iliyo kati kati ya haya (si ya Kiis lam u kh as a w ala y a Kikafiri).
Hao ndio Makafiri kweli.Na tumewaandalia makafiri adhabu idhalilishayo.(4:150-151).
Na waliomwamini Mwenyezi Mungu na Mitume yake wala wasimfarikishe yoyote katika wao (bali wamewaamini wote), hao atawapa ujira wao. Na Mw enyezi Mungu ni Mw ingi w a kusamehe (na) Mw ingi wa kurehemu.” (4 :152).
“Na kwa yakini tuliwatuma mitume kabla yako (Muhammad). Wengine katika hao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia...” (40:78)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu
Soma Zaidi...Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.
Soma Zaidi...Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.
Soma Zaidi...Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.
Soma Zaidi...Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.
Soma Zaidi...Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...