Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?

Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?

Download Post hii hapa

Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?

Mwisho wa Utume



Maswali ambayo huweza kuulizwa ni: Kwa nini wahyi ukatike? Kwa nini Mitume wasiendelee kuletwa hadi kiyama? Kwa nini Muhammad (s.a.w) afunge mlango wa Utume?
Ili kulielewa vizuri suala hili la mwisho wa Utume yafaa kwanza tuzingatie kuwa kilicho muhimu na cha msingi kabisa kwa Mtume yeyote si kule kuwepo kimwili bali ni kule kuufikisha kwake ujumbe aliopewa na Mwenyezi Mungu (s.w) ili watu wake wasiwe na hoja tena iwapo watachagua kupotea.


Na lau ingekuwa lililo muhimu kwa Mtume ni kule kuwapo kimwili basi Mwenyezi Mungu angelimpeleka Mtume mara tu baada ya kufariki Mtumealiyetangulia. Kilicho cha msingi ni mafundisho aliyokuja nayo. Maadamu ujumbe aliouleta uko hai basi Mtume huyo yu hai. Hivyo kifo halisi cha Mtume ni kule kupotea kwa mafundisho aliyoyaleta. Mitume wote waliomtangulia Muhammad (s.a.w) mafundisho yao yalipotea, kwani yalichanganyika na hekaya mbali mbali. Katika vitabu vilivyoitangulia Qur-an, kwa mfano Taurat, Injil, na Zaburi hakuna hata kimoja ambacho kipo katika hali ya usahihi wake wa asili. Hata wafuasi wa vitabu hivyo wanakiri kuwa nakala walizonazo leo si zile walizopewa Mitume. Si hivyo tu bali hata historia za maisha ya Mitume waliomtangulia Muhammad (s.a.w) zimechanganywa na ngano za kushtusha kabisa, hata inakuwa vigumu kupambanua haki na batili.


Kinyume chake mafundisho aliyokuja nayo Muhammad (s.a.w) yako hai kabisa na hayajaharibiwa na katu hayawezi kuharibiwa. Qur-an, kitabu alichoteremshiwa kipo tena katika lugha ile ile ya asili bila ya kupunguza wala kuzidisha japo nukta moja. Historia kamili ya maisha yake, maneno yake, maagizo yake, vitendo vyake, vyote vimehifadhiwa kwa usahihi kabisa kiasi ambacho karne 14 zimepita lakini bado historia yake ni ya wazi na kamili kama kwamba tunamuona kwa macho yetu. Katika kila kipengele cha maisha yetu tunaweza kupata muongozo na mafundisho kutoka kwa Muhammad (s.a.w). hii ndio sababu hakuna haja ya kuletwa Mtume mwingine baada yake.
Zaidi ya hayo yapo mambo matatu ambayo husababisha kuhitajika kuja kwa Mtume mwengine baada ya yule aliyetangulia:



(1)Iwapo mafundisho ya Mtume aliyetangulia yamechanganywa na hekaya za nzushi, kuharibiwa na kupotea. Katika hali kama hiyo Mtume anahitajika ili aje aifundishe dini katika usahihi wake wa awali.



(2)Iwapo mafundisho ya Mtume aliyeondoka hayakukamilika na hivyo kukawa na haja ya kuyakamilisha, kuyarekebisha, au kuongeza jambo fulani.



(3)Iwapo Mtume aliyetangulia alipelekwa kwa watu wa taifa fulani maalum au nchi fulani maalum na hivyo kuwepo haja ya kuletwa Mtume kwa watu wa taifa au nchi nyingine. Au pengine Mtume anaweza kuletwa ili amsaidie Mtume mwingine, lakini kwa kuwa hii si kanuni ya kawaida, hatujaita kama sharti la nne. Katika Qur-an ipo mifano miwili ya hali kama hiyo. Nabii Haruni (a.s) alikuwa msaidizi wa Nabii Musa (a.s). Nabii Lut (a.s) Ismail (a.s) na Is-haq (a.s) walikuwa wasaidizi wa Nabii Ibrahim (a.s).
Haya matatu ndiyo masharti makuu ya kimsingi yanayohitajika ili aletwe Mtume mwingine. Kati ya hayo hakuna hata sharti moja lililopo leo. Kwanza mafundisho ya Mtume wa mwisho, Muhammad (s.a.w) yako hai, yamehifadhiwa na yatadumu hadi siku ya Kiyama. Mwongozo aliouleta kwa walimwengu wote ni sahihi na kamili na umehifadhiwa katika Qur-an humo kuna ahadi ya ulinzi wa Allah (s.w) kama tunavyofahamishwa:


“Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha (haya hii Qur-an); na Hakika sisi ndio tutakaoyalinda.” (15:9).
Pia sunnah zake zimehifadhiwa kikamilifu kiasi ambacho mtu anaweza kujua pasi na shaka yoyote nini mafundisho ya Mtume juu ya jambo fulani. Hivyo sharti la kwanza linaondoka.
Pili, Mwenyezi Mungu amekamilisha mwongozo wake kwa Nabii Muhammad (s.a.w) na hivyo Uislamu ni dini kamilifu kwa ulimwengu wote. Allah (s.w) anasema katika Qur-an:


“… Leo nimekukamilishieni dini yenu, na kukutimizieni neema yangu juu yangu na nim ekupendeleeni Uis lam u uw e dini yenu … (5:3)




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2007

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Nguzo za imani
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...
Aina kuu za dini
Aina kuu za dini

Katika kipengele hichi tutajifunza aina kuu mbili za dini.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nafasi ya  Elimu katika uislamu
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu?

Soma Zaidi...