Ingawa hakuna ajuaye Kiyama kitakuwa lini, kupitia Aya mbali mbali za Qur’an na Hadith kadhaa za Mtume (s.a.w) zinabainisha kwa uwazi juu ya dalili mbali mbali za kusimama kwa kiyama. Ziko Dalili kubwa na Dalili ndogo, na zipo ambazo tayari zimekwishadhihiri nyingine zinaendelea na ambazo bado kudhihiri kwake; Kama Allah Aliyetukuka anavyotubainishia:
“Kwani wanangoja jingine ila kiyama kiwajie kwa ghafla? Basi alama zake(hicho kiyama) zimekw ishakuja. Kutaw afaa w api kukumbuka wakati kitakapow ajia ? ” (47:18)
Pia anasema“Saa ya Kiyama imekaribia; na mwezi umepasuka” (54 :1)
Dalili Ndogo za Kiyama:
(i)Watu kumiliki mali na hali ya kuwa ni madhalimu wasio na uadilifu
(ii)Kuenea mno kwa riba kiasi cha kila mtu kuathiriwa nayo
(iii)Kuenea kwa kila aina ya Ulevi
(iv)Wanawake kukithiri katika kuvaa nguozinazochochea zinaa (nguo nyepesi za kuangaza , fupi na za kubana)
(v)Wanawake watawaiga wanaume katika mavazi kadhalika wanaume watawaiga wanawake katika mavazi. Leo wanaume wanavaa hereni, shanga, bangili, na mengineyo yanayojulikana kuwa mapambo ya kike.
(vi)Kuenea kwa Liwati (kujimai baina ya jinsia moja-wanaume kuwaendea wanaume wenzao na wanawake kuwaendea wanawake wenzao) Homosexuality and Lesbiansm. Jambo hili leo limehalalishwa na watu wa Magharibi, pia hapa kwetu Afrika na hasa Kenya na Afrika kusini ni halali Mwanaume kuolewa na mwanamume mwenzake! Subhaanallah!
(vii)Kuenea sana kwa zinaa na itafanyika hadharani.
(viii)Watu hawatawajali tena wazazi wao, ndugu zao najamaa zao badala yake watawathamini nakuwasaidia rafiki zao.
(ix)Watu watachukia sana kulea watoto.
(x)Unafiki utaenea sana.
(xi)Mauaji yataenea sana, kwa kutoka Taifa mojakwenda kulivamia Taifa jingine na watu baadhikuwaua wengine kwa maslahi yao binafsi
(xii)Watu wataona uzito sana kutoa sadaka
xiii)Watawala watakuwa wengi sana lakini hakuna atakayekuwa mkweli na mwadilifu
xiv)Mtu ataheshimiwa kwa shari yake na si kwa uadilifu na wema wake.
xv)Kujifaharisha kwa misikiti
xvi)Pamoja na haya yote, bado kutakuwepo na kundi dogo tu la waislamu ambalo litadumu katika njia iliyonyooka na halitatetereka kwa lolote.
Umeionaje Makala hii.. ?
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.
Soma Zaidi...Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.
Soma Zaidi...Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.
Soma Zaidi...Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.
Soma Zaidi...Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.
Soma Zaidi...Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...