Mtume (s.a.w) pia ametutajia dalili kubwa za kukaribia kwa siku ya Mwisho. Dalili hizo zinapatikana katika Qur’an na Hadith kama inavyobainishwa hapa chini:“Na kitakapokaribia Kiyama, tutawatolea mnyama kutoka ardhini atawaeleza (watu) kwa kuwa watu walikuwa hawaziamini aya zetu” (27:82)“Mpaka watakapofunguliwa Ya’juj na Ma’juj nao wataporomoka kwa kasi, na ikakaribia ahadi ya kweli kufunguliwa, hesabu na malipo, basi wakati huo macho ya makafiriyatatokeza mno juu ” (21:96 – 97)
Katika hadith aliyoipokea Imam Ahmad, na kusimuliwa na Khudhaifa Ibn Usaid Al – Ghifaar (r.a) amesema; Alitutokea Mtume (s.aw) kutoka chumbani kwake na sisi tukikumbushana jambo la kiyama, Mtume (s.a.w) akasema: Hakitosimama Kiyama mpaka muone alama kumi,
1. Kuchomoza jua Magharibi
2. Kutokea moshi mkubwa utakaochafua mazingira (pollution)
3. Mnyama atatokeza na kuwasemesha watu (27:82)
4. Kufunguliwa Ya’juj na Ma’juj (21:96 97)
5. Kurudi kwa Issa mwana wa Maryam
6.Kuja kwa Masih Dajal (False Messayah)
7.Kutoka Moto (Volcano) katika pango la Aden ukiwaendesha watu
8.Dunia kugawika mapande matatu (Three Blocks); Pande la Mashariki (Eastern Block)
9.Pande la Magharibi na (western block)
10.Bara Arab (Mashariki ya kati - Middle East)
Kwa hakika Qur’an imetaja dalili nyingi mno, Rejea Suratul qiyaamah (75:6 – 9) na nyinginezo nyingi zilizotajwa katika hadith mbali mbali.
Kuamini siku ya mwisho ni kuamini kuwa kuna maisha ya milele baada ya maisha haya ya hapa duniani. Kwa mujibu wa mafundisho ya Qur-an, maisha hayo yatakuwa na hatua kuu nne zifu atazo:
(i)kutokwa na roho
(ii)Maisha ya kaburini - Barzakh.
(iii)Kufufuka na kuhudhurishwa mbele ya Allah (s.w) na kuhesabiwa.
(iv)Maisha ya kukaa Peponi milele kwa watu wema au kukaa motoni kwa watu waovu.Aidha kwa kuzingatia matukio yatakayotokea katika hatua nne za maisha yajayo,
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.
Soma Zaidi...Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...“Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.
Soma Zaidi...Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.
Soma Zaidi...Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.
Soma Zaidi...