Mtume (s.a.w) pia ametutajia dalili kubwa za kukaribia kwa siku ya Mwisho. Dalili hizo zinapatikana katika Qur’an na Hadith kama inavyobainishwa hapa chini:“Na kitakapokaribia Kiyama, tutawatolea mnyama kutoka ardhini atawaeleza (watu) kwa kuwa watu walikuwa hawaziamini aya zetu” (27:82)“Mpaka watakapofunguliwa Ya’juj na Ma’juj nao wataporomoka kwa kasi, na ikakaribia ahadi ya kweli kufunguliwa, hesabu na malipo, basi wakati huo macho ya makafiriyatatokeza mno juu ” (21:96 – 97)
Katika hadith aliyoipokea Imam Ahmad, na kusimuliwa na Khudhaifa Ibn Usaid Al – Ghifaar (r.a) amesema; Alitutokea Mtume (s.aw) kutoka chumbani kwake na sisi tukikumbushana jambo la kiyama, Mtume (s.a.w) akasema: Hakitosimama Kiyama mpaka muone alama kumi,
1. Kuchomoza jua Magharibi
2. Kutokea moshi mkubwa utakaochafua mazingira (pollution)
3. Mnyama atatokeza na kuwasemesha watu (27:82)
4. Kufunguliwa Ya’juj na Ma’juj (21:96 97)
5. Kurudi kwa Issa mwana wa Maryam
6.Kuja kwa Masih Dajal (False Messayah)
7.Kutoka Moto (Volcano) katika pango la Aden ukiwaendesha watu
8.Dunia kugawika mapande matatu (Three Blocks); Pande la Mashariki (Eastern Block)
9.Pande la Magharibi na (western block)
10.Bara Arab (Mashariki ya kati - Middle East)
Kwa hakika Qur’an imetaja dalili nyingi mno, Rejea Suratul qiyaamah (75:6 – 9) na nyinginezo nyingi zilizotajwa katika hadith mbali mbali.
Kuamini siku ya mwisho ni kuamini kuwa kuna maisha ya milele baada ya maisha haya ya hapa duniani. Kwa mujibu wa mafundisho ya Qur-an, maisha hayo yatakuwa na hatua kuu nne zifu atazo:
(i)kutokwa na roho
(ii)Maisha ya kaburini - Barzakh.
(iii)Kufufuka na kuhudhurishwa mbele ya Allah (s.w) na kuhesabiwa.
(iv)Maisha ya kukaa Peponi milele kwa watu wema au kukaa motoni kwa watu waovu.Aidha kwa kuzingatia matukio yatakayotokea katika hatua nne za maisha yajayo,
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi.
Soma Zaidi...Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.
Soma Zaidi...(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.
Soma Zaidi...Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.
Soma Zaidi...Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.
Soma Zaidi...Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu.
Soma Zaidi...