Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama




Mtume (s.a.w) pia ametutajia dalili kubwa za kukaribia kwa siku ya Mwisho. Dalili hizo zinapatikana katika Qur'an na Hadith kama inavyobainishwa hapa chini:'Na kitakapokaribia Kiyama, tutawatolea mnyama kutoka ardhini atawaeleza (watu) kwa kuwa watu walikuwa hawaziamini aya zetu' (27:82)'Mpaka watakapofunguliwa Ya'juj na Ma'juj nao wataporomoka kwa kasi, na ikakaribia ahadi ya kweli kufunguliwa, hesabu na malipo, basi wakati huo macho ya makafiriyatatokeza mno juu ' (21:96 ' 97)
Katika hadith aliyoipokea Imam Ahmad, na kusimuliwa na Khudhaifa Ibn Usaid Al ' Ghifaar (r.a) amesema; Alitutokea Mtume (s.aw) kutoka chumbani kwake na sisi tukikumbushana jambo la kiyama, Mtume (s.a.w) akasema: Hakitosimama Kiyama mpaka muone alama kumi,



1. Kuchomoza jua Magharibi



2. Kutokea moshi mkubwa utakaochafua mazingira (pollution)



3. Mnyama atatokeza na kuwasemesha watu (27:82)



4. Kufunguliwa Ya'juj na Ma'juj (21:96 97)



5. Kurudi kwa Issa mwana wa Maryam



6.Kuja kwa Masih Dajal (False Messayah)



7.Kutoka Moto (Volcano) katika pango la Aden ukiwaendesha watu



8.Dunia kugawika mapande matatu (Three Blocks); Pande la Mashariki (Eastern Block)



9.Pande la Magharibi na (western block)



10.Bara Arab (Mashariki ya kati - Middle East)
Kwa hakika Qur'an imetaja dalili nyingi mno, Rejea Suratul qiyaamah (75:6 ' 9) na nyinginezo nyingi zilizotajwa katika hadith mbali mbali.
Kuamini siku ya mwisho ni kuamini kuwa kuna maisha ya milele baada ya maisha haya ya hapa duniani. Kwa mujibu wa mafundisho ya Qur-an, maisha hayo yatakuwa na hatua kuu nne zifu atazo:



(i)kutokwa na roho



(ii)Maisha ya kaburini - Barzakh.



(iii)Kufufuka na kuhudhurishwa mbele ya Allah (s.w) na kuhesabiwa.



(iv)Maisha ya kukaa Peponi milele kwa watu wema au kukaa motoni kwa watu waovu.Aidha kwa kuzingatia matukio yatakayotokea katika hatua nne za maisha yajayo,





                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1058


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)
Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya vitani
Soma Zaidi...

Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal
Soma Zaidi...

KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' '?... Soma Zaidi...

ukweli na sifa zake kwenye uislamu na sifa za mtu mkweli
Ukweli ni uhakika wa jambo. Soma Zaidi...

mitume
Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI
'Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu
Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i'rab ( '). Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)
SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s. Soma Zaidi...