Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.

Katika somo hili la nne tutakwenda kujifunza mambo makuu matatu ambayo ni:-

  1. Kubadili jina la database
  2. Kufuta database
  3. Kutumia SQL kufanya mabo hayo yaliyotajwa juu na mengineyo.

 

Kama ulishiriki mafunzo katika somo la tatu ulijifunza namna ya kutengeneza database kwa kutumia MySQL na kwa mutumia SAL command. Sasa katika somo hili tutakwenda kutumia database zetu mbili ambazo tulizitengeneza katika somo la tatu.

 

1. Kuona orodha ya database:

Hili ni jambo rahisi tu, baada ya kuingia kwenye MySQL, angalia menu yako, kisha bofya databases hapo utaona orodha ya database zote ambazo umetengeneza.

 

Sasa tunataka kufanya kitu kama hicho cha kuona orodha ta database kwa kutumia SQL language. Kufanya hivi fuata hatuwa hiz:-

  1. Kwenye menu bofya SQL
  2. Utakuja uwanja wa kuandika SQL hapo tumia command hii
  3. SHOW DATABASES;
  4. Baada ya hapo bofya neno GO lipo kwa chini pande wa kulia
  5. Kumbuka kuwa katika kuandika SQL mwisho tunamalizia na hizo semicolon (;) kama ilivyo hapo juu.
  6. Baada ya hapo utaona orodha ya database zote ulizotengeneza.

 

2. Kutumia database

Baada ya kuona orodha ya database zote hatuwa inayofata ni kuitumia hiyo database ama hizo database. Kutumia database maana yake ni kufanya hicho ambacho ulikusudia kwenye hiyo database kwa mfano kufuta, kubadili jiana ama kuweka data ama kuondoa na kubadili.

 

Kufanya hivi kwenye MySQL pia ni rahisi sana, unachotakiwa kufanya ni kubofya hiyo database yako. Ukishaubofya utaona umefunguka na kama kuna taarifa utaanza kuona majedwali yaliyopo.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL pia ni rahisi, fuata hatuwa zifuatazo:-

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Andika command hii
  3. USE post;
  4. Baada ya hapo bofya neno GO
  5. Command yetu hapo ni USE na hiyo post ni database ambayo tayari ipo hivyo tunataka kuitumia. Command hiyo ni maneno ya kiingereza yanayoweza kufahamika kuwa ni kuiambai MySQL kutumia database inayoitwa post.
  6. Mpaka kufika hapo utakuwa tayari kutumia database hiyo na unaweza kuifanya unachotaka.

 

3. Kubadili jina la database

Kwa kutumia MySQL baada ya kubofya hiyo database angalia kwenye menu tafuta neno oprrations, bofya hapo. Kisha tafuta palipoandikwa rename database to chini ya maneno hayo utaona kuna kabox. Kwenye hako kabox utaweka jina ambalo unataka kubadili. Kwa mfano database yetu inaitwa post sasa tunataka kuibadili jina kuiita makala.

 

Hivyo ingiza kwenye hicho kibox jina makala kisha bofya neno GO lipo upande wa kulia.kuna ujumbe utakuja unasema CREATE DATABASE makala / DROP DATABASE post hapo  utabofya OK kukubali. Mpaka kufikia hapo utakuwa umemaliza kubadili jina na hapo database yako itakuwa imebadilika.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL utatumia RENAME ila kwa sasa hatutajifunza kufanya hivi ni kwa sababu command hii iliondolewa kwenye MySQl kwa sababu za kiusalama. Hivyo utaendelea kutumia MySQL interface kubadili jina.

 

4. kufuta database

Kufuta database kwenye MySQL utakwenda kwenye operations kama ulivyofanya hapo juu. Kisha tafuta palipoandikwa Remove database chini ya hayo maneno utaona kuna maneno yanasomeka Drop the database (DROP) bofya hayo maneno kisha kuna ujumbe utakuja You are about to DESTROY a complete database! Do you really want to execute "DROP DATABASE `makala`"? hapo bofya OK kukubali. Kufikia hapo utakuwa umeifuta database yako na hutoweza kuirudisha tena lamda iwe umeshaifanyia backup.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL fuata taratibu zifuatazo. Kwa kuwa database ya makala tumeifuta basi sasa tunakwenda kufuta ile ya mafunzo.

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Andika command hii
  3. DROP DATABASE mafunzo;
  4. Kisha bofya GO
  5. Hapo database ya mafunzo itakuwa imesha futika.

 

Kwa ufupi command ambazo zimetumika kwenye somo hili ni

  1. Show databases hii ni kwa ajili ya kuona orodha ya databases
  2. Use hii umetumika kutumia database
  3. Drop database hii imetumika kufuta database
  4. Create database hii imetumika kutengeneza database

 

Tukutane somo la tano tutakapojifunza Type of data in MySQL somo hili litakuwa ni muhimu sana na ni msingi hasa wa somo la sita. Pia kwa wale abao wanahitaji kujatumia database zao vilivyo wanatakiwa walifahamu vyema somo la tano.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya

Bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021/11/17/Wednesday - 09:33:29 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1042


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Muda wa kuchaji simu yako
Posti hii itakwenda kukujuza juu ya kuda mzuri wa kuchaji simu yako Soma Zaidi...

Sababu za simu kusumbua mtandao
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sabau za simu kusumbua mtandao Soma Zaidi...

Yanayoathiri betri yako
Somo hili linakwenda kukuletea mambo yanayo athiri betri lako Soma Zaidi...

Buibui hupuruka ijapokuwa hana mbawa.
Nataka nikufundishe moja katika maajabu ya mdudu Buibui kwa lugha ya kimombo spider. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1
Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...

Timu ya simba ina miaka 87 sasa toka kuanzishwa
Kutokea kuitwa Sunderland mpaka Simba, timu hii ilianzishwa mwaka 1936 Soma Zaidi...

Cheetah
Posti hii inakwenda kukupa sifa za mnyama cheetah Soma Zaidi...

Nini chanzo cha tatizo la computer au simu yako
Posti hii inakwenda kukupa elimu kuhusu chanzo cha tatizo la computer au simu yako Soma Zaidi...

CONTACT US
Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa pesa ClipClaps kwa Tanzania
Njia za kutoa pesa ClipClaps Soma Zaidi...

Mafunzo ya html level 2 (html full course for beginners)
haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu. Soma Zaidi...