picha

dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba

Jifunze namna ya kuthibitisha dalili za ujauzito kuwa ni za kweli. Tambuwa namna ya kupima mimba na muda mujarabu wa kupima

dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba



JE NITAHAKIKISHA VIPI KAMA NINA UJAUZITO?




Hili ni swali la msingi kabisa, maana unaweza kuwa na dalii za ujauzitio lakini si ujauzito, ama unaweza kuwa ujauzito lakini ukipima huoni kitu. Sasa nini tufanye. Njia pekee ya kuhakiki kama ni ujauzito ama sio ni kupima. Unaweza kutumia kipimo cha mkojo ukiwa nyumbani ama kwenda kupima hospitali.



Kama utatumia kipimo cha mkojo fika duka la dawa na hakikisha unapewa kipimo kilichokuwa hakiku expire. Pata maelekezo kutoka kwa uuzaji kama ni mara yako ya kwanza. Pia maelekezo utaweza kuyakuta kwenye hiko kipimo ila lugha inaweza usielewe. Kipimo hili kinafanya kazi kwa kuangalia uwepo wa kemikali ambazo huzaliwa wakati wa ujauzito. Endapo zitakuwepo kipimo kitaonyesha kuwa ni mjamzito.



Sasa ni muda gani unafaha kupima?
Ni vyema kupia wiki mbili baada ya kukosa hedhi. Endapo utapima wiki moja baada ya kukosa hedhi ama utapima mapema zaidi kuna uwezekano kuwa hutapata majibu kama ni mjamzito. Hivyo inashauriwa sana kusubiri baada ya wiki mbili toka kukosa hedhi ndipo upime. Kama utakwenda kupima hospitali haina shida hata ukiwahi maana zipo njia nyingi wanaweza kutumia.



Nina dalili za uajauzito lakini nikipima sina?
Hili ni katika maswali ambayo wanawake wengi wamekuwa wakiuliza. Inatokea anazo dalili zote za ujauzito lakini akipima hakuna kitu. Kuna sababu nyingi juu ya swala hili. Kabla ya kuendelea na somo hili zaidi, wacha nikufahamishe kuwa, yafuatayo yanaweza kusababisha usione ujauzito kwenye kipimo:-



1.Kama umepima mapema kabisa
2.Kama kipimo ni kibovu
3.Kama umekosea namna ya kupima
4.Kama huna ujauzito
5.Homoni za ujauzito hazipo za kutosha kwenye mkojo.



Hizi ni katika sababu tu zinazotokea hasa wakati wa kupima. Sasa wacha tuingie katika somo hili kitaalamu zaidi. Ni kwa nini unaweza kupata dalili za uajauzitio zilizotaja hapo juu lakini ukipima huna hata ujauzito?. nitaangalia hoja kuu tano za kutokea kwa hali hizi kama ifuatavyo:-



1.Kukosa Hedhi
Kukosa hedhi ni dalili ya ujauzito, lakini haimaanishi kuwa ni lazima utakuwa mjamzito. Kwani mwanamke anaweza kukosa hedhi kwa moja ya sababu zifuatazo:-
A.Uwiyano usiosawa wa homoni (hormene imbalance)
B.Madawa
C.Maradhi katika ovari
D.Magonjwa kama ya PID
E.Misongo ya mawazo
F.Vyakula
G.Njia za uzazi wa mpango



2.Kuuma kujaa na kuvimba kwa matiti. Hii inaweza kuwa ni dalili ya ujauzito.akini pia hali hii inaweza kusababishwa na mambo kadhaa ambayo yanaweza yakakufanya uhisi ni mjamzito.kwa mfano:-
A.Kuwepo kwa uvimbe kwa ndani (breast sore)
B.Kuwepo kwa shida katika tishu za matiti (fibrocystic breast tissue)
C.Kwa wakati mwingine mazoezi makali yanaweza kusababisha hali hii.
D.Uvutaji wa sigara
E.Pia uwiyano mbaya wa homoni (hormone imbalany)



3.Maumivu ya kichwa na kichefuchefu yanaweza kusababishwa pia na sababu nyingine. Ijapokuwa inakadiriwa kuwa asilimia 70 ya kichefuchefu ni ujauzito. Mengine yanayoweza kusababisha ni misongo ya mawazo, vyakula, maradhi na vidonda vya tumbo, sumu katika vyakula na mengineyo.



4.Maumivu ya tumbo na kutokwa na damu kidongo (cramping and spotting). dalili hizi zinawezakufana na sana na mwanzoni mwa hedhi, dalili hizi hazimaanishi moja kwa moja utakuwa na ujauzito. Kwani huwenda pia zikasababishwa na uwiyano mbaya wa homoni (hormone imbalance), matumizi ya baathi ya njia za uzazi wa mpango, matumizi ya madawa, misongo ya mawzo, mashambulizi ya bakteria mwilini (PID) na maradhi yanayojulikana kama uterine fibrinoid.



5.Uchovu, nadhani hapa sina haja ya kuzungumza sana maana kila mtu anafahamu kuwa uchovu unaweza kusbabishwa na mambo mengi sana kama mazoezi, kazi, maradhi mengine.



Hivyo kama unapata dalili za ujauzito na kila ukipima hakuna kitu vyema kufika kituo cha afya kwenda kucheki vyema huwenda kuna kitu haki[o sawa.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 5356

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Soma Zaidi...
Mimi ni mama ninaye nyonyesha toka nimejefunguwa sijawai kuziona siku zangu lakini nilipo choma sindano za yutiai nikaaza kutokwa na tamu kama siku tano na mwanangu ana mwaka moja je ninahatali ya kubeba mimba

Kunyonyesha ni moja katika njia za asili za kuzuia upatikanaji wa miba nyingine. Hata hivyo hii haimaanishi kuwa huwezi kupata mimba ukiwa unavyonyesha.

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa jamii

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii.

Soma Zaidi...
Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba

Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.

Soma Zaidi...
Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.

Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n

Soma Zaidi...
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito

Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.

Soma Zaidi...
Namna ya kutibu ugumba kwa Mwanaume.

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.

Soma Zaidi...
Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake

Soma Zaidi...