Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;
i. Muzabanah
- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).
ii. Mu’awamah
- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.
iii. Hablul-Habalah
- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.
iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.
Ibn Abbas (r.a) ameeleza:
“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka
yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)
v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.
vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.
Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.
(Muslim)
vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.
viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.
ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.
x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.
xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.
“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)
xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.
xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.
Rejea Qur’an (2:276-279)
xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.
Rejea Qur’an (5:90-91)
xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.
Bidhaa Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;
i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k
iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.
Soma Zaidi...Post hii itakufundishabkuhusu mirathi ya kiislamu, maana yake.
Soma Zaidi...Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.
Soma Zaidi...(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha
Soma Zaidi...