4.
4.2 Sheria Katika Uislamu
? Maana ya Sheria
Kilugha: njia ya Kufuata
Kimatumizi: ni taratibu, sharti, kanuni na amri zilizowekwa kuongoza jamii.
Kazi ya Sheria katika Jamii
i. Kulinda binaadamu binafsi dhidi ya madhara mbali mbali ya mwenendo wake mbaya.
ii. Kulinda na kuhifadhi maisha ya watu na mali au rasilimali zao kutokana na kuuliwa, kujeruhiwa, kuharibiwa, kuibiwa, n.k bila sababu ya msingi.
iii. Kuhifadhi na kulinda amani na usalama katika jamii kutokana na migongano, vurugu, n.k.
iv. Kuhifadhi na kulinda maadili ya jamii kama njia ya msingi ya kumbakisha mwanaadamu katika mwenendo mema.
v. Kuweka na kupanga utaratibu wa namna ya kuendesha shughuli na maisha ya kila siku kibinafsi na kijamii.
vi. Sheria ya Kiislamu ina kazi ya kulinda na kuhifadhi misingi mitano ya mwanaadamu ambao ni; imani, uhai, akili, heshima na hadhi na mali.
Chimbuko la Sheria za Kitwaghuti
- Zimetungwa na binaadamu kwa kutumia vipawa vya akili, elimu, mila, desturi, uzoefu, mazingira na matashi ya nafsi zao.
- Katiba ndio msingi (chombo) mkuu wa sheria za Kitwaghuti ambayo hugawanya utekelezaji wake katika vyombo vikuu vitatu;
1. Bunge (Legislature) โ chombo kikuu cha kutunga sheria
2 Serikali (Executive) โ chombo kikuu cha utendaji
3 Mahakama (Judiciary) โ chombo kikuu cha kutafsiri sheria na kutoa haki.
Udhaifu wa Sheria za Kitwaghuti
- Pamoja na mwanaadamu kupewa na vipawa vya akili, ujuzi, elimu, n.k bado ana madhaifu mengi kama ifuatayo;
i. Mwanaadamu ana ujuzi wa mambo machache sana juu ya ulimwengu na yale yanayomzunguka.
Rejea Qurโan (17:85)
ii. Mwanaadamu anaathiriwa sana na matashi ya ubinafsi, uchoyo, upendeleo, chuki, n.k.
iii. Binaadamu wametofautiana mno katika fikra, uoni, vipawa, uzoefu
(mazoea).
iv. Mwanaadamu pia anaathiriwa sana na mabadiliko ya kimazingira na zama
(nyakati).
- Kutokana na mapungufu haya, usimamizi na utekelezaji wa sheria za kitwaghuti hufanywa na watu wachache (watawala) kwa ajili ya manufaa yao tu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao
Soma Zaidi...Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.
Soma Zaidi...(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ููุฑูููุฑูุฉู ุนูุจูุฏู ุงูุฑููุญูู ููู ุจููู ุตูุฎูุฑู ุฑูุถููู ุงูููู ุนููููู ููุงูู: ุณูู ูุนูุช ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ููููููู: "ู ...
Soma Zaidi...Assalaam alykum warahmatullah wabarakatuh.
Soma Zaidi...Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10
Soma Zaidi...