Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho

Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho

Download Post hii hapa

Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho

Swala ya maiti



Mambo yanayostahiki kufanyiwa maiti ya Muislamu
Mambo yaliyo faradhi kufanyiwa maiti ya Muislamu ni manne yafu atayo:
(1)Kuoshwa.
(2)Kuvikwa sanda (kukafiniwa).
(3)Kuswaliwa.
(4)Kuzikwa.



Pamoja na haya manne kuna mambo mengine mengi yanayotakiwa afanyiwe Muislamu anayekaribia kufa na aliyekufa kama alivyotuelekeza Mtume (s.a.w). Hivyo, katika kitabu hiki tumeeleza mambo yote ya msingi yanayostahiki afanyiwe Muislamu pale anapokaribia kufa mpaka baada ya kuzikwa.
Mambo muhimu anayofanyiwa Muislamu anayekaribia Kufa.



Mauti ni jambo la lazima sana kumtokea mwanaadamu na viumbe vyote na huingia bila taarifa wakati wowote na mahali popote kama anavyotufahamisha Allah (s.w):


Popote mlipo mauti yatakufikieni, na hata mkiwa katika ngome madhubuti...” (4:78).



Kila nafsi ita onja ma uti. Na bila s haka m tapew a ujira w enu kam ili s iku ya Kiyama. Na aliyewekwa mbali na moto na akaingizwa Peponi, basi amefuzu (amefaulu kweli kweli). Na maisha ya dunia (hii) si kitu ila ni starehe idanganyayo (watu). (3:185).



Kutokana na ukweli huu ni jambo la busara mno kwa mwanaadamu mwenye akili timamu kujiandaa kukabili mauti wakati wowote na popote atakapokuwa. Ni kweli kuwa maisha ya ulimwengu yamejaa hadaa lakini hatuna budi kukumbuka kuwa maisha yote ni mtihani kwetu na Muumba wetu anatuchunga barabara na kudhibiti tuyatendayo katika kila pumzi ya maisha yetu. Kumbukumbu ya ukweli huu pamoja na kukikumbuka kifo katika kila sekunde ya maisha ndiyo nguvu pekee ya kumsukuma mja kwenye maisha ya wema anayoridhia Allah (s.w). Kifo ni tukio la lazima lisiloepukika kwa kila kiumbe. Hatuna budi kukifanya kifo kitu cha kawaida na kujiandaa kwacho badala ya kufanya zoezi la kukikimbia jambo ambalo ni muhali.



Mtu anapokaribia kufa na baada ya kufa huwa, pamoja na ujanja wake wote na vipaji vyake vyote alivyokuwa navyo, hajimudu kwa chochote na kwa hiyo anahitajia msaada wa kila jambo.



Hivyo Uislamu unatufundisha kuwa mtu anayekaribia kufa tumfanyie yafuatayo:
1. Kumuogesha, kumpigisha mswaki na kumpaka manukato iwapo kuna uwezekano.
2. Kumlaza kwa ubavu wa kulia na kumuelekeza Qibla kama kuna uwezekano. Kama hivi haiwezekani mgonjwa alazwe chali na uso wake unyanyuliwe kiasi cha kuelekea Qibla
3. Kumpa maji ya kunywa.


4. Kutamka kalima ya Laailaahaillallah bila ya kumuashiria kuwa naye atamke. Lengo la kumtamkia kalima hii ya Tawhiid ni kumkumbusha ili naye aweze kutamka kama ni mtu aliyeishi maisha yote kulingana na kalima hiyo. Kumtamkia kalima Muislamu anayekaribia kufa ni agizo la Mtume (s.a.w):



Abu Said na Abu Hurairah (r.a)wamesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Wasomeeni watu wenu wanaokaribia kufa:
“Hapana mola ila Allah”



Pia Mu’az bin Jabal amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema:
Yule ambaye maneno yake ya mw isho yatakuwa: (Hapana mola ila Allah) ataingia Peponi. (Abu Daud).



Kutokana na Hadithi hii haitakuwa rahisi kwa mtu wa motoni kutamka kalima hii bali ataitamka tu yule aliyeishi maisha yake yote kulingana na kalima hii. Kwa mtu mwema kuitamka kalima hii kunampa maliwazo kuwa amali yake njema imetakabaliwa. Kutamka huku si lazima kuwe kwa wazi. Kutamka kimoyo moyo tu kunatosha, japo ni vizuri kuibanisha kwa ulimi iwapo ipo fursa.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1098

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Taratibu za kutaliki katika uislamu.

Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat

Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...
 Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...