Utoaji wa zaka katika Dhahabu, fedha ama silva na pesa

Utoaji wa zaka katika Dhahabu, fedha ama silva na pesa

Download Post hii hapa

Utoaji wa zaka katika Dhahabu, fedha ama silva na pesa

(iii) Dhahabu (gold), fedha (silver) na fedha taslimu (cash)



Miongoni mwa vitu vinavyopendwa na wanaadam ni dhahabu na fedha. Ni vitu hivi walimwengu katika kipindi kirefu cha historia huvitumia kama kipimo cha thamani ya vitu mbali mbali, na ndio vimetumika kama kipimo cha utajiri. Kwa hiyo vimestahiki zaidi kutolewa Zakat:



β€œ... Na wale wakusanyao dhahabu na fedha wala hawazitoi katika njia ya Mwenyezi Mungu, wape habari ya adhabu iumizayo” (9:34).


Aya hii inatuthibitishia kuwa kutoa katika njia ya Allah kutokana na dhahabu na fedha (silver) ni lazima kwa Muislamu. Pia fedha taslimu (Bank money or cash) ziko katika mkumbo huu.



Nisaab ya dhahabu, fedha na fedha taslimu na viwango vya Zakat Nisaab ya dhahabu na fedha imeelezwa katika Hadith ifuatayo:



Ali (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Hapana Zakat kutoka kwa Farasi au Punda. Kwa hiyo chukua Zakat ya fedha (silver), dirham moja kwa kila dirham arobaini (1/40). Hapana Zakat kwa dirham 190. Zinapofika dirham 200, basi kuna dirham 5 za Zakat” (Tirmidh, Abu Da ud).



Kutokana na Hadith, kiwango cha Zakat ya dhahabu, fedha (silver) ni Dirham moja. Dirham ni fedha zilizotumika katika baadhi ya nchi za kiarabu tangu wakati wa Mtume Muhammad (s.a.w) hadi hivi sasa. Pia katika Hadith hii tunafahamishwa kuwa Nisaab ya fedha (silver) ambayo ni sawa na nisaab ya dhahabu na fedha taslim ni dirham 200. Tukitumia kipimo cha uzito Nisaab ya fedha ni gram 577.5 au tola 52.5. Nisaab ya dhahabu ni gramu 82.5 au tola 7.5. Muda wa kutoa Zakat ya fedha, dhahabu na fedha taslim ni baada ya kupindukia mwaka mmoja. Kwa hiyo dhahabu, fedha na fedha taslim zitakapowekwa akiba kwa kipindi cha mwaka mzima zikiwa zimefikia thamani ya dirham 200 au zaidi zitatolewa Zakat kwa kiwango cha 1/40 au 2.5%.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: Dini File: Download PDF Views 795

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

MAANA YA HADITHI SUNNAH
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
NDANI YA SHIMO LA KABURI
NDANI YA SHIMO LA KABURI

Download kitabu Hiki Bofya hapa NDANI YA PANGO LA MAKABURI Mmoja wapo akatowa kamba na kulifunga jeneza vizuri na kuanza kulishusha chini ya mapango kwa kamba ile.

Soma Zaidi...
DARSA ZA TAWHID
DARSA ZA TAWHID

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
TAFSIRI (TARJIMA) YA QURAN KWA LUGHA YA KISWAHILI
TAFSIRI (TARJIMA) YA QURAN KWA LUGHA YA KISWAHILI

Tafsiri ya Quran kwa iswahili iliyotafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-BArwani

Soma Zaidi...