Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Naomba Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake



Namba ya swali 000

Suratul-Quraysh (106)

Kwa jina la Allah,mwingi wa Rehma, Mwenye Kurehemu.
1.Ili kuwafanya Makurayshi waendelee.


2.Waendelee na Safari zao za wakati wa kusi (kwenda Yemen) na wakati wa kaskazi (kwenda Shamu).


3.Basi nawamuabudu Bwana wa nyumba hii (Al-Kaaba).


4.Ambaye anawalisha (wakati Waarabu wenzao wamo) katika njaa, na anawapa amani (wakati wenzao wamo) katika khofu.



Namba ya swali 000

Mafunzo yake je?



Namba ya swali 000

Mafunzo kwa Muhtasari



Kutokana na sura hii kwa muhtasari tunajifunza yafuatayo:
(1 )Neema zote zilizotuzunguka zinatoka kwa Allah (s.w).



(2)Amani, usalama na ustawi wa kweli hupatikana kwa kumtii Allah (s.w) ipasavyo. Kwa mfano amani na ustawi wa Makka ulipatikana kutokana na dua ya Nabii Ibrahim (a.s) ambaye kwa kumtii Mola wake aliacha familia yake mahali pakavu na papweke pasipo na msaada wowote wa kibinaadamu. Wakati anatekeleza amri ya Allah (s.w) ya kuiacha familia yake pale, Nabii Ibrahim (a.s) aliomba:



"Mola wetu! Hakika mimi nimewaweka baadhi ya kizazi changu (mwanangu Ismail na mama yake, Hajar) katika bonde (hili la Makka) lisilokuwa na mimea yoyote katika nyumba yako takatifu. Mola wetu! Wajaalie (wawe) wasimamishaji swala. Na ujaalie nyoyo za watu zielekee kwao na uwaruzuku matunda ili wapate kushukuru" (14:37)



3)Mahusiano, maingiliano na mawasiliano baina ya mataifa katika nyanja mbalimbali za kijamii ni katika neema za Allah (s.w)



Namba ya swali 000

Shukraa, Allah akuzidishie Elimu



Namba ya swali 000

Aaamin Nawe pia ndugu yangu, Allah akupe Neema nyingi



Namba ya swali 000
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2908

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
ADABU ZA KUSOMA QURAN

Adabu wakati wa kusoma quran 1.

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
mgawanyiko katika quran

MGAWANYIKO KATIKA QURAN Juzuu, Sura, Aya, Manzil, Qara Wataalamu wa elimu za Qurani katika fani za uandishi na usomaji wameigawanya Qurani katika mafungu ili kuwezesha urahisi kwa wasomaji wa qurani.

Soma Zaidi...
Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad

(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...