picha

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an

(v)Kuwaombea dua wazazi.

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an
1. Bani-Israil (17: 23-40)
(i)Kujiepusha na kumshirikisha Allah katika nyanja zote.
(ii)Kuwafanyia wema wazazi na kusema nao kwa heshima.
(iii)Kutowakemea wazazi, au kuonesha ishara ya ukaidi kwao, mfano kusema Ah!
(iv)Kuwaonea huruma wazazi na kuwanyenyekea.


(v)Kuwaombea dua wazazi.
(vi)Kuwasaidia wenye shida.
(vii)Kutotumia mali kwa ubadhirifu.
(viii)Kujitaabisha katika kutafuta maisha ili kuwahudumia wazazi ipasavyo.
(ix)Kujiepusha na ubakhili.
(x)Kutowauwa watoto kwa kuhofia umasikini.
(xi)Kujiepusha na zinaa kwani ni njia mbaya na ni uchafu.
(xii)Kujiepusha na kula mali za yatima.
(xiii)Kuchunga ahadi.
(xiv)Kutimiza vipimo wakati wa kupima na kutumia mizani iliyo sawa au kipimo kilicho sawa.
(xv) Kutofuata mambo usiyo na ilimu nayo,yaani kutofuata mambo kwa kibubusa



2. An-Nuur (24:1-31,58-63)pamoja na (7:26),(33:32,59)
(i)Kujiepusha na zinaa.
(ii)Tusifunge ndoa na wenza waovu.
(iii)Kujiepusha kuwasingizia uovu waumini.
(iv)Ni tabia njema kuwa mwenye kufanya toba mara kwa mara.
(v)Tujiepushe na tuhuma mpaka tupate ushahidi. (vi)Kujitahidi kuwadhania vyema waumini.
(vii)Kujiepusha na kutangaza habari mbaya za watu. (viii)Kujiepusha na maovu na machafu (ni amali za shetani).
(ix)Kujiepusha na jazba na viapo.
(x)Kushikamana na kusamehe.
(xi)Tusiingie majumba ya watu mpaka tupate ruhusa (tupige hodi).
(xii)Tukiambiwa turudi tusingie basi turudi. Hakuna kupiga hodi kwenye majumba ya Ummah.
(xiii)Kujiepusha na kutazama yale yaliyokatazwa na sheria ya Allah (s.w).
(xiv)Kujiepusha na zinaa na kulinda tupu zetu.


(xv)Kujisitiri kisheria na kuchunga mipaka ya mahusiano, sauti na mavazi.
(xvi)Wanawake wakae na kujituliza majumbani kwao, wasitoke ila kwa dharura muhimu.
(xvii)Kujitakasa kutokana na uovu na machafu.



3. Luqmaan (31:12-19)
(i)Kuwa na Hikma
(ii)Kumshukuru Allah (s.w).
(iii)Kutoa nasaha njema kwa watoto.
(iv)Kutomshirikisha Allah (s.w), kwani ni dhambi kubwa.
(v)Kuwafanyia wema (Ihsaan) wazazi wetu.
(vi)Kutowatii wazazi kama wakitupeleka vibaya (wakitupelekea kumshirikisha Allah) lakini kukaa nao kwa wema.
(vii)Kushika njia ya waja wema wanaoelekea kwa Allah. (viii)Kuwa na tahadhari katika kila jambo.
(ix)Kuwa na yakini kuwa Allah (s.w), ndiye Mwenye kuruzuku na Mwenye kumlipa mja kile anachostahiki.
(x)Kusimamisha swala.
(xi)Kuamrisha mema.
(xii)Kukataza mabaya.
(xiii)Kuwa na subira katika yale yatakayotusibu. (xiv)Kutowatizama watu kwa dharau.
(xv)Kutotembea katika ardhi kwa maringo. (xvi)Kujiepusha na majivuno na kujifaharisha. (xvii)Kushika mwendo wa kati na kati.
(xviii)Kutopaza sauti, kujiepusha na tabia ya kupiga kelele.



4. Al-Ahqaaf (46:15-18)
(i) Kuwafanyia wema wazazi/walezi.
(ii)Kumuomba Allah (s.w) atupe kizazi chema. (iii)Kufanya toba mara kwa mara.


(iv)Kuwashukuru wazazi kwa kuwatii na kuwaombea dua na msamaha kwa Allah(s.w).
(v)Kufuatilia kwa makini usia mwema wanaotupa wazazi.
(vi )Kutowaka ri pia wazazi/walezi wetu au kuwafanyia mambo mabaya.



5. Al-Hujurat (49:1-13) pamoja na (24:27-29),(33:53), (4:86)
(i)Kutotanguliza maneno/kauli mbele ya kauli ya Allah (s.w) na Mtume wake yaani tusifuate matashi yetu kinyume na maamrisho/matazo ya Allah(s.w) na mtume wake
(ii)Tusipaze sauti zetu juu ya sauti za viongozi wetu.
(iii)Kutowaita watu madirishani au kusema nao mad irishan i.
(iv)Kufanyia uchunguzi taarifa yoyote kabla ya kuifanyia kazi.
(v)Kupatanisha ndugu na jamaa kwa uadilifu.
(vi)Kuunganisha udugu wa Kiislamu.
(vii)Kujiepusha na dharau na kujiona (kujikweza). (viii)Kutoitana majina mabaya.
(ix)Tusitukanane kwa makabila, rangi, taifa au vyeo n.k.
(x)Kujiepusha na kuwadhania watu dhana mbaya.
(xi)Kujiepusha na kupeleleza habari za watu. (xii)Kujiepusha na kusengenya.
(xiii)Kumcha Allah (s.w) ukweli wa kumcha).
(xiv)Kupiga hodi majumba ya watu kabla ya kuingia na kuwatolea salamu wenyeji.
(xv)Tunapokaribishwa majumbani mwa watu tushughulike
na kile kilichotupeleka na tukimaliza tutawanyike. (xvi)Tukiongea na wanawake ambao si maharim zetu
tuongee nao nyuma ya Pazia.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1335

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Nafasi ya Elimu katika uislamu

Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu?

Soma Zaidi...
Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake

Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Athari za vita vya Uhud

Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.

Soma Zaidi...
Sifa za waumini wa ukweli katika uislamu

Je unamjuwq ni nani muumini, na ni zipi sifa za muumini?

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...