Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an

(v)Kuwaombea dua wazazi.

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an
1. Bani-Israil (17: 23-40)
(i)Kujiepusha na kumshirikisha Allah katika nyanja zote.
(ii)Kuwafanyia wema wazazi na kusema nao kwa heshima.
(iii)Kutowakemea wazazi, au kuonesha ishara ya ukaidi kwao, mfano kusema Ah!
(iv)Kuwaonea huruma wazazi na kuwanyenyekea.


(v)Kuwaombea dua wazazi.
(vi)Kuwasaidia wenye shida.
(vii)Kutotumia mali kwa ubadhirifu.
(viii)Kujitaabisha katika kutafuta maisha ili kuwahudumia wazazi ipasavyo.
(ix)Kujiepusha na ubakhili.
(x)Kutowauwa watoto kwa kuhofia umasikini.
(xi)Kujiepusha na zinaa kwani ni njia mbaya na ni uchafu.
(xii)Kujiepusha na kula mali za yatima.
(xiii)Kuchunga ahadi.
(xiv)Kutimiza vipimo wakati wa kupima na kutumia mizani iliyo sawa au kipimo kilicho sawa.
(xv) Kutofuata mambo usiyo na ilimu nayo,yaani kutofuata mambo kwa kibubusa



2. An-Nuur (24:1-31,58-63)pamoja na (7:26),(33:32,59)
(i)Kujiepusha na zinaa.
(ii)Tusifunge ndoa na wenza waovu.
(iii)Kujiepusha kuwasingizia uovu waumini.
(iv)Ni tabia njema kuwa mwenye kufanya toba mara kwa mara.
(v)Tujiepushe na tuhuma mpaka tupate ushahidi. (vi)Kujitahidi kuwadhania vyema waumini.
(vii)Kujiepusha na kutangaza habari mbaya za watu. (viii)Kujiepusha na maovu na machafu (ni amali za shetani).
(ix)Kujiepusha na jazba na viapo.
(x)Kushikamana na kusamehe.
(xi)Tusiingie majumba ya watu mpaka tupate ruhusa (tupige hodi).
(xii)Tukiambiwa turudi tusingie basi turudi. Hakuna kupiga hodi kwenye majumba ya Ummah.
(xiii)Kujiepusha na kutazama yale yaliyokatazwa na sheria ya Allah (s.w).
(xiv)Kujiepusha na zinaa na kulinda tupu zetu.


(xv)Kujisitiri kisheria na kuchunga mipaka ya mahusiano, sauti na mavazi.
(xvi)Wanawake wakae na kujituliza majumbani kwao, wasitoke ila kwa dharura muhimu.
(xvii)Kujitakasa kutokana na uovu na machafu.



3. Luqmaan (31:12-19)
(i)Kuwa na Hikma
(ii)Kumshukuru Allah (s.w).
(iii)Kutoa nasaha njema kwa watoto.
(iv)Kutomshirikisha Allah (s.w), kwani ni dhambi kubwa.
(v)Kuwafanyia wema (Ihsaan) wazazi wetu.
(vi)Kutowatii wazazi kama wakitupeleka vibaya (wakitupelekea kumshirikisha Allah) lakini kukaa nao kwa wema.
(vii)Kushika njia ya waja wema wanaoelekea kwa Allah. (viii)Kuwa na tahadhari katika kila jambo.
(ix)Kuwa na yakini kuwa Allah (s.w), ndiye Mwenye kuruzuku na Mwenye kumlipa mja kile anachostahiki.
(x)Kusimamisha swala.
(xi)Kuamrisha mema.
(xii)Kukataza mabaya.
(xiii)Kuwa na subira katika yale yatakayotusibu. (xiv)Kutowatizama watu kwa dharau.
(xv)Kutotembea katika ardhi kwa maringo. (xvi)Kujiepusha na majivuno na kujifaharisha. (xvii)Kushika mwendo wa kati na kati.
(xviii)Kutopaza sauti, kujiepusha na tabia ya kupiga kelele.



4. Al-Ahqaaf (46:15-18)
(i) Kuwafanyia wema wazazi/walezi.
(ii)Kumuomba Allah (s.w) atupe kizazi chema. (iii)Kufanya toba mara kwa mara.


(iv)Kuwashukuru wazazi kwa kuwatii na kuwaombea dua na msamaha kwa Allah(s.w).
(v)Kufuatilia kwa makini usia mwema wanaotupa wazazi.
(vi )Kutowaka ri pia wazazi/walezi wetu au kuwafanyia mambo mabaya.



5. Al-Hujurat (49:1-13) pamoja na (24:27-29),(33:53), (4:86)
(i)Kutotanguliza maneno/kauli mbele ya kauli ya Allah (s.w) na Mtume wake yaani tusifuate matashi yetu kinyume na maamrisho/matazo ya Allah(s.w) na mtume wake
(ii)Tusipaze sauti zetu juu ya sauti za viongozi wetu.
(iii)Kutowaita watu madirishani au kusema nao mad irishan i.
(iv)Kufanyia uchunguzi taarifa yoyote kabla ya kuifanyia kazi.
(v)Kupatanisha ndugu na jamaa kwa uadilifu.
(vi)Kuunganisha udugu wa Kiislamu.
(vii)Kujiepusha na dharau na kujiona (kujikweza). (viii)Kutoitana majina mabaya.
(ix)Tusitukanane kwa makabila, rangi, taifa au vyeo n.k.
(x)Kujiepusha na kuwadhania watu dhana mbaya.
(xi)Kujiepusha na kupeleleza habari za watu. (xii)Kujiepusha na kusengenya.
(xiii)Kumcha Allah (s.w) ukweli wa kumcha).
(xiv)Kupiga hodi majumba ya watu kabla ya kuingia na kuwatolea salamu wenyeji.
(xv)Tunapokaribishwa majumbani mwa watu tushughulike
na kile kilichotupeleka na tukimaliza tutawanyike. (xvi)Tukiongea na wanawake ambao si maharim zetu
tuongee nao nyuma ya Pazia.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 123

Post zifazofanana:-

JITIBU KWA TIBA ASILI, TIBA ZITOKANAZO NA VYAKULA
1. Soma Zaidi...

TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO
Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Stafeli
Soma Zaidi...

Kitabu Cha hadithi ya Chongo
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a. Soma Zaidi...

Zakaria(a.s) Akabidhiwa Ulezi wa Maryam
Baada ya kupigwa kura juu ya nani awe mlezi wa Maryam, Nabii Zakaria akachaguliwa kuwa mlezi wa Maryam. Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa jirani
Soma Zaidi...

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

matunda na mboga
Soma Zaidi...

Imam Abu Hanifa: Nuuman Ibn Thabit
Soma Zaidi...

Fahamu vitamini D, kazi zake vyakula vya vitamini D na athari za upungufu wake
Soma Zaidi...

maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba
Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi? Soma Zaidi...