Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur-an ili kuleta Umoja na Ukombozi wa Waarabu:

(vii)Dai kuwa Muhammad (s.

Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur-an ili kuleta Umoja na Ukombozi wa Waarabu:

(vii)Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur-an ili kuleta Umoja na Ukombozi wa Waarabu:



Wako baadhi ya watu wanaodai kuwa Muhammad(s.a.w) aliitunga Qur-an ili awaunganishe na kuwakomboa Waarabu. Dai hili pia halina nguvu kwa sababu zifuatazo:



Kwanza, lau dai hilo lingekuwa la kweli basi hapana shaka kuwa Qur-an ingetia msisitizo mkubwa sana katika mada ya umoja na ukombozi wa Waarabu. Kwa hakika hakuna aya hata moja katika Qur-an nzima inayolingania umoja na ukombozi wa taifa la Kiarabu. Itayumkinikaje basi Muhammad (s.a.w) atunge Kitabu kwa lengo la kujenga utaifa wa Waarabu na kusiweko katika kitabu hicho hata aya moja juu ya suala hilo?



Pili, msingi wa umma (taifa) unaofundishwa na Qur-an umejengwa juu ya itikadi ya haki na Qur-an inapinga hisia zote za utaifa kwa kufuata misingi ya rangi au kabila. Kila anayekubali itikadi ya Uislamu anakubalika katika umma wa Waislamu bila ya kujali rangi au kabila, au damu. Umoja uliodhihiri Arabia baada ya kushamiri kwa Uislamu ulikuwa umejengwa juu ya misingi ya Uislamu na siyo utaifa wa Kiarabu.



Tatu, lau umoja wa Waarabu ungekuwa ndilo jambo lililomsukuma Muhammad (s.a.w) hapana shaka angekubali kuwa mfalme wa Waarabu ili atumie fursa hiyo kujenga umoja wa taifa la Waarabu. Lakini tunaona alikataa ufalme pale wakuu wa Kikuraysh walipotaka kumrubuni ili aache kuutangaza Uislamu.



Nne, zipo aya katika Qur-an zinazolikanusha dai hilo. Aya mojawapo ya Qur-an yasema:


"Na (kumbuka) Malaika waliposema: Ewe Maryamu! Kwa hakika


Allah amekuchagua na kukutakasa na kukutukuza kuliko wanawake wa ulimwengu (wote)." (3:42)
Aya hii inamzungumzia Maryamu, mama yake Nabii Isa (a.s). Maryamu alikuwa ni Myahudi.Na Wayahudi walikuwa wanadharau Waarabu kuwa ni taifa duni. Muhammad (s.a.w) alikuwa ni Mwarabu na Qur-an imeshuka kwa lugha ya Kiarabu na watu wa mwanzo kusomewa hii Qur-an walikuwa Waarabu.



Swali ni hili: Ikiwa Muhammad (s.a.w) alitaka kukuza hisia za utaifa wa Waarabu vipi basi aweke katika Qur-an aya hii inayomsifu mwanamke wa Kiyahudi kuwa amechaguliwa, ametakaswa na kutukuzwa na Allah(s.w) kuliko wanawake wote? Kwa nini asimsifie mama yake au mwanamke mwingine yeyote wa Kiarabu?
Aya nyingine ni hii ifuatayo:


Enyi kizazi cha Israili (Mayahudi)! Kumbukeni neema zangu nilizokuneemesheni, na nikakutukuzeni kuliko viumbe wengine. (2:47)
Mifano hii yaonesha kuwa haiingii akilini kuwa Muhammad (s.a.w) awe ametunga Qur-an kwa lengo la kuleta umoja na utukufu wa taifa la Waarabu halafu ndani ya hiyo hiyo Qur-an akasifia kwa sifa za kipeo cha juu kabisa watu walio maadui wa Waarabu!




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 298


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Quran haikuchukuliwa kutoka kwenye biblia
Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

MAANA YA Quran
Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi. Soma Zaidi...

ADABU ZA KUSOMA QURAN
Adabu wakati wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an
Soma Zaidi...

Hukumu za waqfu na Ibtida
waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al adiyat
Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah. Soma Zaidi...

yaliyomo: HUKUMU YA MIM SAKINA, NUN SAKINA, MADA, WAQFU, QALAQALA, TAFKHIM NA TARQIQ, USOMAJI WA QURAN
DARSA ZA TAJWID YALIYOMOSURA YA 01 . Soma Zaidi...

Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s. Soma Zaidi...

fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume. Soma Zaidi...

Maudhui ya Qur-an na Mvuto wa Ujumbe Wake
Soma Zaidi...