Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab



Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wasemao kweli, na wanawake wasemao kweli, na wanaume wanaosubiri, na wanawake wanaosubiri, na wanaume wanaonyenyekea na wanawake wanaonyenyekea, na wanaume wanaotoa (Zaka na) sadaka, na wanawake wanaotoa (Zaka na) sadaka, na wanaume wanaofunga, na wanawake wanaofunga, na wanaume wanaojihifadhi tupu zao, na wanawake wanaojihifadhi, na wanaume wanaomtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wanawake wanaomtaja Mwenyezi Mungu (kwa wingi) Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na ujira mkubwa. (33:35)


Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu (upotevu) ulio wazi (kabisa). (33:36).



Mafunzo
Kutokana na aya hizi tunapata mafunzo yafuatayo:
Kwanza,
Muumini wa kweli ni yule anayejitahidi kwa kadiri ya uwezo wake kutekeleza yale yote yaliyoorodheshwa katika aya (33:35) na kutekeleza maamrisho mengine yote ya Allah (s.w) na Mtume wake pamoja na kuacha makatazo yote ya Allah (s.w) na Mtume wake. Kwa muhtasari sifa za waumini zilizoorodheshwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo.



(i)Wenye kutoa shahada ya kweli kwa kutekeleza vilivyo maamrisho yote ya Allah(s.w) na kuacha makatazo yake yote.
(ii)Wenye kuziingiza katika matendo nguzo zote za imani.
(iii)Wenye kumtii Allah (s.w) na Mtume wake ipasavyo katika kukiendea kila kipengele cha maisha na kuwatii wenye mamlaka juu yao kwa mujibu ya maelekezo ya Allah (s.w) na Mtume wake.
(iv)Wenye kusema na kusimamia ukweli
(v)Wenye kujipinda katika kufanya subira katika kuendesha maisha yao ya kila siku na katika kusimamisha Uislamu katika jamii.
(vi)Wenye kujiepusha na kibri, majivuno, majigambo, n.k. katika kuhusuhubiana na watu katika mchakato wa maisha ya kila siku.
(vii)Wenye kutoa yale Allah(s.w) aliyowaruzuku kwa ajili ya kuwahurumia wenye kuhitajia na pia kwa ajili ya kuundeleza Uislamu na kuusimamisha katika jamii.
(viii)Wenye kuleta mara kwa mara funga za sunnah baada ya kuikamilisha funga ya Ramadhani na funga za kafara kwa yule aliyelazimika kwazo. Yaani wenye kuwa katika
swaumu angalu siku tatu kwa kila mwezi.
(ix)Wanaojihifadhi na zinaa na kujiepusha na vishawishi vyote vya zinaa.
(x) Wenye kumtaja na kumbumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi.



Pili, katika Uislamu waumini wanaume na waumini wanawake wana haki sawa mbele ya Allah (s.w). anayeheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule aliye mchaji zaidi kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:


"Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja, Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja, Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu).Hakika aheshimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni mjuzi mwenye habari (za mambo yote)." (49:13)




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 80

Post zifazofanana:-

Dalili (Alama) za Qiyama
Soma Zaidi...

KUELEKEA BONDE LA UOKOZI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KUELEKEA BONDE LA UOKOZI Alinibeba akapaa angani sana hata sikuona ardhi. Soma Zaidi...

Ni zipi sifa za imamu wa swala?
Soma Zaidi...

Vitabu
VITABU: Karibu kwenye Maktaba yetu ya vitabu, hapa utaweza kusoma na kudownload vitabu vyetu bure. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani
Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii. Soma Zaidi...

Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal
Soma Zaidi...

MAANA NA FADHILA ZA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Soma Zaidi...

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

Ghasia na chokochoko za Makhawariji na kuuliwa kwa Ally
Soma Zaidi...

haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)
Soma Zaidi...

quran tahadhari
TAHADHARI KWA WASOMAJI WA QURAN Wasomaji wa qurani wawe na tahadhari katika usomaji wao. Soma Zaidi...

NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO: kuosha mikono, kuwa msafi, kuvaa viatu, maji safi, kuivisha nyama vyema
NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO Kwa kuwa tumekwisha kuona namna ambavyo minyoo huenezwa, hivyo basi ni rahisi sasa kutaja namna ya kubambana na minyoo. Soma Zaidi...