Dalili za uti kwa wanaume na wanawake

Dalili za uti kwa wanaume na wanawake

tambuwa chanzo na dalili za UTI na tiba yake, pamoja na njia za kupambana na UTI

Dalili za uti kwa wanaume na wanawake

UGONJWA WA UTI
Ugonjwa wa UTI ni kifupisho cha Urinary Track infections. Haya ni maambukizi yanayoshambulia mfumo wa mkojo. Mashambulizi haya kwa kiasi kikubwa husababishwa na bakteria aina ya E.Coil. Bakteria hawa huishi kwenye utumbo (gastrointestinal track). Pia UTI inaweza kusababishwa na fangasi na virusi kwa kiasi kidogo sana. UTI inasumbuwa sana watu, inakadiriwa kuwa kati ya kila watu watano mmoja ana UTI. Wanawake wapo hatarini zaidi kupata UTI kuiko wanaume



UTI inaambukizwa vipi?
Maambukizi mengi ya UTI yana tokea choon wakati wa kujisafisha. Bakteria hawa wanatoka kwenye utumbo kuja nje kupitia haja kubwa. Sasa ikitokea mtu amejisafisha vibaya anaweza kuwachukuwa bakteria hawa na kuwapa njia kuingia kwenye njia ya mkojo na kusababisha mashambulizi. Pia wakati wa kushiriki tendo la ndoa (ngono). hii inaweza kusababisha UTI kuhama kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine. Pia kushirikiana vifaa vya ngono, kutumia vifaa vya uzazi wa mpango na njia nyinginezo.



Dalili za UTI
1.Kukojoa mara kwa mara
2.Kuhisi kuunguwa ama umoto wakati wa kukojoa
3.Kutoa mikojo kwa uchache
4.Mkojo kuwa mchafu, kama mawingu ama mwekundu uliopauka
5.Harufu kali ya mkojo
6.Maumivu ya kwenye njonga kwa wanawake
7.Maumivu ya mkundu na puru kwa wanaume.



Dalili za UTI zinaweza pia kuwa tofauti na hizo hapo juu. Dalili hizi hutofautiana kwa kulingana na aina ya UTI. Kama unataka kuzijuwa dalili zaidi za UTI endelea kusoma makala hii mpaka mwisho.



Aina za UTI na dalili zake.
Ugonjwa wa UTI umegawanyika katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni kama:-
1.UTI ya kwenye figo (acute pyelonephritis). UTI hii huathiri figo, na kusababisha dalili kama:-
1.Maumivu ya mgongo kwa juu
2.Homa kali
3.Kuhisi baridi na kutetemeka
4.Kichefuchefu
5.Kutapika.



2.UTI ya kwenye kibofu (cystitis). hii ni aina ya UTI ambayo huathiri kibofu cha mkojo. Dalili zake ni:-
1.Maumivu ya nyonga
2.Maumivu ya tumbo kwa chini ya kitovu ama mvurugiko wa tumbo kwa chini
3.Kukojoa mara kwa mara huku ukiwa na maumivu.
4.Kukojoa damu, ama mkojo wenye rangi nyekundu ya kupauka.



3.UTI ya kwenye mrija wa mkojo (urethritis). mrija wa mkojo kitaalamu unaitwa urethra. Huu ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuuleta nje. Dalili za UTI hii ni kuhisi kuunguwa wakati wa kukojoa.



Dalili za UTI kwa upande wa wanawake.
Kwa upande wa wanawake dalili za UTI zinaweza kuwa zaidi ya tulizotaja hapo juu. Kwa wanawake UTI inaweza kuathiri mfumo mzima wa uzazi kwa mwanmke. Kwa mfano mwanamke anaweza kupata dalili za mimba kumbe ni UTI. Kuvimba kwa matiti, kuuma kwa tumbo, kubadilika hedhi, kukojoa mara kwa mara. Kwa ufupi kwa wanawake uti inaweza kusumbuwa sana kwani inadhaniwa ni maradhi mengine.



Dalili za UTI kwa wanaume.
Kwa wanaume dalili za UTI ni kama ambazo tumetangulia kuzitaja hapo juu. Kwa wanaume hawana dalili maalumu kama wanawake. Hata hivyo maumivu ya kwenye puru na mkundu hutokea kwa wanaume na si kwa wanawake.



Watu hawa wapo hatarini kupatwa na UTI.



1.Kuwa mwanamke. Wanawake wapo hatarini kwa sababu ya maumbile yao. Njia yao ya mkojo ipo karibu sana na njia ya hajakubwa. Hata hivyo njia yao ya mkojo ni fupi kukifikia kibofu kuliko wanaume.
2.Kuwa ni mwenye kushiriki ngoni.
3.Kama unatumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango kama spermicidal agent
4.Kama mwanamke hapati tena hedhi, yaani amefikia kikomo cha kupata hedhi
5.Kama una matatizo kwenye mfumo wa mkojo.
6.Kama njia ya mkojo imeziba kwa mfano kama unavijiwe kwenye figo na vikaziba njia ya mkojo.
7.Kama unatumia matibabu ya kuongezea kinga ya mwili nguvu kama vile wenye kisukari
8.Kama unatumia mpira wa kukojolea.



NJIA ZA KUJILINDA NA KUIJIKINGA NA UTI
1.Kunjwa maji mengi sana
2.Nenda ukakojoe punde baada ya kufanya ngono
3.Kwa mwanamke jisafishe kuelekea nyuima na si kutokea nyuma kuelekea mbele
4.Safisha vyema choo baada ya kujisaidia
5.Nenda ukakojpoa punde tu unapohisi unataka kukojoa
6.Vaa nguo za ndani zilizo kavu na zisizo bana.
7.Jisafishe vyema sehemu za siri kabla na baada ya kufanya ngono.





                   



Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 3684

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Bawasili usababishwa na nini?
Bawasili usababishwa na nini?

Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...
Fangasi mdomoni ni dalili ya minyoo aina gani
Fangasi mdomoni ni dalili ya minyoo aina gani

Zipo aina nyingi za fantasy ambazo ni rahisi kuathiri binadamu. Wipe ambao haiathiri mdomo, nyayo, shemu za siri na kwenye ngozi.

Soma Zaidi...
Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?
Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?

Hivi huwa unachunguza choo chako? ivi huwa kinazama kwenye maji ama kinaelea? Kila damu ama malendalenda, je ni cheusi sana na kina harufu kali sana.

Soma Zaidi...
Walio katika hatari ya kupata homa ya inni
Walio katika hatari ya kupata homa ya inni

Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia
Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
ATHARI ZA KUTOKUTIBU MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kutapika damu, kichefuchefu, miwasho
ATHARI ZA KUTOKUTIBU MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kutapika damu, kichefuchefu, miwasho

ATHARI ZA KUTOKUTIBU MINYOO Kukaa na minyoo na kutoitibu kwa muda mrefu kunaweza kusababisha madhara mengi hususani kwenye ini na maeneo mengine ya mfumo wa kumeng’enya chakula.

Soma Zaidi...
  Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo
Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe au puto katika mshipa wa damu kwenye ubongo. Uvimbe kwenye Ubongo unaweza kuvuja au kupasuka, na kusababisha kuvuja damu kwenye ubongo. Mara nyingi, kupasuka kwa Uvimbe wa Ubongo hutokea katika nafasi kati

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa unaohusiana na kuzidi kwa joto  mwilini (anhidrosis) ama heatshock
Fahamu Ugonjwa unaohusiana na kuzidi kwa joto mwilini (anhidrosis) ama heatshock

posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa na Ugonjwa unaohusiana na joto ambao hujulikana Kama Anhidrosis ni kutoweza jasho kawaida. Usipotoa jasho mwili wako hauwezi kujipoza, jambo ambalo linaweza kusababisha joto kupita. wakati mwingine inaweza k

Soma Zaidi...