Nabii Lut(a.
Nabii Lut(a.s), kama Mitume wengine walivyofanya aliwanasihi watu wake wamuamini Allah(s.w) na wamche ipasavyo na waogope adhabu yake ambayo ikimfika mtu hapana awezaye kuizuia au kuiondosha.
(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao, (Nabii) Lut: 'Je, hamuogopi?' 'Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.' 'Basi Mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini.(26:161-163)
'Wala sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa (Mwenyezi Mungu) Mola wa walimwengu wote.' 'Je, mnawaingilia wanaume katika viumbe (vyake Mwenyezi Mungu)!' 'Na mnawacha alichokuumbieni Mola wenu katika wake zenu? Kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka (mliyowekewa).'(26:164-166)
Na (wakumbushe) Lut alipowambia watu wake: 'Je, mnaufanya uchafu, na hali mnaona?' Mnawaingilia wanaume kwa matamanio mabaya badala ya wanawake? Hakika nyinyi ni watu mfanyao ya ujinga kabisa. (27:54-55)
Pamoja na nasaha hizi nzuri zilizoambatana na hoja madhubuti, hawakumuamini Lut(a.s) ila watu wachache tu. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu. (51:36)
Pamoja na Nabii Lut(a.s) kuwanasihi kwa maneno ya hekima na hoja zilizo wazi, watu wake hawakuwa tayari kabisa kuacha maovu yale.
Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)
Walishakuwa walevi wa machafu hayo na walipania kumfukuza Nabii Lut na wale walioamini pamoja naye ambao huchukia ubaladhuli huo.
'Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: Wafukuzeni wafuasi wa Lut katika mji wenu, hao ni watu wanaojitakasa, (basi wasikae na sisi wachafu)' (27:56)
'Wakasema: Kama usipoacha, ee Lut (kutukataza haya), bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaofukuzwa (katika nchi hii).' (26:167)
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Mwandhishi Tarehe 2018-08-01 Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 220
Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 kitabu cha Simulizi
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Kitau cha Fiqh
Masharti ya swala
Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali. Soma Zaidi...
UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles. Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s. Soma Zaidi...
DARSA ZA TAWHID
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...
Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu
Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Soma Zaidi...
quran na sayansi
2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio. Soma Zaidi...
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma
Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma. Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga? Soma Zaidi...
Ndoa ya mke zaidi ya mmoja katika uislamu na taratibu zake, faida zake na namna ya kuitekeleza
- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke? Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...