Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah


Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu
75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.a.w) aliwaita Waislamu na kuwapa habari njema, akawaambia:



“Allah(s.w) keshakupeni mahala pazuri pa amani pa kukaa na kuendesha Dini yenu bila ya kuteswa na yeyote. Mahali penyewe ni Yathrib. Nimekwisha pata habari kuwa ndugu zenu wako tayari kukupokeeni kwa hali na mali. Basi kila aliyetayari aondoke leo asingoje kesho, kwani ndugu zenu huko wamesimama mikono wazi, wanangoja kukupokeeni.”17?



Mtume(s.a.w) alitoa amri ya kuhama mnamo April, 622 A.D. mwaka wa 13 B.U na Waislamu katika makundi makundi walianza kuhama kwa siri kuelekea Yathrib. Ili maadui wasije ng’amua kuhama kwao, Waislamu walisafiri usiku na mchana walijipumzisha mafichoni. Walihama na mali ile tu iliyokuwa nyepesi kuchukulika. Vitu vyao vingine vyote waliviacha Makka ikiwa ni pamoja na nyumba zao, vikachukuliwa na jamaa zao waliobakia katika ukafiri. Ni ‘Uthman bin Affan peke yake aliyeweza kuchukua mali yake yote. Mali ya ‘Uthman isiyochukulika ilinunuliwa na jamaa zake kwa fedha taslimu.



Baada ya miezi miwili hivi, takriban Waislamu wote walikwisha hamia Yathrib. Waislamu wachache, akiwemo Abubakar na ‘Ali bin Abu Talib, walibakia Makka na Mtume(s.a.w) ili kufanikisha maandalizi ya kuhama kwake pale atakapopewa ruhusa ya kuhama na Mola wake.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 809

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana: