Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu. Kila palipo na fursa nzuri ni muhimu kuibadili misikiti iliyopo na kuifanya vituo vya harakati. Lakini ichukuliwe tahadhari kubwa ili tusije tumbukia kwenye kosa la kuvamia misikiti ya watu kabla ya kufikia kipindi cha kuikomboa – Fat-h-Makka.



Pili, hatunabudi kujenga mshikamano wa Waislamu kwa njia ya kupendana na kuhurumiana na hasa kwenye matatizo na shida. Rejea udugu baina ya Answar na Muhajiriina. Hatunabudi kujenga mazingira na tabia ya kufanya kazi za bega kwa bega (za kitamasha) katika kuendeleza shughuli mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya Uislamu.



Tatu, hatunabudi kukaa vizuri na wasiokuwa Waislamu hasa wale wasiotupiga vita bayana.Tuwaheshimu, tuwatendee haki na tusiwatukanie miungu yao wala kuidhihaki dini yao. Tuwalinganie kwa hekima na tuwape changamoto ya hoja na mawaidha mazuri.




Waite (waite watu) katika njia ya Mola wako kwa hikima na mauidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora (siyo kwa kuwatukana wao au kutukana Dini yao. Kwa njia hii huwezi kumvuta mtu). Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake, naye ndiye anayewajua walioongoka. (16:125)



Nne, hatunabudi kuwajua vema maadui wa Uislamu na Waislamu na kuzijua vyema hila na mbinu zao katika kuuhujumu Uislamu. Kila Muislamu anatakiwa awe msalama kwa kumjua ni nani adui wa Uislamu, yuko wapi na anafanya nini dhidi ya Uislamu.



Tano, kila Muislamu mwanamume hanabudi kuwa mkakamavu na jasiri aliyetayari kuingia vitani ili kuihami Dini ya Allah(s.w).

Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezazo (silaha), na mafarasi yaliyofungwa tayari (mipakani), ili kwazo (nguvu hizi) muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, (mnaowajua) na pia (maadui zenu) wengine wasiokuwa wao, msiowajua nyinyi (lakini) Mwenyezi Mungu anawajua. Na chochote mtakachokitoa katika njia ya Mwenyezi Mungu (kama hii misaada ya vita vya Jihadi) mtarudishiwa kamili wala hamtadhulumiwa. (8:60)



Sita, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii yetu, hatuna budi kuimarisha uchumi wetu.Uchumi ndio raslimali kuu ya kusimamishia Uislamu katika jamii. Kila kitu cha kimaendeleo kinahitaji matumizi ya mali. Hatunabudi kuhuisha na kuimarisha ukusanyaji na ugawaji wa Zakat na Sadaqat kijamii.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1158

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.

Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto.

Soma Zaidi...
Nasaba ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.

Soma Zaidi...