Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)


Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.s) tunajifunza
yafuatayo:

(i) Binaadamu hapa ulimwenguni yuko mtihanini kama Qur-an inavyobainisha:



Ametukuka yule ambaye Mkononi mwake umo ufalme (wote); Naye ni mwenye uweza juu ya kila kitu. Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni (kukufanyieni mtihani); ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Msamaha. (67:1-2)



Kwa hakika tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyochanganyika; (ya mwanamume na mwanamke), ili tumfanyie mtihani (kwa amri zetu na makatazo yetu); kwa hiyo tukamfanya ni Mwenye kusikia (na) Mwenye kuona. (76:2)



Mwanaadamu anachoweza kufanya si kuepa mitihani bali kutekeleza wajibu wake kwa kadiri ya uwezo wake na kufanya subira juu ya mazito mbali mbali yatakayomfika huku akimtegemea Allah(s.w) ipasavyo



(ii) Muumini baada ya kumcha-Allah(s.w) ipasavyo alipokee kwa moyo mkunjufu lolote litakalomfika likiwa la kheri au lenye sura ya shari, kwani Allah yuko pamoja na waja wake.



(iii) Kwa elimu ndogo ya mwanaadamu kuna matukio mengine yanamtokea mwanaadamu kwa sura ya shari, kumbe ni ya kheri kwake na kinyume chake kama Allah(s.w) anavyotutanabahisha katika aya ifuatayo:



Mmelazimishwa kupigana vita (kwa ajili ya dini). Nalo ni jambo zito kwenu. Lakini huenda mkachukia kitu, nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua, (lakini) nyinyi hamjui. (2:216)


(iv) Muumini wa kweli anatakiwa awe anamkumbuka Allah(s.w) nyakati zote katika hali zote, akiwa na dhiki au wasaa. Na mtu anapokuwa katika dhiki ndio anazijua na kuzithamini vizuri neema mbali mbali alizoneemeshwa na Mola wake na ndio anakuwa na nafasi nzuri ya kushukuru. Kwa mfano ni kweli kuwa mtu hawezi kujua thamani ya shibe kama hajafikiwa na dhiki ya njaa.



(v) Waumini wanalazimika kutekeleza ahadi au viapo wanavyotoa katika kufanya mambo ya kheri.



(vi) Hapana kizuizi chochote kiwezacho kuwazuia waumini kumcha-Mola wao na kusimamisha Uislamu katika jamii.



(vii) Matatizo yanayowafika waumini pasina yale ya kujitakia (ya uzembe), ni nyenzo muhimu za kunoa imaniyao juu ya Allah na kuwapa hamasa na msukumo wa kusimamisha Uislamu katika jamii.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1568

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 web hosting    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Kifo cha Nabii Sulaiman

Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine.

Soma Zaidi...
tarekh 10

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...
Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani

Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.

Soma Zaidi...
Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni

β€œNa (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.

Soma Zaidi...
tarekh11

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...