vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu
Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu

Upungufu wa damu, dalili zake na vyakula vya kuongeza damu
VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU
Damu ni tishu iliyo katika kimiminika. Katika miili yetu damu ina kazi ya kusafirisha viinilishe na hewa ya oksijeni na kuondoa hewa chafu ya kabonidaiyoksaidi mwilini. Pia urekebishwaji wa joto na usafirishwaji wa homoni ndani ya mwili hutegemea damu. Kwa ufupi damu in akazi nyingi. Upungufu wowote wa damu mwilini unaweza kuleta athari nyingi mbaya za kiafya mwilini. Makala hii inakwenda kukueleza njia ya kuongeza damu kwa haraka.
Kazi za damu mwilini
1.Kusafirisha viinilishe kutoka katika mfumo wa mmengβenyo wa chakula kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.
2.Kusafirisha hewa ya oksijeni kutokakwenye mapafu kwenda maeneo mengine ya mwli.
3.Kusafirisha hewa ya kabonikaiyoksaidi kutoka kwenye seli na kpeleka kwenye mapafu kwa ajili ya kutolewa nje
4.Kudhibiti joto la mwili kwa kulipooza inapohitajika na kuliongeza inapohitajika
5.Kusafirisha homoni kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.
Vyakula vya kuongeza damu mwilini
1.Nyama nyekundu kama nyama ya ngβombe, mbuzi. Kondoo
2.Maini
3.Nyama ya figo
4.Mboga za rangi ya kijani kama mchicha na apinachi
5.Maharagwe
6.Kunde
7.Mayai
8.Nafaka nyinginezo
9.Njegere
10.Koeosho na karanga
11.Samaki
12.Nyama ya ndege
13.Karoti
14.Matikiti
15.Zabibu
16.Viazi vitamu
17.Matunda yenye uchachu kama machungwa, ndimu na limao.
18.Polipili nyekundu
Dalili za kupungua kwa damu mwilini
1.Uchovu wa hali ya juu
2.Udhaifu wa mwili
3.Ngozi kuwa na rangi ya njano au mauko
4.Kupumua kwa shida
5.Mapigo ya moyo kutokuwa ya kawaida
6.Kizunguzungu na kichwa kuhisi chepesi
7.Maumivu ya kifua
8.Miguu na mikono kuwa ya ubaridi
9.Maumivu ya kichwa
Sababu za upungufu wa damu mwilini
1.Upungufu wa madini ya chuma mwilini
2.Upungufu wa vitamini A na B-12 mwilini
3.Maradhi kama HIV, UKIMWI, saratani, mardhi ya figo haya huweza kuleta upungufu wa damu
4.Mfumo wa kinga mwilini kuuwa na kuharibu seli hai nyekundu (autoimmune)
5.Uharibifu wa seli hai nyekundu kufanyika kwa haraka kuliko utengenezwaji.
6.Kuwa na maradhi ya sickle cell
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Kitabu cha Afya π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Faida za kiafya za kula kabichi
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kabichi
Soma Zaidi...VYAKULA HATARI KWA VIDONDA VYA TUMBO
Hivi ni vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo. mwenye vidonda vya tumbo hatakiwi kula vyakula hivi
Soma Zaidi...AINA KUU ZA VYAKULA: vyakula vya protini, wanga, fat na mafuta, vitamini, madini na maji
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia katika kusafisha ini
Post hii inahusu zaidi baadhi ya vyakula ambavyo vinaweza kutumika ili kuweza kuweka ini kwenye hali yake ya kawaida.
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kula korosho
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula korosho
Soma Zaidi...