image

Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)

Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.

Surat Ash sharh, imeteremka Makkah na ina aya 8. Sura hii ni miongoni mwa sura za mwanzo kushuka. Sura hii ni ya 94 katika mpangilio wa Quran jinsi ilivyoandikwa kwenye mashaf. Sura hii ni sura iliyotangulia yaani surat dhuhaa zinafanana maudhui zao, na zinakadiriwa kushuka katika nyakati sawa. Wakati mwingine sura hizi huchanganywa kwenye kusoma.

 

Sura hii inasimulia kisa cha kupasuliwa kifua mtume. Tukio hili inasemekeana limetokea mara mbili. Moja alipokuwa mtoto na mara nyingine ni pale alipokuwa katika safari ya Israa na Miraj. Sura hii na iliyofuata zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume s.a.w.

 

Sababu za kushuka sura hii:

Katika historia hakuna sababu maalumu za kushuka sura hii kama ambavyo tumeona sura zilizopita. Lakini ipo hivi. Sura hii na iliyotangulia zilishuka katika wakati ambao ndio Mtume s.a.w amepewa Utume. bado ni mgeni wa kazi ya utume. Wakati ambao vikwazo, fitina kutoka kwa makafiri vilikuwa vimeanza kupamba moto. Sura hizi zilishuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w. Na ndio maana sura hizi zinataja baadhi ya neema ambazo Allah amempa Mtume Muhammad, ambazo miongoni mwazo hakuna Mtume mwingine aliyepewa. Kwa mfano kupasuliwa kifu na kuondolewa uzito ambao ambao ungemfanya kazi ya utume iwe ngumu. Pia neema nyingine ni kutukuzwa utajo wake. Yaani huwezi shahadia kwa kusema laa ilaaha Illa Llha, mpaka umalizie Muhammad rasulullah. 

 

Kisha sura ikaendelea kumfariji kuwa hakika kila utakapopata uzito basi kuna wepesi pia ndani yake. Yaani baada ya taabu utakayoipata basi ujuwe kuna neema zinafuata mbele. Aya ikaendelea kuwa utakapopa faragha fanya juhudi ya kutafuta radhi za Allah kwa ibada na adhkar na mambo mengine.

 

Ufupi wa maneno ni kuwa sura hii imeshuka kwa lengo la kumfariji Mtume s.a.w kutokana na yale aliyoyakuta katika kazi ya utume, na ktokana na yatakayokuja kutokea kama matokeo ya kazi ya Utume. Allah ndiye anajuwa zaidi





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1842


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Haikufundisha Mtume Muhammad quran kwa lengo la kurekebisha tabia za waarabu
Soma Zaidi...

Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mpangilio wa quran ni wa kipekee na uliotumia ujuzi mkubwa
Soma Zaidi...

QURAN: TAJWID, FADHIKA ZA KUSOMA QURAN, FADHILA ZA KUSIKILIZA QURAN, FAIDA ZA SURAT FATIHA, YASIN, BAQARA, TABARAK
Soma Zaidi...

Quran haikutoka kwa Mtu zezeta wala mwenye upungufu wa akili
Soma Zaidi...

Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya. Soma Zaidi...

HIKUMU YA BASMALLAH YAANI KUSOMA BISMILLAH
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?
Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi Soma Zaidi...

ADABU ZA KUSOMA QURAN
Adabu wakati wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

Tofauti kat ya sura za Maka na Madina
Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina. Soma Zaidi...