picha

DALILI ZA KUTOKA AU KUHARIBIKA KWA MIMBA

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

DALILI ZA KUTOKA AU KUHARIBIKA KWA MIMBA

DALILI ZA KUTOKA KWA MIMBA

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka. Yaani karibia robo ya mimba zinazopatikana hutoka. Kitendo hiki cha kutoka kitaalamu huitwa misscarriage. Hiki ni kitendo cha kupotea kwa ujauzito kabla ya wiki ya 20. karibia mimba nyingi hutoka ndani ya miezi mitatu ya mwanzo. Mimba iliyotoka inakuwa na dalili kadhaa. Pia wakati mwingine dalili hizi huashiria kuwa ujauzito upo hatarini.

 

Dalili hizi ni kama;

  1. Kutokwa na damu nyingi ukeni. Mjamzito anaweza kuona damu ikitoka ikiwa chache yaani matone kadhaa ama madoa hii ni kawaida. Lakini ikiwa nyingi huashiria hatari kwa ujauzito.
  2. Kupungua uzito kwa ghafla. Bila ya kujuwa sababu yeyote mjamzito anapungua uzito wake kwa ghafla sana.
  3. Kutokwa na uteute wa rangi ya pink iliyo pauka kwenye uke
  4. Kuondoka kwa dalili za ujauzito kwa ghafla
  5. Kutokwa na tishu yaani kama vipande vya nyama vinatoka ukeni
  6. Maumivu makali ya mgongo ama tumbo


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 1865

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 ai web app     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 web hosting     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

YANAYOATHIRI AFYA TABIA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
MAZINGIRZ

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Afya na Lishe

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 1-20

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...