picha

FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI

Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.

 

Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.

 

Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.

 

FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME

  1. Kuvimba kwa kichwa cha uume
  2. Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
  3. Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
  4. Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
  5. Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
  6. Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
  7. Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.

DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE

  1. Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
  2. Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
  3. Uuke kuwaka moto kwa ndani
  4. Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
  5. Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
  6. Kutokwa na majimaji kwenye uke
  7. Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.

 

WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA

  1. Wachafu
  2. Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
  3. Wenye kisukari
  4. Wenye HIV
  5. Wenye saratani
  6. Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
  7. Wajawazito

 

NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA

  1. Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
  2. Kutokuvaa nguo mbichi
  3. Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
  4. Kuwa msafi muda wowote
  5. Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
  6. Kuosha uke mara kwa mara
  7. Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
 


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 7377

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto

Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Soma Zaidi...
Chanjo Muhimu kwa Watoto Wachanga

โ€‹Chanjo ni kinga madhubuti dhidi ya magonjwa hatari ya utotoni. Post hii inatoa mwongozo kwa wazazi kuhusu umuhimu wa chanjo kwa watoto wachanga, ratiba zake, na jinsi zinavyosaidia kujenga kinga imara ya mwili.

Soma Zaidi...
Jipu: Chanzo chake na njia salama ya kulitibu.

โ€‹Jipu (abscess) ni mkusanyiko wa usaha unaotokea chini ya ngozi au ndani ya tishu za mwili kutokana na maambukizi ya bakteria. Mwili hujaribu kujilinda dhidi ya vimelea hivyo kwa kutuma seli nyeupe za damu kwenye eneo husika, na matokeo yake ni kutengeneza mfuko wa usaha unaosababisha maumivu, uvimbe, na joto. Makala haya yanafafanua chanzo cha majipu na mbinu salama za kuyatibu bila kusababisha maambukizi zaidi.

Soma Zaidi...
Mambo Yanayoharibu Mahusiano Kimya Kimya

โ€‹Mahusiano mengi hayavunjiki kwa sababu ya matukio makubwa ya ghafla, bali kwa sababu ya mambo madogo yanayokusanyika kwa muda na kusababisha mmomonyoko wa upendo na uaminifu. Makala hii inachunguza "wauaji wa mahusiano" wasioonekana waziwazi na namna ya kuwazuia kabla hayajafika mwisho.

Soma Zaidi...
Zijue hatua za kufata ili kuepuka maradhi ya tumbo

Posti hii inaelezea kuhusiana na hatua za kufata ili kujikinga au kuepuka maradhi ya tumbo.kuna vitu vikikosekana husababisha maumivu ya tumbo.

Soma Zaidi...
Dalili za UTI kwa wanaume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume

Soma Zaidi...