FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Madrasa kiganjani π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 Kitabu cha Afya π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili za Fangasi Ukeni kwa Mwanamke
βMakala hii inaangazia maambukizi ya fangasi ukeni (vaginal yeast infection), hali inayowapata wanawake wengi katika hatua mbalimbali za maisha. Tutaangalia dalili kuu za utambuzi, sababu zinazochangia maambukizi haya, na ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi ya kuyashughulikia.
Soma Zaidi...Kazi ya Ini: Jinsi ya kulilinda dhidi ya sumu.
Ini ni kiungo kikubwa zaidi cha ndani mwilini na kinafanya kazi kama "kiwanda cha kusafisha sumu" cha mwili wako. Kazi yake ni muhimu sana kwa uhai, kuanzia kuchuja damu hadi kuyeyusha chakula. Hata hivyo, kutokana na mtindo wa maisha wa kisasa, ini linaweza kulemewa na sumu, jambo linalopelekea maradhi kama ini la mafuta (fatty liver) au uvimbe wa ini (hepatitis). Makala haya yanachambua kazi kuu za ini na mbinu madhubuti za kulilinda dhidi ya uharibifu.
Soma Zaidi...Presha ya kushuka/hypotension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka/ hypotension
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa,ni madhara ambayo utokea endapo Maambukizi kwenye mifupa yasipotibiwa kwa mda wake.
Soma Zaidi...Njia za kupunguza makali ya pressure au shinikizo la damu
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kupunguza ugonjwa wa pressure au shinikizo la damu kwa waliokwisha kupata wanaweza kupunguza na kwa wake ambao hawajapata ni nzuri inawasaidia kuepuka hatari ya kupata ppresha.
Soma Zaidi...