FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili za maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo,ni dalili ambazo ujionesha kwa mtu akiwa na shida kwenye utumbo mdogo na tumbo la kawaida.
Soma Zaidi...Elimu kuhusu HIV na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI
Soma Zaidi...Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Soma Zaidi...Dalili za Saratani ya figo.
Saratani ya Figo ni Saratani ambayo huanzia kwenye figo. Figo zako ni viungo viwili vyenye umbo la maharagwe, kila kimoja kikiwa na ukubwa wa ngumi yako. Ziko nyuma ya viungo vyako vya tumbo, na figo moja kila upande wa mgongo wako.
Soma Zaidi...Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu
Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake
Soma Zaidi...Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.
Soma Zaidi...