FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Kitau cha Fiqh π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).
Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre
Soma Zaidi...Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye mrija wa mkojo(urethritis )
Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye mrija wa mkojo, maambukizi haya usababishwa na virusi na bakteria.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI
Soma Zaidi...Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)
Ugonjwa wa mdomo unaounguaΓΒ ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea
Soma Zaidi...