FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Kitau cha Fiqh π3 web hosting π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Njia za kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi njia mbali mbali ambazo uweza kitumiwa na wataalamu ili kuweza kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.
Soma Zaidi...βNjia za Kutatua Migogoro Katika Ndoa
βMigogoro katika ndoa ni jambo lisiloepukika, lakini uwezo wa kuitatua ndiyo siri ya ndoa yenye furaha na kudumu. Posti hii inatoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kukabiliana na kutoelewana, kukuza mawasiliano bora, na kujenga msingi wa kuaminiana kati ya wanandoa.
Soma Zaidi...Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?
Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza
Soma Zaidi...Maumivu Wakati wa Hedhi: Sababu na Suluhisho
Post hii inachunguza hali ya maumivu wakati wa hedhi (dysmenorrhea), ikigusia sababu za kibaolojia zinazosababisha maumivu haya, dalili za kawaida, na mbinu mbalimbali za nyumbani na kitiba za kupunguza usumbufu huo ili kuboresha hali ya maisha ya mwanamke.
Soma Zaidi...Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo
Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.
Soma Zaidi...