FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...Tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nina minyoo
Mie ni kijana wa kiume umri 33, nna tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nna minyoo lakini hata nikinywa dawa sioni afadhali, niliona labda ni pombe nikapumzika kunywa tatizo lipo pale pale japo nisipokunywa haliwi kwa ukubwa ule ila lipo.
Soma Zaidi...Kutetemeka kwa mikono au mwili bila sababu.
Kutetemeka (tremor) ni miondoko isiyo ya hiari ya sehemu yoyote ya mwili, kwa kawaida mikono, kichwa, au sauti, inayotokana na mikazo ya misuli ya mara kwa mara. Ingawa wengi huhisi ni tatizo la wazee pekee, linaweza kutokea kwa mtu yeyote na kwa sababu mbalimbali. Makala haya yanafafanua sababu za kutetemeka, kuanzia hali za kawaida za muda mfupi hadi changamoto za neva zinazohitaji matibabu.
Soma Zaidi...Kupunguzwa kwa nguvu za kiume: Sababu za kisaikolojia na kimwili.
Kupungua kwa nguvu za kiume, kitaalamu ikijulikana kama erectile dysfunction (ED), ni hali inayoweza kuathiri ustawi wa kihisia na mahusiano ya kijamii ya mwanamume. Ingawa mara nyingi huchukuliwa kama aibu, ni hali ya kawaida ya kiafya inayoweza kutibiwa. Makala haya yanachambua kwa kina sababu mbalimbali za kisaikolojia na kimwili zinazosababisha hali hii, umuhimu wa utambuzi sahihi, na njia za kurejesha afya ya uzazi na nguvu za kiume.
Soma Zaidi...Sababu za Kuwashwa Sehemu za Siri
Kuwashwa kwa sehemu za siri (vaginal itching) ni tatizo linalowapata wanawake wengi na linaweza kusababisha usumbufu mkubwa katika maisha ya kila siku. Makala hii inachambua sababu kuu zinazosababisha hali hii, kuanzia maambukizi ya fangasi, mzio, hadi mabadiliko ya homoni, na kutoa mwongozo wa lini unapaswa kuonana na daktari.
Soma Zaidi...