FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO
FANGASI
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.
Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.
Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.
FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME
- Kuvimba kwa kichwa cha uume
- Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
- Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
- Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
- Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
- Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
- Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.
DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE
- Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
- Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
- Uuke kuwaka moto kwa ndani
- Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
- Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
- Kutokwa na majimaji kwenye uke
- Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.
WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA
- Wachafu
- Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
- Wenye kisukari
- Wenye HIV
- Wenye saratani
- Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
- Wajawazito
NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA
- Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
- Kutokuvaa nguo mbichi
- Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
- Kuwa msafi muda wowote
- Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
- Kuosha uke mara kwa mara
- Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 web hosting π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Madrasa kiganjani π5 Dua za Mitume na Manabii π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Kupambana na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari
Soma Zaidi...Dalili za HIV kwa Mwanaume Baada ya Wiki 2
Makala haya yanaangazia dalili za mwanzo za virusi vya HIV kwa wanaume zinazoweza kujitokeza katika kipindi cha wiki mbili baada ya maambukizi (kipindi cha Acute HIV Infection). Inafafanua jinsi dalili hizi zinavyofanana na mafua ya kawaida, umuhimu wa kutambua ishara hizi mapema, na hatua za kuchukua ikiwemo umuhimu wa kupima na kuanza tiba ili kulinda afya yako na ya mwenza wako.
Soma Zaidi...Umuhimu wa kliniki na vipimo kwa wajawazito.
Ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya kimwili, kihisia, na kisaikolojia. Huduma za kliniki kwa wajawazito (Antenatal Care - ANC) ni nguzo muhimu inayohakikisha mama anakuwa na afya njema na mtoto anazaliwa akiwa salama. Makala hii inaangazia kwa nini kila mjamzito anapaswa kuhudhuria kliniki na umuhimu wa vipimo mbalimbali vinavyofanyika katika kipindi hicho.
Soma Zaidi...Arthritis (Maumivu ya viungo): Vyakula vya kusaidia kupunguza maumivu.
βArthritis, au uvimbe wa viungo, ni hali sugu inayoweza kusababisha maumivu makali, ugumu wa kusonga, na kupungua kwa ubora wa maisha. Ingawa dawa za kitaalamu ni muhimu, lishe sahihi ina jukumu kubwa katika kupunguza uvimbe wa ndani (inflammation) na kupunguza maumivu. Makala haya yanachambua kwa kina vyakula bora zaidi vya kusaidia wagonjwa wa arthritis na jinsi ya kuviingiza kwenye mlo wako wa kila siku.
Soma Zaidi...Dalili za minyoo na sababu zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake
Soma Zaidi...