Aina za swala..

Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.

Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:

 

  1. Swala ya Maamkizi ya Msikiti.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.

   

  1. Swala za Qabiliyyah na Ba’adiyyah.

      -    Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba’adiyyah) ya swala za Faradh.

      -    Ziko aina mbili; ‘Mu’akkadah’ (zilizokokotezwa) na ‘Ghairu Mu’akkadah’ (Hazikukokotezwa).

    Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 152.

 

  1. Swala ya Witiri.

-    Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.

      -    Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.

 

  1. Swala ya Tahajjud (Qiyaamul-layl).

-    Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11. 

-    Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur’an.

    Rejea Qur’an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).

 

  1. Swala ya Tarawehe (Qiyaamu Ramadhan).

-    Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur’an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.

-    Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11. 

 

  1. Swala ya Idil-Fitr na Al-Udhuhaa.

-    Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.

-    Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.

 

  1. Swalatudh-Dhuhaa.

-    Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.

-    Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.

 

  1. Swalatul-Istikharah.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.

 

  1. Swala ya Kukidhi Haja.

-    Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.

 

  1. Swalatut – Tawbah.

-    Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.

    Rejea Qur’an (3:135-136).

 

  1. Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi.

-    Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke. 

 

  1. Swala ya Kuomba (Swalatul-Istisqaa).

-    Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.

-    Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2170

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mifumo ya benki na kazi zake

Hapa utajifunza kazi za benki.

Soma Zaidi...
Funga ya ramadhan na nyinginezo

Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za kufunga ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...