picha

Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.

Aina ya kwanza ya kisukari.

1.Ugonjwa huu wa kisukari utokea kwa Aina kuu mbili, Aina ya kwanza ni pale ambapo mwili inashindwa kabisa kuzalisha insulin kwa hiyo mgonjwa maisha yake yote anaishi kwa kuchomwa insulin, kwa hiyo mgonjwa anaishi kwa kutumia insulin maisha yake yote, hii Aina ya kisukari pengine mtu anazaliwa nayo na maisha yake yote anaishi kwa kutumia insulini Ili iweze kuweka kiwango Cha sukari katika usawa. Kwa hiyo mgonjwa anapaswa kujua hali yake kwa ujumla Ili kuweza kushika masharti yabayohitajika.

 

2. Ugonjwa huu wa kisukari Aina ya kwanza usababishwa na kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho seli hizi kwa kitaamu huitwa beta seli na Alfa seli ambazo kazi zake ni kuweka kiwango Cha sukari kwenye hali ya usawa, kwa hiyo hii Aina ya kisukari ni shida kuiweka sawa bila kutumia  insulini, kwa hiyo tunapaswa kuwa waaminifu katika kutumia insulin mara nyingi  hii Aina ya kisukari kama mtu hajazaliwa nayo ugundulika pale mtu akiwa na miaka chini ya thelathini.

 

3. Kuna sababu ambao upelekea kuwepo kwa ugonjwa huu kama vile , Kuna wakati mwingine mwili uzalisha antibodies ambazo uharibu beta seli zinazokuwepo kwenye kongosho  kwahiyo antibodies hizi zinafanya seli ambazo zimo kwenye kongosho kushindwa kufanya kazi yake na baadae sukari kwenye mwili inashindwa kuwa sawa na hatimaye insulin utumika kila siku kwa mgonjwa na kusaidia kuweka sukari katika hali ya usawa. Na kufanya maisha ya mtu kuendelea kuwa kawaida.

 

4.pengine hali hii ya kuwepo kwa Aina hii ya kwanza ni kwa sababu za kuurithi kutoka kwenye familia kwa sababu Kuna familia ambapo Kuna Aina hii ya sukari Aina ya kwanza kwa sababu ya gene pengine Kuna shida katika kufanya kazi  katika kongosho ambalo usababisha seli zinashindwa kufanya kazi yake kwa sababu ya kuridhi kutoka katika familia. Kwa hiyo tunapaswa kuwa macho na kuchunguza matatizo haya kama yako kwenye ukoo na kuyafanyia kazi.

 

5. Sababu nyingine ya chanzi Cha kuwepo kwa Aina ya kwanza ya sukari ni Ile hali ya kumpatia mtoto mapema kuanza kutumia maziwa ya ngombe na kutumia madini ya nitrate usababisha kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho kwa hiyo watoto wanapaswa kula kwa mda mwafaka na kuzuia kutumia maji yenye nitrate na mtoto kama hakufanikiwa kupata maziwa ya Mama kwa sababu mbalimbali anapaswa kuonana na wataalam wa afya Ili kumwonyesha maziwa anavyopaswa kutumia siyo kutumia maziwa ya ngombe kwa mda mrefu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1673

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 ai web app     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Matatizo ya kisaikolojia baada ya kujifungua (Postpartum Depression).

Kipindi cha baada ya kujifungua ni wakati wa mabadiliko makubwa ya kimwili na kihisia. Makala haya yanalenga kuelimisha kuhusu Postpartum Depression (PPD)β€”hali ya huzuni kali na msongo inayowapata akina mama wengi. Tutachambua dalili, sababu, na njia muhimu za kutafuta msaada ili kuhakikisha afya ya akili ya mama na ustawi wa mtoto.

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI kwa Mtu Aliyeambukizwa Karibuni

Makala hii inaelezea hatua ya awali ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), inayojulikana kama hatua ya maambukizi makali (acute HIV infection). Inafafanua dalili za kawaida zinazoweza kujitokeza wiki chache baada ya mtu kupata maambukizi, umuhimu wa kupima mapema, na kuondoa dhana potofu kuhusu dalili hizi.

Soma Zaidi...
Dawa za kupunguza uzito: Je, zina faida au madhara?

Dawa za Kupunguza Uzito: Je, Zina Faida au Madhara? Mwongozo wa Kitaalamu

Soma Zaidi...
Viungo vinavyoathiriwa na malaria

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya viungo vinavyoathiriwa na ugonjwa wa malaria

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.

Soma Zaidi...
Dalili za Homa ya uti wa mgongo (meningitis)

Posti hii inahusu zaidi dalili za Homa ya uti wa mgongo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye maambukizi kwenye uti wa mgongo.

Soma Zaidi...