picha

Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.

Aina ya kwanza ya kisukari.

1.Ugonjwa huu wa kisukari utokea kwa Aina kuu mbili, Aina ya kwanza ni pale ambapo mwili inashindwa kabisa kuzalisha insulin kwa hiyo mgonjwa maisha yake yote anaishi kwa kuchomwa insulin, kwa hiyo mgonjwa anaishi kwa kutumia insulin maisha yake yote, hii Aina ya kisukari pengine mtu anazaliwa nayo na maisha yake yote anaishi kwa kutumia insulini Ili iweze kuweka kiwango Cha sukari katika usawa. Kwa hiyo mgonjwa anapaswa kujua hali yake kwa ujumla Ili kuweza kushika masharti yabayohitajika.

 

2. Ugonjwa huu wa kisukari Aina ya kwanza usababishwa na kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho seli hizi kwa kitaamu huitwa beta seli na Alfa seli ambazo kazi zake ni kuweka kiwango Cha sukari kwenye hali ya usawa, kwa hiyo hii Aina ya kisukari ni shida kuiweka sawa bila kutumia  insulini, kwa hiyo tunapaswa kuwa waaminifu katika kutumia insulin mara nyingi  hii Aina ya kisukari kama mtu hajazaliwa nayo ugundulika pale mtu akiwa na miaka chini ya thelathini.

 

3. Kuna sababu ambao upelekea kuwepo kwa ugonjwa huu kama vile , Kuna wakati mwingine mwili uzalisha antibodies ambazo uharibu beta seli zinazokuwepo kwenye kongosho  kwahiyo antibodies hizi zinafanya seli ambazo zimo kwenye kongosho kushindwa kufanya kazi yake na baadae sukari kwenye mwili inashindwa kuwa sawa na hatimaye insulin utumika kila siku kwa mgonjwa na kusaidia kuweka sukari katika hali ya usawa. Na kufanya maisha ya mtu kuendelea kuwa kawaida.

 

4.pengine hali hii ya kuwepo kwa Aina hii ya kwanza ni kwa sababu za kuurithi kutoka kwenye familia kwa sababu Kuna familia ambapo Kuna Aina hii ya sukari Aina ya kwanza kwa sababu ya gene pengine Kuna shida katika kufanya kazi  katika kongosho ambalo usababisha seli zinashindwa kufanya kazi yake kwa sababu ya kuridhi kutoka katika familia. Kwa hiyo tunapaswa kuwa macho na kuchunguza matatizo haya kama yako kwenye ukoo na kuyafanyia kazi.

 

5. Sababu nyingine ya chanzi Cha kuwepo kwa Aina ya kwanza ya sukari ni Ile hali ya kumpatia mtoto mapema kuanza kutumia maziwa ya ngombe na kutumia madini ya nitrate usababisha kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho kwa hiyo watoto wanapaswa kula kwa mda mwafaka na kuzuia kutumia maji yenye nitrate na mtoto kama hakufanikiwa kupata maziwa ya Mama kwa sababu mbalimbali anapaswa kuonana na wataalam wa afya Ili kumwonyesha maziwa anavyopaswa kutumia siyo kutumia maziwa ya ngombe kwa mda mrefu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1631

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Maumivu ya shingo na mabega kutokana na kazi za ofisini.

Msongo wa mawazo (stress) ni hali ya kawaida ya kisaikolojia na kimwili inayotokana na shinikizo la maisha. Ingawa kiasi kidogo cha msongo kinaweza kuchochea ubunifu na utendaji, msongo wa muda mrefu ni hatari kwa afya ya mwili na akili. Makala haya yanachunguza kwa kina dalili za msongo wa mawazo—kuanzia mabadiliko ya kihisia, kimwili, hadi kitabia—pamoja na mikakati ya kitaalamu ya kuyatambua na kuyadhibiti mapema ili kuzuia madhara ya kudumu.

Soma Zaidi...
Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono

Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa.

Soma Zaidi...
Kujiamini na jinsi ya kuondoa hofu ya kushindwa.

Hofu ya kushindwa ni moja ya vikwazo vikubwa vinavyozuia watu wengi kufikia malengo na ndoto zao. Inatufanya tubaki kwenye maeneo tuliyoyazoea (comfort zone) na kuogopa kujaribu fursa mpya. Makala haya yanachambua jinsi hofu hii inavyofanya kazi na kukupa mbinu za kisaikolojia za kukusaidia kujenga ujasiri na kubadili mtazamo wako kuelekea mafanikio makubwa.

Soma Zaidi...
Ni bakteria gani husababisha ugonjwa wa pumu

Post hii inakwenda kujibu swali linalosema je ni bakteria aina gani husababisha igonjwa wa pumu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini

Soma Zaidi...
Madhara ya kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Soma Zaidi...