Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Surat at Tin ni sura ya 95 katika mpangilio wa Quran kama ilivyoandikwa kwenye Mashaf. Sura hii ina aya 8 na imeshuka Makkah. Mtume s.a.w alikuwa akiisoma sura hii wakati anaposwali swala ya safari. 

 

Amesimulia Ala Baraa bin Azib kuwa alikuwa Mtume s.a.w akisoma katika swala za safa katika moja ya rakaa mbili alikuwa akisoma surat at Tin (watin wazaytun)…… 

 

Sababu za kushuka kwake. 

Hakuna nukuu hasa za kuonyesha kama kulikuwa na tukio maalumu lililopelekea kushuka sura hii. Kuna baadhi ya kauli ni kuwa kuna swahaba alimfuata Mtumr s.a.w navkumuuliza kuhusu watu ambao ni wazee, na wana matatizo ya kusahau, ama ya akili, vipi amali zao je wataendelea kulipwa? Hapo ndipo ikashuka sura hii. 

 

Sura hii imrjibu vyema swali hilo. Allah anasema wale waliokuwa na imani na kufanya matendo mema basi wana wao malipo yasiokatika. 

 

Maana ya tin, zaitun na mlima sinai

Wametofautiana wafasiri kuhusu maana ya tin na zaitun. Wapo waliosema kuwa hii ni misikiti, yaani msikiti wa Damaska na wa palestina Bayt al Maqsid. 

 

Ila uhakika wa maneno na kaulicyenye nguvu makusudio hapa ni matunda mawili haya yani tunda Tini na tunda Zaituni. Matunda haya yanafahamika kwa kuwa navladha nzuri na manufaa makubwa kwa afya. Allah anaapia kwa kitu chochote kile akitakacho. 

 

Makusudio ya mlima sinai, huu ni mlima ambao Nabii Musa alikuwa akizungunza na Allah. Na Mji wa amani uliotajwa makusudio ni Makkah ambapo kuna msikito mtukufu zaidi.  

 

Ujumla wa sura hii

Sura hii Allah ameanza kuapa kisha akatupa masingatio kuwa hakika mwanadamu ameumbwa katika umbo zuri. Kisha akatupa mazingatio kuwa mwanadamu huyu aliyekuwa katika umbo zuri endapo atafanyavmatendo mema atabakia katika hadhi yake ya juu. Na endapo atamuasi Allah atushushwa awe na hadhi ya chini kabisa katika wenye hadhi za chini. 

 

Allah akatupa mazingatio menginr kuwa wale wanaomuamini Allah ana kufanya matendo mema wana wao malipo yasiokatika. 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 3404

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Maswali yanayohusu quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya id-gham katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq

Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq.

Soma Zaidi...
Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.w)

(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Fatiha

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake

Soma Zaidi...
Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

Soma Zaidi...
Kulaaniwa Bani Israil

Pamoja na kuteuliwa na Allah(s.

Soma Zaidi...