image

Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Surat at Tin ni sura ya 95 katika mpangilio wa Quran kama ilivyoandikwa kwenye Mashaf. Sura hii ina aya 8 na imeshuka Makkah. Mtume s.a.w alikuwa akiisoma sura hii wakati anaposwali swala ya safari. 

 

Amesimulia Ala Baraa bin Azib kuwa alikuwa Mtume s.a.w akisoma katika swala za safa katika moja ya rakaa mbili alikuwa akisoma surat at Tin (watin wazaytun)…… 

 

Sababu za kushuka kwake. 

Hakuna nukuu hasa za kuonyesha kama kulikuwa na tukio maalumu lililopelekea kushuka sura hii. Kuna baadhi ya kauli ni kuwa kuna swahaba alimfuata Mtumr s.a.w navkumuuliza kuhusu watu ambao ni wazee, na wana matatizo ya kusahau, ama ya akili, vipi amali zao je wataendelea kulipwa? Hapo ndipo ikashuka sura hii. 

 

Sura hii imrjibu vyema swali hilo. Allah anasema wale waliokuwa na imani na kufanya matendo mema basi wana wao malipo yasiokatika. 

 

Maana ya tin, zaitun na mlima sinai

Wametofautiana wafasiri kuhusu maana ya tin na zaitun. Wapo waliosema kuwa hii ni misikiti, yaani msikiti wa Damaska na wa palestina Bayt al Maqsid. 

 

Ila uhakika wa maneno na kaulicyenye nguvu makusudio hapa ni matunda mawili haya yani tunda Tini na tunda Zaituni. Matunda haya yanafahamika kwa kuwa navladha nzuri na manufaa makubwa kwa afya. Allah anaapia kwa kitu chochote kile akitakacho. 

 

Makusudio ya mlima sinai, huu ni mlima ambao Nabii Musa alikuwa akizungunza na Allah. Na Mji wa amani uliotajwa makusudio ni Makkah ambapo kuna msikito mtukufu zaidi.  

 

Ujumla wa sura hii

Sura hii Allah ameanza kuapa kisha akatupa masingatio kuwa hakika mwanadamu ameumbwa katika umbo zuri. Kisha akatupa mazingatio kuwa mwanadamu huyu aliyekuwa katika umbo zuri endapo atafanyavmatendo mema atabakia katika hadhi yake ya juu. Na endapo atamuasi Allah atushushwa awe na hadhi ya chini kabisa katika wenye hadhi za chini. 

 

Allah akatupa mazingatio menginr kuwa wale wanaomuamini Allah ana kufanya matendo mema wana wao malipo yasiokatika. 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2656


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake
Soma Zaidi...

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran
Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Quraysh
Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao. Soma Zaidi...

Aina za Madd far-iy
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al_ikhlas (qul huwallahu) na fadhila zake
3. Soma Zaidi...

Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

hukumu za kujifunza tajwid
Kujifunza tajwid ni katika mambo muhimu wakati wa kusoma Quran Soma Zaidi...

Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake
4. Soma Zaidi...