Binti wa ndotoni

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad

BINTI WA NDOTONI.

Baada ya kufikiri kwa kina na kumuomba mungu nilipitiwa na usingizi. Niliwa usingizini nikaota ndoto ya ajabu sana. Nilipokuja kuamka niliona watu ndo wanaanza kujaa msikitini lakini mfalme bado hajafika. Nikaanza kujiuliza maana na tafasiri ya ndoto ile ya ajabu. Nikiwa katika hali ya mawazo nilikuwa nikikumbuka machache kuhusu tafasiri za ndoto. Nikaanza kuichambua ndoto yangu nilioora. Nikiwa kwenye mawazo hayo nikaona kama kuna mtu amekuja na kuniuliza kuhusu ndoto yangu ili anitafasirie.

 

Nimeota nipo safarini na binti mfalme akiwa kwenye safari ile. Tukiwa tupo kwenye jahazi kwa ghafla tulipatwa na ajali. Mule kwenye jahazi lile hakuna mtu ninayemjua asipokuwa ni binti mfalme tu. Katika ajali ile jino lanhu moja liling’oka na nikatumbukia ndani ya maji. Binti mfalme akaja na kamba na kunirushia nikaikamata kamba ile na kufika kwenye mbao kubwa ambayo binti mfalme alikuwemo. Kwa bahati mbaya bint mfalme aliteleza kwenye mbao ile na kuingia kwenye maji, niliwa sijui uogelea nilijitahidi kumuokoa bila mafanikio na akaniashiria kuwa niondoke niendezangu. Baada ya hapo nikashituka

 

Katika hali kama hiyo yule mtu akanieleza kuwa ndoto ile ni ya ukweli na kunajambo ninaelezwa kwenye ndoto ile. Yule mtu akaanza kunieleza maana ya ndoto ile. “kuhusu kuwa safarini wewe na bint mfalme ni ishara ya kushirikiana. Na kuhusu kupata ajali inamaanisha kuwa katika kushirikiana kwenu mtapatwa na matatizo lakini yeye ndiye atakayekuokoa.

 

Na kwakuwa kwenye ndoto ni wewe ndiye uliyeokolewa inamaana wewe katika matatizo yako utapata njia kupitia kushirikiana nae. Na kuhusu yeye kushindwa kuokolewa na wewe na hatimaye akaishia majini inaonesha atapatwa na matatizo na atafariki bila ya wewe kufanikiwa kumuokoa. Ama jino linamaanisha kituchako cha karibi kama mke na ndugu. Hivyo jino lako lile linaonesha ni bint mfale atakuwa mkeo na kung’oka kwa jino ni ishara ya kufariki kwa mkeo. Hii ndiyo tafariri ya ndoto yako”

 

Baada ya hpo yule mtu akatoweka, nilipokuja kupaa fahamu kutoka kwenye mawazo yale sikumuona yeyote. Nikutaka kutafuta zaidi nikaweka imani kuwa huenda ni malaika ametumwa kunisaidia kufasiri ndoto yangu. Basi nikaamuwa kumuoa bint mfalme kutokana na ndoto ile inaonesha yeye ataanza kufa na mimi nitaokoka. Hivyo nikaamini hii ni mipango ya mungu. Basi baada ya swala nikaende kwa mfalme na kumueleza kuwa nimekubai ombi lake.

 

Nilipokuwa nazungumza na mfalme kumbe yele binti alikuwa akisikiliza mazungumzo yale na aliposikia nimekubali alipata furaha kubwa iliyopelekea akazimia. Tulishangaa kusikia kishindo nyuma ya mlango na kuenda kuangalia alikuwa ni binti mfalme aliyezimia pale chini. Moyowangu uliruka sana nikawa najiuliza ndo qadar zimeanza yaani atakufa kweli hapahapa na kuniacha mimi. Aliitwa muuguzi na kuanza kumpa tiba. Nilirudi nyumbani nikiwa nasikilizia kama atakufa au atapona maana akifa nitazikwa hatakama shererhe ya ndoa haijafanyika.

 

Nikiwa na wasiwasi siku ilofata nilielekea kwa mfalme kwenda kujulia hali ya binti yake. Nilishangaa kuona mfalme akiwa na bashasha punde tu aliponiona “mwanangu, mwenzio amepata fahamu tayari na mama yenu anaandaa maandalizi ili wiki ijayo iwe ni sherehe ya ndoa yenu. Nilifurahi sana kuona kuwa binti yupo hai maana alikuwa amebeba dhamana ya uhai wangu. Nikawa najiambia moyoni kuwa wiki ijayo naingia maisha mapya na nitakuwa mfalme mtarajiwa. Sinbad mimi ndo utakuwa mwisho wa kuiona familia yangu.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-08     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1187

Post zifazofanana:-

Dalili za malaria
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama. Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sababu za mngurumo wa moyo
Mngurumo wa moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako. Sauti hizi zinaweza kusikika na kifaa kinachojulikana kama stethoscope. Mapigo ya moyo ya kawaida Soma Zaidi...

Matatizo yanayoweza kusababisha Saratani.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na matatizo yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa Saratani. Soma Zaidi...

Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Zifahamu sifa za mtoto mchanga.
Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy Soma Zaidi...

Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume Soma Zaidi...

dawa ya kutibu infection kwenye kizazi nisaidie doctor
Je unasumbuliwa na maambukizi na mashambulizi ya virusi na bakteria kwenye sehemu za siri ama via vya uzazi?. Posti hii inakwenda kuupa ushauri. Soma Zaidi...

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji
Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea. Soma Zaidi...

Faida za kula bamia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia Soma Zaidi...

Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia
Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali? Soma Zaidi...

Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...