Chanzo cha kiungulia
Post hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa kiungulia, kiungulia ni kitendo cha kupanda kwa gesi kutoka kwenye tumbo mpaka kwenye mdomo,hali uwasumbua wengi na kusababisha hali isiyo rafiki.
Vyanzo vya kiungulia.
1. Kudhoofika kwa utendaji kazi wa kizuizi cha juu cha tumbo kwa kitaalamu huitwa (lower esophagus sphincter) sehemu hii uhakikishe kuwa kila kitu ambacho kinaenda mwilini hakirudi ila sehemu hii ikiharibika usababisha kurudi kwa vyakula na vitu vingine kutoka kwenye tumbo kwenda kwenye mdomo.
2. Mfumo dhaifu wa mmeng'enyo wa chakula.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na mfumo dhaifu wa mmeng'enyo wa chakula .
Kwa sababu ya kuwepo kwa vyakula mbalimbali ambavyo uleta shida kwenye mmeng'enyo wa chakula kama vyakula vya mafuta, sukari, vyakula vya caffeine, chocolate na vyakula vya aina hiyo Usababisha mmeng'enyo wa chakula kutoenda sawa na hatimaye kusababisha kiungulia.
3. Kuwepo kwa kiwango kikubwa cha tindikali kwenye mmeng'enyo wa chakula,
Kwa kawaida tindikali ni lazima kwenye mmeng'enyo wa chakula ila ikizidi inaleta kiungulia aina hii ya tindikali ambayo ukaa tumboni kwa kitaalamu huitwa hydrocholic asidi, ikiwa nyingi upanda mpaka kwenye mdomo na kusababisha kiungulia.
4. Kuwepo kwa baadhi ya madini kwenye mwili .
Kwa sababu kwenye mwili wa binadamu kuna madini mbalimbali na kila aina ya madini ufanya kazi tofautitofauti na yakikosa usababisha matatizo mengi mwilini . Kwa mfano ukosefu wa madini ya magnesium na potassium, yakikosa usababisha kuongezeka kwa kiungulia.
5. Kuwepo kwa uzito mkubwa na kitambi.
Kwa kawaida uzito mkubwa ni chanzo cha magonjwa mengi kwa sababu kuna watu wanene na hawafanyi mazoezi usababisha na wanaopenda kula sana usababisha chakula kupanda juu na kusababisha kiungulia.
6. Wamama wajawazito na wenye umri mkubwa.
Kuna wakati mwingine wamama wajawazito wanakuwa na kiungulia kwa sababu ya hali zao na wengine wenye umri mkubwa kwa sababu ya kushuka kwa immunity upate kiungulia.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Hali ya wasiwasi (Anxiety): Dalili na jinsi ya kuishinda.
Hali ya wasiwasi (anxiety) ni sehemu ya maisha ya binadamu, lakini inapogeuka kuwa tatizo sugu, huathiri vibaya ustawi wa kimwili na kiakili. Makala hii inachunguza kwa kina maana ya wasiwasi, dalili zake za kimwili na kisaikolojia, sababu zake, na mikakati ya kisayansi ya kuishinda. Lengo ni kutoa mwongozo wa kitaalamu utakaomsaidia msomaji kutambua hali hii na kuchukua hatua za kimatibabu na kitabia ili kurejesha utulivu wa maisha.
Soma Zaidi...Madhara ya maambukizi kwenye tumbo
Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi ya sikio kwa watu wazima
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi ya sikio mara nyingi ni maambukizi ya bakteria au virusi ambayo huathiri sikio la kati, nafasi iliyojaa hewa nyuma ya ngoma ya sikio ambayo ina mifupa midogo ya sikio inayotetemeka. Maambukizi ya si
Soma Zaidi...Jinsi ya kutofautisha maumivu ya kichwa cha kawaida na ya malaria.
Maumivu ya kichwa ni tatizo la kawaida linaloweza kusababishwa na mambo mengi, kuanzia uchovu, njaa, hadi magonjwa kama malaria. Kwa kuwa malaria ni ugonjwa unaoweza kuwa hatari ndani ya muda mfupi, ni muhimu kujua jinsi ya kutofautisha maumivu ya kichwa ya kawaida na yale yanayoashiria maambukizi ya vimelea vya malaria. Makala haya yanakupa mwongozo wa dalili za msingi ili uweze kuchukua hatua sahihi za kiafya.
Soma Zaidi...Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV
Soma Zaidi...Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri
Soma Zaidi...