picha

Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

DALILI ZA MINYOO

Aina za minyoo:

Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-

 

  1. Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
  2. Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
  3. Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
  4. Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
  5. Tapeworm (flatworm)  unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.

 

Je ni wapi naweza kupata minyoo?

Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.

 

  1. Kwenye majimaji
  2. Ndani ya maji
  3. Kwenye udongo
  4. Kwenye nyama
  5. Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
  6. Kwenye mbog za majani

 

Ni kivipi naweza pata minyoo?

  1. kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
  2. Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
  3. Kula chakula chenye mayai ya minyoo
  4. Kula udongo wenye mayai ya minyoo
  5. Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
  6. Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue

 

Ni ziipi dalili za minyoo?

  1. Maumivu ya tumbo
  2. Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
  3. Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
  4. Uchofu wa mara kwa mara
  5. Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
  6. Tumbo kujaa na kuwa gumu

 

Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?

  1. Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
  2. Kula chakula kilichopikwa vyema
  3. Usile matunda bila ya kuosha
  4. Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
  5. Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
  6. Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
  7. Kuwa makini na nyama ya nguruwe.

 

JE minyoo inatibika?

Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4273

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)

Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa ya jicho

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya jicho,ni Magonjwa ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za jicho kwa mfano kwenye retina,kuaribu mishipa ya retina ,macho kuwa makavu na pia mtoto wa jicho, hali hii ya magonjwa ya macho Usababisha madhara mbalimbali kama

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia kiungulia

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kuzuia kiungulia

Soma Zaidi...
Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

Soma Zaidi...
Fahamu Dalili zinazotokana na kuzama kwenye majj kwa watoto.

Kuzama hufafanuliwa kama mchakato unaosababisha upungufu mkubwa wa kupumua kutokana na kuzamishwa kwenye chombo cha kuogelea (kioevu). Kuzama hurejelea tukio ambalo njia ya hewa ya mtoto huzamishwa kwenye kioevu, na kusababisha kuharibika kwa kupumua.

Soma Zaidi...
Dalili za mtu aliyegongwa na nyoka

Post hii inahusu zaidi dalili za mtu aliyegongwa na nyoka, nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na sumu ikiingia mwilini mtu huwa na dalili mbalimbali

Soma Zaidi...