picha

Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

DALILI ZA MINYOO

Aina za minyoo:

Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-

 

  1. Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
  2. Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
  3. Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
  4. Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
  5. Tapeworm (flatworm)  unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.

 

Je ni wapi naweza kupata minyoo?

Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.

 

  1. Kwenye majimaji
  2. Ndani ya maji
  3. Kwenye udongo
  4. Kwenye nyama
  5. Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
  6. Kwenye mbog za majani

 

Ni kivipi naweza pata minyoo?

  1. kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
  2. Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
  3. Kula chakula chenye mayai ya minyoo
  4. Kula udongo wenye mayai ya minyoo
  5. Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
  6. Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue

 

Ni ziipi dalili za minyoo?

  1. Maumivu ya tumbo
  2. Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
  3. Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
  4. Uchofu wa mara kwa mara
  5. Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
  6. Tumbo kujaa na kuwa gumu

 

Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?

  1. Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
  2. Kula chakula kilichopikwa vyema
  3. Usile matunda bila ya kuosha
  4. Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
  5. Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
  6. Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
  7. Kuwa makini na nyama ya nguruwe.

 

JE minyoo inatibika?

Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4949

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu

Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.

Soma Zaidi...
dondoo 100

Basi tambua haya;- 1.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa schizophrenia

Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini

Soma Zaidi...
Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...