Dalili kuu za minyoo
Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen
DALILI ZA MINYOO
Aina za minyoo:
Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-
- Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
- Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
- Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
- Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
- Tapeworm (flatworm) unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.
Je ni wapi naweza kupata minyoo?
Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.
- Kwenye majimaji
- Ndani ya maji
- Kwenye udongo
- Kwenye nyama
- Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
- Kwenye mbog za majani
Ni kivipi naweza pata minyoo?
- kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
- Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
- Kula chakula chenye mayai ya minyoo
- Kula udongo wenye mayai ya minyoo
- Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
- Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue
Ni ziipi dalili za minyoo?
- Maumivu ya tumbo
- Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
- Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
- Uchofu wa mara kwa mara
- Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
- Tumbo kujaa na kuwa gumu
Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?
- Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
- Kula chakula kilichopikwa vyema
- Usile matunda bila ya kuosha
- Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
- Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
- Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
- Kuwa makini na nyama ya nguruwe.
JE minyoo inatibika?
Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI
Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.
Soma Zaidi...ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan
Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa pepopunda kwa watoto
Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na
Soma Zaidi...Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu
Soma Zaidi...Athari za kutotibu fangasi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za kutokutibu fangasi
Soma Zaidi...