Dalili kuu za minyoo
Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen
DALILI ZA MINYOO
Aina za minyoo:
Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-
- Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
- Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
- Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
- Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
- Tapeworm (flatworm) unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.
Je ni wapi naweza kupata minyoo?
Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.
- Kwenye majimaji
- Ndani ya maji
- Kwenye udongo
- Kwenye nyama
- Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
- Kwenye mbog za majani
Ni kivipi naweza pata minyoo?
- kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
- Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
- Kula chakula chenye mayai ya minyoo
- Kula udongo wenye mayai ya minyoo
- Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
- Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue
Ni ziipi dalili za minyoo?
- Maumivu ya tumbo
- Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
- Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
- Uchofu wa mara kwa mara
- Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
- Tumbo kujaa na kuwa gumu
Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?
- Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
- Kula chakula kilichopikwa vyema
- Usile matunda bila ya kuosha
- Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
- Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
- Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
- Kuwa makini na nyama ya nguruwe.
JE minyoo inatibika?
Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 Kitabu cha Afya π3 web hosting π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
DALILI ZA SELIMUDU
Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos
Soma Zaidi...Ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster
Soma Zaidi...Akili kuchoka na kushindwa kufanya maamuzi (Decision fatigue).
βMuhtasari βKatika maisha ya kisasa yenye changamoto nyingi, kila siku tunafanya maelfu ya maamuzi, kuanzia yale madogo kama "nivae nini?" hadi makubwa ya kikazi na kifamilia. Hali hii ya kufanya maamuzi mengi mfululizo husababisha hali inayofahamika kama Decision Fatigue (uchovu wa maamuzi). Makala hii inachambua kisaikolojia jinsi hali hii inavyoathiri tija yako, afya ya akili, na inatoa mbinu za kisayansi za kupunguza athari zake ili uweze kufanya maamuzi bora kila siku.
Soma Zaidi...Visababishi vya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...