Dalili na ishara za shambulio la moyo

Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

DALILI 

Daliliza na ishara za kawaida za Shambulio la Moyo ni pamoja na:

1. Shinikizo, kujaa au maumivu ya kufinya katikati ya kifua ambayo hudumu kwa zaidi ya dakika chache

2. Maumivu yanayoenea zaidi ya kifua chako hadi kwenye bega lako, mkono, mgongo, au hata kwenye meno na taya yako

3. Kuongezeka kwa vipindi vya Maumivu ya Kifua

4. Maumivu ya muda mrefu kwenye tumbo la juu

5 Upungufu wa pumzi

6. Kutokwa na jasho kwa wingi sana

7. Kuzimia na kupoteza fahamu.

8. Kichefuchefu na kutapika.

9.kuhisi mapigo ya moyo yanaenda haraka.

10.maumivu ya kichwa.

11.maumivu ya kifua

 

Namna ya Kuzuia

Hatua za kujikinga na  kuzuia shambulizi la moyo

1.Kuacha kuvuta sigara

2.Kufanya mazoezi ya mara kwa mara

3.Kupunguza unywaji wa pombe

4.Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.

5.Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)

6.Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.

 

Mambo ya hatari

Madhara ya shambulizi la moyo Ni Kama Yafuatayo

1.Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

2.Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo ambayo hatimaye hupelekea kifo

3.Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili

4.Kifo cha ghafla.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 2815

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Virusi vya Homa ya Ini (Hepatitis B): Dalili na chanjo.

Homa ya ini aina ya B (Hepatitis B) ni maambukizi makubwa ya virusi yanayoathiri ini. Virusi hivi vinaweza kusababisha ugonjwa wa papo hapo (wa muda mfupi) au sugu (wa maisha yote). Maambukizi sugu ya Hepatitis B yanaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa ini, ikiwemo makovu (cirrhosis), saratani ya ini, na kushindwa kwa ini kufanya kazi. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na umuhimu wa chanjo kama njia kuu ya kujikinga.

Soma Zaidi...
Dalili za HIV kwa Mwanaume Baada ya Wiki 2

Makala haya yanaangazia dalili za mwanzo za virusi vya HIV kwa wanaume zinazoweza kujitokeza katika kipindi cha wiki mbili baada ya maambukizi (kipindi cha Acute HIV Infection). Inafafanua jinsi dalili hizi zinavyofanana na mafua ya kawaida, umuhimu wa kutambua ishara hizi mapema, na hatua za kuchukua ikiwemo umuhimu wa kupima na kuanza tiba ili kulinda afya yako na ya mwenza wako.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya tishu ya Matiti.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi ya tishu ya matiti ambayo husababisha maumivu ya matiti, uvimbe, joto na uwekundu. Pia unaweza kuwa na Homa na baridi. Ugonjwa huu huwapata zaidi wanawake wanaonyonyesha ingawa wakati mwingine hali hi

Soma Zaidi...
Maradhi yatokanayo na fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yatokanayo na fangasi

Soma Zaidi...
Tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nina minyoo

Mie ni kijana wa kiume umri 33, nna tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nna minyoo lakini hata nikinywa dawa sioni afadhali, niliona labda ni pombe nikapumzika kunywa tatizo lipo pale pale japo nisipokunywa haliwi kwa ukubwa ule ila lipo.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .

Soma Zaidi...