Dalili za gonorrhea
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea
Dalilii za gonorrhea
Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.
Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.
Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.
Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.
Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi
Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐2 kitabu cha Simulizi ๐3 Kitau cha Fiqh ๐4 Kitabu cha Afya ๐5 ai web app ๐6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Vyakula Bora kwa Mtoto Anayekua
โLishe sahihi ni msingi mkuu wa ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili. Makala haya yataangazia vyakula muhimu vinavyopaswa kuwemo katika mlo wa mtoto, jinsi ya kuandaa mlo kamili, na ukweli wa kisayansi kuhusu virutubisho vinavyohitajika katika kila hatua ya ukuaji.
Soma Zaidi...Upungufu wa furaha na mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara.
โMakala haya yanachunguza kiini cha upungufu wa furaha (anhedonia) na mabadiliko ya hisia ya mara kwa mara (mood swings), yakichambua visababishi vya kibiolojia na kisaikolojia, pamoja na kutoa mwongozo wa kitaalamu wa kukabiliana nayo.
Soma Zaidi...Mambo ya kufanya kama una kiungulia
Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo unapaswa kufanya kama una tatizo la kiungulia.
Soma Zaidi...Dalili za ovulation kwa mwanamke
โOvulation (kipindi cha upevu wa yai) ni hatua muhimu zaidi katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke, hasa kwa wale wanaopanga kupata ujauzito au wanaotaka kuepuka mimba kwa njia za asili. Makala haya yanachambua dalili kuu zinazoonyesha mwili upo kwenye hatua hii, jinsi ya kuzitambua, na kuweka sawa baadhi ya dhana potofu kupitia ukweli wa kisayansi (Fact Check).
Soma Zaidi...Makosa Yanayofanywa na Wapenzi Wengi
Mahusiano ni safari ya kujifunza kila siku. Makala hii inachambua makosa ya kawaida yanayoweza kuathiri ustawi wa mahusiano, ikitoa mwongozo wa jinsi ya kuyatambua na kuyafanyia kazi ili kujenga uhusiano imara na wenye furaha.
Soma Zaidi...