picha

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6122

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 ai web app     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Dalili na Sababu za homa ya manjano kwa watoto

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili na Sababu za Homa ya manjano ya watoto wachanga ni kubadilika rangi kwa manjano katika ngozi na macho ya mtoto mchanga. Homa ya manjano ya mtoto hutokea kwa sababu damu ya mtoto ina ziada ya rangi ya

Soma Zaidi...
Dalili za Mimba Kabla ya Kukosa Hedhi

​Siku za mwanzoni baada ya kutunga mimba, mwili wa mwanamke huanza kuonyesha mabadiliko madogo ya homoni. Post hii inaangazia ishara za awali ambazo zinaweza kujitokeza hata kabla ya siku ya hedhi inayotarajiwa, ikielezea sababu zake na jinsi ya kuzitofautisha na dalili za kawaida za kabla ya hedhi (PMS).

Soma Zaidi...
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya usafi wa sikio

Post hii inahusu zaidi namna ya kufanya usafi wa sikio, sikio ni mojawapo ya ogani ambayo usaidia kusikia,kwa hiyo sikio linapaswa kusafishwa kwa uangalifu kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Mapigo ya moyo kwenda mbio, mwili kuchoka,kichefuchefu, kizungungu, joto kiasi.

Je, mtu mwenye dalili zifuatazo Kama, Mapigo ya moyo kwenda mbio, mwili kuchoka,kichefuchefu, kizungungu, joto kiasi.

Soma Zaidi...
Tatizo la Kikohozi Cha muda mrefu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kikohozi cha muda mrefu ni zaidi ya kero. Kikohozi cha muda mrefu kinaweza kuharibu usingizi wako na kukuacha unahisi uchovu. Matukio makali ya kikohozi cha muda mrefu yanaweza kusababisha kutapika, kizunguz

Soma Zaidi...