Dalili za gonorrhea

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 6413

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Je, Maumivu ya Tumbo ni Dalili ya Mimba?

​Maumivu ya tumbo ni jambo linaloweza kuleta wasiwasi kwa mwanamke yeyote anayehisi anaweza kuwa mjamzito. Makala hii inafafanua sababu za maumivu haya, kutofautisha kati ya maumivu ya kawaida na yale yanayohitaji tahadhari, na kutoa mwongozo wa hatua za kuchukua.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo za mimba

​Wiki za kwanza za ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya ndani na nje ya mwili wa mwanamke. Makala hii inafafanua mabadiliko hayo ili kumsaidia mama kuelewa kinachoendelea na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo kwa usalama.Utangulizi​Wakati mwingine, mabadiliko ya mwili huanza kujitokeza hata kabla hujapima na kupata majibu chanya ya mimba. Hii inatokana na msukosuko wa homoni unaolenga kutengeneza mazingira rafiki kwa ukuaji wa kiumbe kilichotungwa. Kuelewa dalili hizi ni muhimu ili uweze kujijali na kumpa mtoto wako nafasi nzuri zaidi ya ukuaji kuanzia siku ya kwanza.​Maudhui: Mabadiliko ya Mwili katika Wiki za Mwanzo​Katika kipindi hiki, mwili wako unafanya kazi kubwa kurekebisha mfumo wake:​Mabadiliko ya Homoni: Kiwango cha homoni za estrogen na progesterone hupanda kwa kasi ili kusaidia ujauzito, hali inayoweza kubadili hisia zako (mood swings).​Mabadiliko katika Matiti: Matiti yanaweza kuwa makubwa, mazito, na yenye maumivu mepesi kutokana na kuongezeka kwa mtiririko wa damu na kujiandaa kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.​Mabadiliko ya Mfumo wa Chakula: Unaweza kuhisi kichefuchefu, hasa asubuhi, au kupata mabadiliko ya ladha (kuchukia vyakula fulani ulivyokuwa unapenda awali).​Uchovu: Mwili hutumia nishati nyingi katika wiki za mwanzo kuunda mfumo wa kondo la nyuma (placenta), hali inayokufanya uhisi uchovu na usingizi wa mara kwa mara.​Kukojoa Mara kwa Mara: Uterasi inapoanza kukua na shinikizo la damu kuongezeka, kibofu cha mkojo hupata shinikizo zaidi, jambo linalokufanya utake kwenda chooni mara kwa mara.​Fact Check: Je, mabadiliko haya ni hatari?​Ukweli: Mabadiliko mengi unayoyahisi ni ya kawaida kabisa na ni ishara kuwa mwili wako unakubali ujauzito. Hata hivyo, si kila mwanamke anapata dalili hizi zote.​Tahadhari: Ikiwa utapata dalili hizi, unapaswa kuonana na daktari mara moja:​Maumivu makali ya tumbo (upande mmoja au sehemu ya chini).​Kutokwa na damu nyingi ukeni (vaginal bleeding).​Homa kali au maumivu wakati wa kukojoa.​Kutapika sana kiasi cha kushindwa kuhifadhi maji mwilini.​Hitimisho​Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo ni ishara ya maajabu ya kimaumbile yanayotokea ndani yako. Ingawa baadhi ya hali hizi zinaweza kuwa kero, kumbuka kuwa ni za muda mfupi. Kula mlo kamili, kunywa maji ya kutosha, na kupumzika ipasavyo kutakusaidia kupitia kipindi hiki kwa urahisi zaidi. Usisahau kuhudhuria kliniki mapema ili kupata ushauri wa kitaalamu na ufuatiliaji wa ukuaji wa mtoto wako

Soma Zaidi...
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya njia ya mkojo kwa wanawake

​Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) ni moja kati ya changamoto kubwa za kiafya zinazowasumbua wanawake wengi kote ulimwenguni. Makala haya yanajadili kwa kina vyanzo vya maambukizi haya, dalili zake, sababu zinazowafanya wanawake kuwa katika hatari zaidi, mbinu za kujikinga, na ufafanuzi wa ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu zilizopo kwenye jamii.

Soma Zaidi...
VIDONDA VYA TUMBO SUGU

VIDONDA VYA TUMBO SUGU Matibabu ya vidonda vya tumbo mara nyingi hufanikiwa, na kusababisha uponyaji wa vidonda.

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa ini

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa inni, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye ugonjwa wa inni, Dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...