Dalili za gonorrhea
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea
Dalilii za gonorrhea
Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.
Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.
Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.
Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.
Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi
Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 ai web app π3 Kitau cha Fiqh π4 Madrasa kiganjani π5 web hosting π6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...dalili za mwanzo za ukimwi kwa mwanamke
Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke
Soma Zaidi...Mazoezi ya viungo kama tiba ya unyogovu na wasiwasi.
βGundua uhusiano wa kisayansi kati ya mazoezi ya viungo na afya ya akili. Makala hii inachambua jinsi shughuli za kimwili zinavyoweza kutumika kama nyenzo madhubuti ya tiba ya unyogovu na wasiwasi, ikitoa mwongozo wa kitaalamu wa kuanza safari ya ustawi wa kimwili na kiakili
Soma Zaidi...Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?
Hivi huwa unachunguza choo chako? ivi huwa kinazama kwenye maji ama kinaelea? Kila damu ama malendalenda, je ni cheusi sana na kina harufu kali sana.
Soma Zaidi...Maradhi yatokanayo na fangasi
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yatokanayo na fangasi
Soma Zaidi...Athari za unywaji pombe na sigara wakati wa ujauzito.
Ujauzito ni kipindi muhimu ambacho afya ya mama huathiri moja kwa moja ukuaji na ustawi wa mtoto aliye tumboni. Makala hii inachunguza kwa kina madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya pombe na sigara wakati wa ujauzito. Tunajadili jinsi vitu hivi vinavyovuka kizuizi cha plasenta (placenta) na kuathiri mfumo wa neva, viungo, na ukuaji wa mtoto, huku tukitoa ushauri wa kitaalamu wa jinsi ya kuacha tabia hizi kwa ajili ya usalama wa mtoto na mama.
Soma Zaidi...