picha

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5581

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 ai web app     ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.

Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya seli nyeupe.

Posti hii inazungumzia kuhusiana naร‚ย Sarataniร‚ย ambayo hutokea katika aina ya seli nyeupe ya damu inayoitwa seli ya plasma. Seli za plasma hukusaidia kupambana na maambukizo kwa kutengeneza kingamwili zinazotambua na kushambulia vijidudu. Pia husababish

Soma Zaidi...
Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?

Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua.

Soma Zaidi...
Namna Maambukizi kwenye milija na ovari yanavyotokea

Post hii inahusu zaidi namna Maambukizi kwenye milija na ovari ambayo yanatokea,Mara nyingi usababisha na bakteria wanaoweza kuingia kupitia sehemu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Dalili za uti kwa wanaume na wanawake

tambuwa chanzo na dalili za UTI na tiba yake, pamoja na njia za kupambana na UTI

Soma Zaidi...