picha

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-11-06 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 5480

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za saratani ya ini.

posti inaonyesha dalili mbalimbali za Saratani ya ini. Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako. Ini lako ni kiungo cha ukubwa wa mpira wa miguu ambacho kinakaa sehemu ya juu ya kulia ya tumbo lako, chini ya diaphr

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Fahamu sababu za ugonjwa unanipeleka Kuvimba kwa mishipa ya Damu

posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa ya damu katika mwili wako wote. Kuvimba kwa Mishipa ya Damu hujulikana Kama Behcet amboyo husababisha dalili nyingi ambazo hapo awali zinaweza kuonekana kuwa hazihusiani. Dalili na ish

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma

Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae.

Soma Zaidi...
Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?

Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kipindupindu

Post hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa kipindupindu.Ni dalili zinzojitokeza kwa magonjwa wa kipindupindu.

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa mapigo ya moyo

Mapigo ya moyo ni hisia za kuwa na moyo wa haraka, Kupepesuka au kudunda. Mapigo ya moyo yanaweza kuchochewa na mafadhaiko, mazoezi, dawa au, mara chache, hali ya kiafya. Ingawa mapigo ya moyo yanaweza kuwa ya kutisha, kwa kawaida hayana madhara. Katik

Soma Zaidi...
Ukiwa na aleji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?

Swali langu: Ukiwa na areji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?

Soma Zaidi...
Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

Soma Zaidi...
VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)

Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.

Soma Zaidi...