picha

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5592

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 web hosting     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Madhara ya Tiba kemikali kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba kemikali, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wa saratani, madhara haya yanayoweza kuwa ni kwa Sababu mbalimbali kama vile kuaribika kwa seli zinazoendelea kufanya kazi kwenye mwili.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.

Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dadili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu ambao kitaalamu hujulikana Kama multiple sclerosis.

Soma Zaidi...