Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea
Dalilii za gonorrhea
Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.
Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.
Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.
Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.
Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi
Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU
Soma Zaidi...Kisukari cha Aina ya 2, ambacho wakati mmoja kilijulikana kama Kisukari cha watu wazima au kisichotegemea insulini, ni ugonjwa sugu unaoathiri jinsi mwili wako unavyobadilisha sukari (glucose), chanzo muhimu cha nishati ya mwili wako.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kuhusu kushambuliwa kwa moyo na kupumua, kushambuliwa kwa moyo na kupumua kwa kitaala huitwa (cardiopulmonary Arrest) ni kitendo Cha kusimama ghafla kwa moyo na kupumua.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya magonjwa ya koo yanavyosambaa, magonjwa haya usambaa kutoka sehemu Moja kwenda nyingine kwa njia tofauti kama ifuayavyo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo
Soma Zaidi...Dr huwa nasikia maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos
Soma Zaidi...