picha

Dalili za gonorrhea

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya dalili za gonorrhea

Dalilii za gonorrhea

 

Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.

 

Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?

Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-

1.Maumivu wakati wa kukojoa

2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.

3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.

 

Dalili za gonorrhea kwa wanawake

1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri

2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga

3.Maumivu makali wakati wa kukojoa

4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi

 

Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:

1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.

2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha

3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo

4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6005

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 web hosting     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO

NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupata nafuu kutoka kwa maumivu ya kidonda cha tumbo ikiwa utafata taratibu za kiafya kama:- 1.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya njia ya mkojo kwa wanawake

​Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) ni moja kati ya changamoto kubwa za kiafya zinazowasumbua wanawake wengi kote ulimwenguni. Makala haya yanajadili kwa kina vyanzo vya maambukizi haya, dalili zake, sababu zinazowafanya wanawake kuwa katika hatari zaidi, mbinu za kujikinga, na ufafanuzi wa ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu zilizopo kwenye jamii.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Soma Zaidi...
Makosa Yanayofanywa na Wapenzi Wengi

Mahusiano ni safari ya kujifunza kila siku. Makala hii inachambua makosa ya kawaida yanayoweza kuathiri ustawi wa mahusiano, ikitoa mwongozo wa jinsi ya kuyatambua na kuyafanyia kazi ili kujenga uhusiano imara na wenye furaha.

Soma Zaidi...
Dalili za tetekuwanga

Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu

Soma Zaidi...