picha

Dalili za Homa ya uti wa mgongo (meningitis)

Posti hii inahusu zaidi dalili za Homa ya uti wa mgongo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye maambukizi kwenye uti wa mgongo.

Dalili za ugonjwa wa Homa ya uti wa mgongo.

1.Maumivu ya kichwa.

  Tunajua kuwa uti wa mgongo umeenda mpaka kwenye kichwa na pengine maambukizi ujitokeza kwenye sehemu ambayo ufunika ubongo kwa hiyo maumivu ya kichwa utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye uti wa mgongo na kwenye sehemu ya kichwa inayofunika ubongo, kwa Sababu bakteria na virusi amba usababisha ugonjwa huu ushambulia sana uti wa mgongo na sehemu ya kichwa  hiyo usababisha kichwa kuuma kwa sababu ya maambukizi.

 

2.Mgonjwa mwenye Homa ya uti wa mgongo uhisi kizunguzungu, hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kichwa ambapo bakteria na virusi ushambulia kwenye sehemu za mfumo wa ubongo na kusababisha kizunguzungu kwa mgonjwa.

 

3. Hamu ya kula upungua

Mtu mwenye matatizo ya Homa ya uti wa mgongo usababisha hamu ya kula kupungua kwa sababu ya maambukizi ambayo utokea kwa mgonjwa na kusababisha hamu ya kula kupungua na kusababisha mgonjwa hashindwe  kula chakula

 

4. Degedege hasa kwa watoto

Homa ya uti wa mgongo usababisha degedege hasa kwa watoto utokea sana ukiulinganisha na watu wazima, kwa sababu ya maambukizi kwenye ubongo mawasiliano ya ubongo na misuli upungua mtu mzima au mtoto ushikwa na degedege na kusababisha madhara makubwa kwa mgonjwa na watu waliomzunguka.

 

5. Homa upanda.

Ugonjwa wa Homa ya uti wa mgongo usababisha Homa kupanda kuliko kawaida hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye mwili, Homa kupanda ni kwa sababu system za kwenye mwili zinakuwa sio sawa na hivyo kusababisha Homa kupanda.

 

6. Kukakama kwa shingo.

Hali hii utokea pale ambapo maambukizi yameenea na kusababisha shingo kukakamaa na kuwa fupi kuliko kawaida, hii pengine inawezekana kuwa sababu ya kukaza kwa misuli kwa sababu ya maambukizi yaliyosambaa mpaka kwenye shingo na kusababisha shingo kukukamaa au pengine ni kwa sababu ya degedege ambayo usababisha shingo kukukamaa.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2652

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
Tetekuwanga kwa watu wazima: Ni hatari zaidi?

Tetekuwanga (Varicella) kwa kawaida huchukuliwa kama ugonjwa wa utotoni, na watoto wengi huupata na kupona bila matatizo makubwa. Hata hivyo, unapoupata ukiwa mtu mzima, hali inabadilika. Tetekuwanga kwa watu wazima huchukuliwa kuwa na hatari zaidi, ikiwa na uwezekano mkubwa wa kusababisha dalili kali na maambukizi ya viungo muhimu kama mapafu. Makala haya yanafafanua kwa nini hali hii ni hatari na nini unapaswa kufanya.

Soma Zaidi...
Kutokwa na jasho kupita kiasi wakati wa kulala: Chanzo chake.

kuamka katikati ya usiku ukajikuta nguo zako au mashuka yameloa jasho hadi unalazimika kubadilisha, licha ya kwamba chumba kina ubaridi wa kutosha? Hali hii kitaalamu inajulikana kama Night Sweats. Makala haya yanachambua vyanzo mbalimbali vinavyosababisha tatizo hili, kuanzia sababu za kawaida za kimazingira hadi viashiria vya matatizo ya kiafya yanayohitaji ushauri wa daktari.

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fangasi za miguu na ngozi (Ringworm): Jinsi ya kuwatibu.

Fangasi za ngozi, zinazojulikana kitabibu kama Dermatophytosis au Tinea, ni maambukizi ya kawaida sana ya ngozi yanayosababishwa na fangasi aina ya dermatophytes. Ingawa jina "Ringworm" linaweza kuleta picha ya mdudu, hakuna mdudu anayehusikaβ€”ni fangasi tu! Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua, kutibu, na kuzuia maambukizi haya ili kudumisha afya ya ngozi yako.

Soma Zaidi...