dalili za mimba changa ndani ya wiki moja

dalili za mimba changa ndani ya wiki moja

Je na wewe ni katika ambao wanahitaji kujuwa dalili za mimba ndani ya wiki moja? kama ndio makala hii ni kwa ajili yako. Utakwenda kuona dalili za mwanzo sana za ujauzito toka siku za mwanzoni.

Mimba huweza kutungwa baada ya mbegu ya kiume kukutana na yai na kulirutubisha. Mchakato huu kiasili hufanyika katika tumbo la uzazi katika mirija ya falopia ya mama. Siku hizi teknolojia imekuwa, mimba inaweza kutungishwa nje na baadaye yai kurudishwa kwa mama na tayari kukuwa kama mtoto. Watu wengi wamekuwa wakisumbuka na kutafuta ujauzito. Makala hii itakuwa na maada katika nyanja hii ya afya ya uzazi.

 

Dalili za mimba maana yake ni kuona mabadiliko katika mwili wa mwanamke baada ya kushiriki tendo la ndoa. Mabadiliko haya yawe yamesababishwa na kutungishwa kwa yai. Mabadiliko ya homoni katika mwili wa mwanamke huweza kuzungumza mabo mengi kuhusu afya ya mwanamke huyo. Miongoni mwa dalili za mwanzoni za ujauzito ni mabadiliko ya homoni. Mabadilko haya ndiyo baadaye yanasababisha kichefuchefu, kupata harufu, na mengineyo.

 

JE NI ZIPI DALILI ZA UJAUZITO NDANI YA WIKI MOJA?
Mwanamke anaweza kupatwa na mabadiliko ndani ya wiki moja ya ujauzito. Mabadiliko haya anaweza asiyahisi kwani yamekuwa yakifanana na hali za kawaida. Hii husababisha mwanamke ajegunduwa kuwa ana ujauzito hadi pale atakapokosa siku zake. Hapa nitakuletea baadhi ya mabadiliko ambayo huweza kuonekana mwanzoni sana mwa ujauzito ambayo huweza kuashiria dalili za mimba changa ndani ya wiki moja.


1.Kuona damu kidogo yneye rangi hafifu. Damu hii inaweza kuwa ni kitone ama mabadiliko ya rangi kwenye nguo ya ndani. Huwenda pia asigundue damu hii hadi wakati anapojisafisha. Damu hii kitaalamu hufahamika kama implantation bleeding. Kwa baadhi ya wanawake wanaweza kuiona damu hii mwanzoni kabisa katika wiki ya kwanza.

 

2.Maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanafanana na tumbo la chango. Yanaweza kuuma kwamuda kama unachomwa kisha yanakata. Yanaweza kufanya hivikwa siku kadhaa kisha yanapotea. Kwa wanwake wengine yanaweza kuchukuwa muda mfupi sana hata kwa siku moja ama mbili hivi, ila wengine hata wiki.

 

3.Kichwa kuwa chepesi na kuwa na maumivu ya hapa na pale. Mwanamke anaweza kuhisi kizunguzungu yaani kichwa kinakuwa chepesi sana. Hali hii huweza kuambatana na maumivu ya kichwa ama joto la mwili kuongezeka.

 

4.Kuhisi uchovu. Uchovu ni hali za kawaida ambapo kila mtu anaweza kuihisi hali hii. Kuna sababu nyingi za kuwa na uchovu.lakni kwa mwanamke mwenye mimba hana sababu maalumu. Yaani ghafla anaweza kuhisi uchovu ambao hauna chanzo.

5.Tumbo kujaa gesi na kujaa nakuwa gumu. Hali hii inaweza kuambatana na kupungua kwa hamu ya kula na kukosa choo. Mwanamke atahisi tumbo kuwa limejaa, akila kidogo ameshiba hii ni kwa sababu ya gesi. Gesi hii hutokea kutokana na mabadiliko ya homoni aliyonayo.

 

Kwa ufupi hizo ni baadhi tu ya dalili za mwanzo sana za ujauzito. Mabadiliko haya pia yanaweza kuwa si ujauzito hivyo kuashiria shida nyingine za kiafya kwa mfano. Kuna baadhi ya maradhi yenyewe yanaweza kuwa na baadhi ya dalili za ujauzito kama:-
1.Mabadiliko ya homoni
2.UTI
3.PID
4.Fangasi
5.Shida kwenye kizazi

 

Je ni siku ipi ya kushiriki tendo la ndoa upate ujauzito?
Ujauzito huweza kupatikana katika siku chache sana zisizozidi 10 katika mzunguko wa siku za mwanamke. Siku hizi zipo ambazo nimujarabu sana kutafuta ujauzito na nyingine sio sana. Hivyo kama unataka kutafuta ujauzito zinagtia yafuatayo:
1.Shiriki tendo la ndoa katika siku hatari zote ama ruka kwa mojamoja
2.Shiriki tendo la ndoa siku ambayo una hamu sanna
3.Shiriki tendo la ndoa utakapoona majimaji ya ukeni yameongezeka
4.Shiriki tendo la ndoa utakapoona joto la mwili wako limeongezeka, si kwa sababu unahoama ama ulilala n.k.

Soma zaidi hapa

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 83973

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dalili za madhara ya figo
Dalili za madhara ya figo

Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa upele na matibabu yake
Ugonjwa wa upele na matibabu yake

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa upele na matatibabu yake, ni ugonjwa unaosabavishwa na mdudu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scrabie mdudu huyu usababisha miwasho kwenye ngozi.

Soma Zaidi...
Baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha
Baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, ni madhara ambayo yanaweza kutokea iwapo maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo hayatatibiwa kwa wakati.

Soma Zaidi...
Walio katika hatari ya kupata homa ya inni
Walio katika hatari ya kupata homa ya inni

Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Sasa UKIMWI unatokeaje?
Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

Soma Zaidi...
Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi
Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi

Kubana kwa kifuwa ni katika hali ambazo si naweza kuhatarisha maisha. Huwenda kuwa ni miongoni mwa dalili za magonjwa mengi. Je unadhani na HIv na UKIMWI ni moja ya magonjwa hayo?

Soma Zaidi...
 Dalili za Ugonjwa wa mapigo ya moyo
Dalili za Ugonjwa wa mapigo ya moyo

Mapigo ya moyo ni hisia za kuwa na moyo wa haraka, Kupepesuka au kudunda. Mapigo ya moyo yanaweza kuchochewa na mafadhaiko, mazoezi, dawa au, mara chache, hali ya kiafya. Ingawa mapigo ya moyo yanaweza kuwa ya kutisha, kwa kawaida hayana madhara. Katik

Soma Zaidi...
Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?
Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?

Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua.

Soma Zaidi...
Dalili za ukosefu wa misuli.
Dalili za ukosefu wa misuli.

Posti hii inahusu dalili za ukosefu wa misuli. ukosefu wa udhibiti wa misuli wakati wa harakati za hiari, kama vile kutembea au kuokota vitu. Ishara ya hali ya msingi, Ataxia inaweza kuathiri harakati, hotuba, harakati za jicho na kumeza.

Soma Zaidi...