DALILI ZA MIMBA YA WATOTO MAPACHA


image


Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.


Mapacha hutokea endapo mbegu Mwanamke atatoa mayai mawili na yote yakarutubishwa mapacha wa aina hii ni mapacha ambao hawafanani. Na pia mapacha hutokea endapo yai lililorutubishwa nikajigawa sehemu mbili na kila moja katika sehemu hizo ikakuwa kama mtoto. mapacha wa aina hii hufanana.

 

Dalili za mapacha ni kawaida na zile za mimba za kawaida. hata hivyo kunakuwa na ongezeko la ukali wa dalili hizo. Pia kuna dalili baadhi ambazo hawezi kuzipata mwenye mimba ya mtoto mmoja. Dalili za kawaida za mimba ni kama:

  1. kukosa hedhi
  2. maumivu ya tumbo
  3. kupata kichefuchefu
  4. uchovu
  5. maumivu ya tumbo na kichwa

 

Dalili ambazo ni za kawaida za mimba lakini mwenue mappacha zinaweza kuwa kali zaidi:

  1. Kujaa sana kwa maziwa
  2. maumivu makali ya maziwa
  3. uchovu mkali sana
  4. kuhisi njaa kali na kupata hamu ya kula

 

Tofauti na dalili hizo sasa nitakwenda kukuelekeza daili za mimba mapacha. Hata hivyo dalili hizi zinahitaji kuthibitishwa na kipimo ili kuwa na uhakika kama ni mimba mapacha. Dalili hizo ni kama:-

  1. Mtoto kuanza kucheza mapema sana tofauti na mimba nyingine
  2. Mtoto anapocheza unahizi anacheza kwenye maeneo tofautitofauti ya tumbo na sio sehemu moja.
  3. tumbo huwa kubwa zaidi na hukuwa kwa haraka sana.
  4. kuongezeka kwa uzito haraka haraka
  5. mapigo ya moyo ya mtoto huwa ni zaidi ya mapigo ya mtoto mmoja.

 

Changamoto za mimba mapacha

Mwanamke mwenye mimba ya mapacha anaweza kupatwa na changamoto ambazo zinaweza kuwa kali zaidi ya asiye na mpacha. Changamoto hizo ni kama:-

  1. ongezeko la shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) wakati wa ujauzito
  2. Yupo hatarini kupata kisukari cha mimba
  3. uchache wa majimaji ya amniotic fluid
  4. kujifunguwa watoto njiti
  5. kupasuka kwa placenter

 

Changamoto za mimba mapacha sio tu sitaishia kwa mama bali pia zinaweza kumpata mtoto ama watoto. Matatizo yanayoweza kuwapata watoto ni pamoja na:-

  1. Ubongo kuvuja damu
  2. Kuzaliwa njiti
  3. kuzaliwa na uzito kidogo
  4. kuwa na tatizo la kupata baridi
  5. mtoto kushundwa kula
  6. mtoto kupata matatizo ya kuona

 

Nini kifanyike kumlinda mama na watoto

Kutokana na changamoto ambazo mama mwenye mimba mapacha anaweza kuyapata ama matatizo ambayo yanaweza kuwapata watoto, hapa nitakupa mambo ya kufanya kukabiliana na shida hizo:-

  1. kuhudhuria clinic kila inapofika tarehe ya kwenda bila kukosa
  2. onana na daktari kila unapopata tatizo la kiafya.
  3. kula vizuri
  4. pata muda wa kuoumzika
  5. fanya mazoezi hata ya kutembea
  6. kunywa maji mengi
  7. kuwa na furaha. epuka mambo ya kukuletea misongo ya mawazo.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    6 Jifunze fiqh    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Sabau za maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

image Mke Wang Ana tatizo la tumbo kuuma chini upande wa kushoto akishika ni pagumu ,anapatwa na kichefuchef tumbo kujaa ges na kujiisi kusiba he mtanisaidije ili kuondoa tatizo Hilo Ila anaujauzito wa wiki mbili
Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali. Soma Zaidi...

image Madhara ya mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa. Soma Zaidi...

image Fahamu siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu. Soma Zaidi...

image Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.
Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka. Soma Zaidi...

image Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.
posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtoto kwenye uterasi wakati wa ujauzito au nyenzo za fetasi, kama vile nywele, zinapoingia kwenye damu ya mama. Amniotic Fluid Embolism ina uwezekano mkubwa wa kutokea wakati wa kuzaa au mara tu baadaye. Soma Zaidi...

image Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi. Soma Zaidi...

image Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia
Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali? Soma Zaidi...

image Kutokwa maji yan seminal swhemu za siri kwa mwanamke nidalili ya ugojwa gan?
Kutokwa Majimaji sehemu za siri kwa mwanamke sio jambo la kushangaza na kuhisivunaumwa. Majimajivhaya ndio huboresha afya ya uzazi kwa kusafisha na kulinda via vya uzazi. Lakini majimajivhaya yakiwa mengi, ama yanawasha ama yanaharufu haa ndipo kwenye tatizo. Soma Zaidi...

image Mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika. Soma Zaidi...