Posti hii inahusu zaidi dalili za mtoto Mwenye UTI,ni dalili ambazo uwapata watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano.
Dalili za UTI kwa mtoto chini ya umri wa miaka mitano.
1. Mtoto anakuwa na njano
Mtoto mdogo mwenye chini ya umri wa miaka mitano akiwa na ugonjwa wa UTI akiwa na Maambukizi ya UTI anaweza kuwa na njano kama dalili mojawapo ya ugonjwa wa UTI.
2. Joto la mwili kushuka kuzidi kiasi
Mtoto mdogo akiwa na ugonjwa wa UTI joto lake la mwili kushuka kupitia kiasi, hii utokea hasa kwa watoto wenye Chini ya umri wa miezi miwili kwa hiyo mama akiona dalili hii anapaswa kumwangalia mtoto wake na kupima UTI.
3. Mtoto akiwa na UTI anaweza kuharisha na kutapika, hii utokea kwa sababu maambukizi yanakuwa yameenea sehemu mbalimbali za mwili na usababisha kutoa kila kitu ambacho uingia mdomoni na kumfanya mtoto aanze kutapika na kuharisha, lakini si kila mtoto anayeharisha na kutapika ni kwa sababu ya ugonjwa wa UTI lakini mama na mlezi wanapaswa kupima mtoto ikiwa ataonyesha dalili za kuharisha na kitapika.
4.Maumivu ya chini ya Tumbo.
Hii ni dalili ambazo ujitokeza kwa watoto kuanzia miezi miwili mpaka miaka mitano, kwa Sababu ya maambukizi kuenea sehemu mbalimbali tumbo uanza kuuma hasa chini ya kitovu kwa hiyo mtoto kama hawezi kuongea ukimgusa kwenye tumbo anasikia maumivu lakini wale wenye uwezo wa kuongea wanaweza kuponyesha dalili.
5.Maumivu wakati wa kukojoa
Hii ni dalili mojawapo kwa mtoto Mwenye dalili ya UTI, kwa Sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na bakteria wameshaharibu kibofu mtoto usikia maumivu makali wakati wa kukojoa na pengine uanza kulia Lia kwa sababu ya maumivu.hapa mtoto kama anaweza kuongea atakwambia kama hawezi utaona analia wakati wa kukojoa.
6. Kiasi Cha kikohoa kwa mtoto kuongezeka.
Hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, kwa hiyo kibofu Cha mkojo hushindwa kutunza mkojo kwa mda mrefu na halimaye mkojo uanza kutoka mara kwa mara. Kwa hiyo hii Dalili ukolijitokeza mama inabidi awe makini kwenda kwenye vipimo Ili kuangalia kama Kuna UTI au la.
Angalisho: hapo juu ni Dalili za UTI kwa watoto iwapo mtoto atapatwa na dalili hizo usinunue dawa kumpatia ukadhani mara Moja ni UTI Bali inabidi kuchukua vipimo maana hizo Dalili uweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.
Soma Zaidi...Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini.
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za ugonjwa wa mapafu.ambapo kitaalamu hujulikana Kama Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu yako. Majimaji mengi kw
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Soma Zaidi...