Dalili za mtoto Mwenye UTI
Posti hii inahusu zaidi dalili za mtoto Mwenye UTI,ni dalili ambazo uwapata watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano.
Dalili za UTI kwa mtoto chini ya umri wa miaka mitano.
1. Mtoto anakuwa na njano
Mtoto mdogo mwenye chini ya umri wa miaka mitano akiwa na ugonjwa wa UTI akiwa na Maambukizi ya UTI anaweza kuwa na njano kama dalili mojawapo ya ugonjwa wa UTI.
2. Joto la mwili kushuka kuzidi kiasi
Mtoto mdogo akiwa na ugonjwa wa UTI joto lake la mwili kushuka kupitia kiasi, hii utokea hasa kwa watoto wenye Chini ya umri wa miezi miwili kwa hiyo mama akiona dalili hii anapaswa kumwangalia mtoto wake na kupima UTI.
3. Mtoto akiwa na UTI anaweza kuharisha na kutapika, hii utokea kwa sababu maambukizi yanakuwa yameenea sehemu mbalimbali za mwili na usababisha kutoa kila kitu ambacho uingia mdomoni na kumfanya mtoto aanze kutapika na kuharisha, lakini si kila mtoto anayeharisha na kutapika ni kwa sababu ya ugonjwa wa UTI lakini mama na mlezi wanapaswa kupima mtoto ikiwa ataonyesha dalili za kuharisha na kitapika.
4.Maumivu ya chini ya Tumbo.
Hii ni dalili ambazo ujitokeza kwa watoto kuanzia miezi miwili mpaka miaka mitano, kwa Sababu ya maambukizi kuenea sehemu mbalimbali tumbo uanza kuuma hasa chini ya kitovu kwa hiyo mtoto kama hawezi kuongea ukimgusa kwenye tumbo anasikia maumivu lakini wale wenye uwezo wa kuongea wanaweza kuponyesha dalili.
5.Maumivu wakati wa kukojoa
Hii ni dalili mojawapo kwa mtoto Mwenye dalili ya UTI, kwa Sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na bakteria wameshaharibu kibofu mtoto usikia maumivu makali wakati wa kukojoa na pengine uanza kulia Lia kwa sababu ya maumivu.hapa mtoto kama anaweza kuongea atakwambia kama hawezi utaona analia wakati wa kukojoa.
6. Kiasi Cha kikohoa kwa mtoto kuongezeka.
Hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, kwa hiyo kibofu Cha mkojo hushindwa kutunza mkojo kwa mda mrefu na halimaye mkojo uanza kutoka mara kwa mara. Kwa hiyo hii Dalili ukolijitokeza mama inabidi awe makini kwenda kwenye vipimo Ili kuangalia kama Kuna UTI au la.
Angalisho: hapo juu ni Dalili za UTI kwa watoto iwapo mtoto atapatwa na dalili hizo usinunue dawa kumpatia ukadhani mara Moja ni UTI Bali inabidi kuchukua vipimo maana hizo Dalili uweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Kivimba kwa mishipa ya Damu
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa yako ya damu. Inasababisha mabadiliko katika kuta za mishipa ya damu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha, kudhoofisha, kupungua na kupungua. Mabadiliko haya huzuia mtiririko wa damu, na kusababi
Soma Zaidi...Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...Kupambana na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari
Soma Zaidi...Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI
Soma Zaidi...Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutambua dalili za msongo wa mawazo (Stress).
Msongo wa mawazo (stress) ni hali ya kisaikolojia na kimwili inayotokana na shinikizo la maisha, ambalo linaweza kuathiri afya ya jumla ikiwa halitadhibitiwa. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu wa kutambua dalili za msongo wa mawazo, ikijumuisha mabadiliko ya kihisia, kimwili, na kitabia, pamoja na mikakati ya usimamizi ili kudumisha afya bora ya akili.
Soma Zaidi...