Dalili za mtoto Mwenye UTI

Dalili za mtoto Mwenye UTI

Posti hii inahusu zaidi dalili za mtoto Mwenye UTI,ni dalili ambazo uwapata watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano.

Dalili za UTI kwa mtoto chini ya umri wa miaka mitano.

1. Mtoto anakuwa na njano

Mtoto mdogo mwenye chini ya umri wa miaka mitano akiwa na ugonjwa wa UTI akiwa na Maambukizi ya UTI anaweza kuwa na njano kama dalili mojawapo ya ugonjwa wa UTI.

 

2. Joto la mwili kushuka kuzidi kiasi

Mtoto mdogo akiwa na ugonjwa wa UTI joto lake la mwili kushuka kupitia kiasi, hii utokea hasa kwa watoto wenye Chini ya umri wa miezi miwili kwa hiyo mama akiona dalili hii anapaswa kumwangalia mtoto wake na kupima UTI.

 

3. Mtoto akiwa na UTI anaweza kuharisha na kutapika, hii utokea kwa sababu maambukizi yanakuwa yameenea sehemu mbalimbali za mwili na usababisha kutoa kila kitu ambacho uingia mdomoni na kumfanya mtoto aanze kutapika na kuharisha, lakini si kila mtoto anayeharisha na kutapika ni kwa sababu ya ugonjwa wa UTI lakini mama na mlezi wanapaswa kupima mtoto ikiwa ataonyesha dalili za kuharisha na kitapika.

 

4.Maumivu ya chini ya Tumbo.

Hii ni dalili ambazo ujitokeza kwa watoto kuanzia miezi miwili mpaka miaka mitano, kwa Sababu ya maambukizi kuenea sehemu mbalimbali tumbo uanza kuuma hasa chini ya kitovu kwa hiyo mtoto kama hawezi kuongea ukimgusa kwenye tumbo anasikia maumivu lakini wale wenye uwezo wa kuongea wanaweza kuponyesha dalili.

 

5.Maumivu wakati wa kukojoa

Hii ni dalili mojawapo kwa mtoto Mwenye dalili ya UTI, kwa Sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na bakteria wameshaharibu kibofu mtoto usikia maumivu makali wakati wa kukojoa na pengine uanza kulia Lia kwa sababu ya maumivu.hapa mtoto kama anaweza kuongea atakwambia kama hawezi utaona analia wakati wa kukojoa.

 

6. Kiasi Cha kikohoa kwa mtoto kuongezeka.

Hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, kwa hiyo kibofu Cha mkojo hushindwa kutunza mkojo kwa mda mrefu na halimaye mkojo uanza kutoka mara kwa mara. Kwa hiyo hii Dalili ukolijitokeza mama inabidi awe makini kwenda kwenye vipimo Ili kuangalia kama Kuna UTI au la.

Angalisho: hapo juu ni Dalili za UTI kwa watoto iwapo mtoto atapatwa na dalili hizo usinunue dawa kumpatia ukadhani mara Moja ni UTI Bali inabidi kuchukua vipimo maana hizo Dalili uweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 9882

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

MALARIA NI NINI? NI WATU WANGAPI WANAKUFA KWA MALARIA DUNIANI

Malaria ni katika maradhi yanayosumbua sana na kusababisha maradhi ya watu wengi sana duniani.

Soma Zaidi...
Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanawake na wanaumr?

Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu. Ni katika maumivu amaboyo kwa wanaume mara nyingi huhusishwa an ngiri na kwa upande wa wanawake huhusishwa na chango hasa pale wanapokaribia kuingia katika siku zao. Ma

Soma Zaidi...
Vyakula vinavyosaidia afya ya ubongo

Je, umewahi kuhisi ukungu wa akili (brain fog) au kusahau mambo madogo madogo? Ubongo ndio injini ya mwili wako, na unahitaji mafuta sahihi ili kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Makala hii inajadili vyakula vitano muhimu vilivyothibitishwa kisayansi kuboresha kumbukumbu, kuongeza umakini, na kulinda ubongo wako dhidi ya kuzeeka

Soma Zaidi...
Saratani ya Matiti ya wanaume.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ya matiti ya Mwanaume ni Saratani nadra ambayo hutokea katika tishu za matiti za wanaume. Ingawa saratani ya matiti hufikiriwa zaidi kuwa ugonjwa wa wanawake, saratani ya matiti ya mwanaume hutokea. Saratani y

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo mviringo (ascariasis)

Ascariasis ni aina ya maambukizi ya minyoo mviringo. Minyoo hii ni vimelea wanaotumia mwili wako kama mwenyeji kukomaa kutoka kwa mabuu au mayai hadi minyoo wakubwa. Minyoo ya watu wazima, ambayo huzaa, inaweza kuwa zaidi ya futi (sentimita 30) kwa

Soma Zaidi...
Athari za unywaji pombe na sigara wakati wa ujauzito.

Ujauzito ni kipindi muhimu ambacho afya ya mama huathiri moja kwa moja ukuaji na ustawi wa mtoto aliye tumboni. Makala hii inachunguza kwa kina madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya pombe na sigara wakati wa ujauzito. Tunajadili jinsi vitu hivi vinavyovuka kizuizi cha plasenta (placenta) na kuathiri mfumo wa neva, viungo, na ukuaji wa mtoto, huku tukitoa ushauri wa kitaalamu wa jinsi ya kuacha tabia hizi kwa ajili ya usalama wa mtoto na mama.

Soma Zaidi...