picha

Dalili za tezi dume.

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.

Dalili za tezi dume.

1. Kwanza kabisa Mgonjwa anaweza kupata tatizo la kukojoa mkojo ukiwa pamoja na damu.

Kwa kuwepo kwa Maambukizi ambayo kwa kiasi kikubwa yanakuwa yameshambuliwa sehemu za tezi kwa hiyo mkojo ukitoka unakuwa na damu.

 

2. Pengine uume unashindwa kabisa kusimama au ukisimama ni kwa shida na hauchukui mda mrefu.

Kwa sababu sehemu za mishipa ambayo inakuwa imeshikilia uume ili usimame wakati wa kujamiiana ushambuliwa kwa hiyo inakuwa haina nguvu ya kufanya uume usimame.

 

3. Kuhisi kukojoa mara kwa mara hasa wakati wa usiku.

Hali hiyo utokea kwa sababu ya sehemu za kibofu na mishipa yake ambayo utumika kuruhusu mkojo kutoka nje huwa imelegea kwa sababu ya kuenea kwa Maambukizi kwenye mfumo wa utunzaji wa mkojo kwa hiyo Mgonjwa ukojoa sana hasa wakati wa usiku kwa sababu usiku kila mfumo unakua umetulia vizuri kabisa.

 

4. Pia wakati wa kukojoa mkojo utoka kwa mtiririko dhaifu.

Kwa sababu ya kuenea kwa Maambukizi na mishipa ya kibofu nayo ulegea kwa hiyo na spidi ya mkojo upungua.

 

5. Kupata maumivu kwenye kibofu cha mkojo na kutilia kwa mkojo baada ya kukojoa .

Kwa hiyo utamkita mtu anahangaika anapokuwa anakojoa na pia kwa wakati mwingine mkojo unaweza kutiririka chini hata kwenye nguo na ukiwa kidogo kidogo.

 

6.Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi mtu anapaswa kuwahi hospitalini mara moja ili kuweza kupata matibabu haraka kwa sababu kama shida haijakuwa kubwa walau matibabu yanaweza kusaidia chochote na pia tunapaswa kujua kuwa sio Dalili zote ni za tezi dume ili kuhakikisha ni lazima kwenda hospitalini.

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2285

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA

Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.

Soma Zaidi...
Huduma kwa wasioona hedhi

Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.

Soma Zaidi...
TATIZO LA KUVIMBA KWA USO NA MIGUU KWA WAJAWAZITO

KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.

Soma Zaidi...
Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?

Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.

Soma Zaidi...
Nimetoka kufanya tendo la ndoa ghafla tumbo likaanza kukaza upande wa kushoto na kutoka maji yenye uzito wa kawaida kama ute mengi je hii itakuwa ni nini

Maumivu yavtumbo huwenda yakachanganya sana, Keane yanahusianana sababu nyingi sana. Kina baadhi ya watu hupata na maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa ama punde tu baada ya kumaliza.

Soma Zaidi...