Dalili za tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Dalili za tezi dume.
1. Kwanza kabisa Mgonjwa anaweza kupata tatizo la kukojoa mkojo ukiwa pamoja na damu.
Kwa kuwepo kwa Maambukizi ambayo kwa kiasi kikubwa yanakuwa yameshambuliwa sehemu za tezi kwa hiyo mkojo ukitoka unakuwa na damu.
2. Pengine uume unashindwa kabisa kusimama au ukisimama ni kwa shida na hauchukui mda mrefu.
Kwa sababu sehemu za mishipa ambayo inakuwa imeshikilia uume ili usimame wakati wa kujamiiana ushambuliwa kwa hiyo inakuwa haina nguvu ya kufanya uume usimame.
3. Kuhisi kukojoa mara kwa mara hasa wakati wa usiku.
Hali hiyo utokea kwa sababu ya sehemu za kibofu na mishipa yake ambayo utumika kuruhusu mkojo kutoka nje huwa imelegea kwa sababu ya kuenea kwa Maambukizi kwenye mfumo wa utunzaji wa mkojo kwa hiyo Mgonjwa ukojoa sana hasa wakati wa usiku kwa sababu usiku kila mfumo unakua umetulia vizuri kabisa.
4. Pia wakati wa kukojoa mkojo utoka kwa mtiririko dhaifu.
Kwa sababu ya kuenea kwa Maambukizi na mishipa ya kibofu nayo ulegea kwa hiyo na spidi ya mkojo upungua.
5. Kupata maumivu kwenye kibofu cha mkojo na kutilia kwa mkojo baada ya kukojoa .
Kwa hiyo utamkita mtu anahangaika anapokuwa anakojoa na pia kwa wakati mwingine mkojo unaweza kutiririka chini hata kwenye nguo na ukiwa kidogo kidogo.
6.Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi mtu anapaswa kuwahi hospitalini mara moja ili kuweza kupata matibabu haraka kwa sababu kama shida haijakuwa kubwa walau matibabu yanaweza kusaidia chochote na pia tunapaswa kujua kuwa sio Dalili zote ni za tezi dume ili kuhakikisha ni lazima kwenda hospitalini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Je chuchu zikiwa nyeusi Nini kinasababisha,, kando ya kuwa mjamzito? Na Kama sio mjamzito sababu ya chuchu kua nyeusi ni nini
Chuchu kubadilika range ni mojavkatika mabadiliko ambayo huwapa shoka wengi katika wasichana. Lucinda nikwambie tu kuwa katika hali ya kawaida hilo sio tatizo kiafya.
Soma Zaidi...Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba
Soma Zaidi...Mabadiliko ya Matiti kwa Mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuacha kupiga punyeto.
Post hii inakwenda kukupa njia za kukusaidia kuacha punyeto.
Soma Zaidi...Changamoto za ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu
Soma Zaidi...Kuwepo kwa maziwa wakati wa ujauzito.
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa maziwa kwa akina Mama wakati wa ujauzito ni kawaida kwa sababu ya kuzaliwa kwa homoni ambayo usaidia kutoa maziwa.
Soma Zaidi...