Dalili za ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
Dalili za ugonjwa wa Bawasili.
1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.
3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.
4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,
Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.
Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.
6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.
7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Dalili za fangasi ukeni
Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri.
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya mapafu
Saratani ya Mapafu ni aina ya Kansa inayoanzia kwenye mapafu. Mapafu yako ni viungo viwili vya sponji kwenye kifua chako ambavyo huchukua oksijeni unapovuta na kutoa kaboni dioksidi unapotoa nje.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI
Soma Zaidi...Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga
Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali
Soma Zaidi...Makundi ya watu walio katika hatari ya kupata Ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi,ni kutokana na kazi zao pamoja na mazingira yao kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa ukimwi.
Soma Zaidi...VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)
Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.
Soma Zaidi...