Dalili za ugonjwa wa Donda koo
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na
Dalili za ugonjwa wa Donda Koo.
1. Kuwepo kwa vidonda kooni.
Hali hii utokea kwa mgonjwa mwenye Donda Koo kw kuwepo kwa vidonda kooni ni kwa sababu ya maambukizi ya bakteria ambao ushambulia Koo na kusababisha vidonda na kwa kiwango kikubwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wenye Chini ya umri wa miaka mitano kwa hiyo baada ya kutambua Dalili hii mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi.
2. Mgonjwa huwa na makamasi yaliyochanganywa na damu.
Hii ni mojawapo ya dalili ya Dondakoo kwa watoto tukumbuke kuwa ugonjwa huu ushambulia sana sehemu za mfumo wa hewa baada ya bakteria kushambulia sehemu za mfumo wa hewa usababisha michubuko kwenye mfumo na kwa sababu ya maambukizi mafua uwepo yakiandamana na damu iliyotoka kwenye sehemu za maambukizi.
3. Kuwepo kwa utando kwenye Koo.
Kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria usababisha utando kwenye Koo la mtoto ambapo hali hii usababisha mtoto hashindwe kunyonya au kumeza kitu chochote na mtoto upumua kwa shida, kwa hiyo tunaona ugonjwa huu ulivyo mbaya kwa watoto tunapaswa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili kuepusha madhara makubwa zaidi kama kuwepo kwa utando kwenye Koo. Ambao huzuia mtoto ashindwe kumeza.
4, Maumivu makali ya shingo.
Kwa upande wa mtoto kunakuwepo maumivu makali ya shingo kwa sababu ya kuenea kwa bakteria ambao usambaza maumivu kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye shingo na Mtoto uhisi maumivu makali na pengine kushindwa kugeuka kwa hiyo tunapaswa kuzingatia chanjo kwa ajili ya kuepuka madhara makubwa kama hayo.
5. Kuvimba kwa shingo na kusababisha shingo kuwa kubwa ambayo umnyima mtoto amani na kumfanya mtoto aanze kulia mda wote na kitendo Cha mgonjwa kuvimba shingo huitwa shingo ngoti Ili kuitofautisha na matimbwitimbwi kwa hiyo jamii inabidi kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu na kuhakikisha kila mtoto anapata chanjo Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayotokea kwa mtoto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Mambo ya kuzingatia kabla ya upasuaji,
Upasuaji ni kundi la ki medical linalohusu kutoa kiungo kisichohitajika kwenye mwili.
Soma Zaidi...Dalilili za kidole tumbo (appendicitis)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa Kidole ambao kitaalamu hujulikana Kama Appendicitis. Kidole tumbo husababisha maumivu kwenye tumbo la chini la kulia. Hata hivyo, kwa watu wengi, maumivu huanza karibu na kitovu na kisha kusonga. Kadiri uvi
Soma Zaidi...Njia za kutibu saratani
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kumfurahisha Mwenza Wako
Mahusiano yenye furaha hayajitokezi kwa bahati; yanajengwa kupitia juhudi za makusudi. Posti hii inatoa mwongozo wa mbinu rahisi lakini zenye nguvu za kumfanya mwenza wako ajihisi anathaminiwa, anapendwa, na anafurahia maisha ya pamoja nawe.
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya koo
Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.
Soma Zaidi...Ujuwe ugonjwa wa ebola, dalili zake na jinsi unavyoweza kusambazwa.
Posti hii inahusu sana kuhusu ugonjwa wa ebora. Ugonjwa huu usababishwa na virusi.Virusi hivyo husababisha kutokwa na damu nyingi mwilini kutokana na kupasuka kwa mishipa ya damu
Soma Zaidi...