picha

Dalili za ugonjwa wa Donda koo

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na

Dalili za ugonjwa wa Donda Koo.

1. Kuwepo kwa vidonda kooni.

Hali hii utokea kwa mgonjwa mwenye Donda Koo kw kuwepo kwa vidonda kooni ni kwa sababu ya maambukizi ya bakteria ambao ushambulia Koo na kusababisha vidonda na kwa kiwango kikubwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wenye Chini ya umri wa miaka mitano kwa hiyo baada ya kutambua Dalili hii mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi.

 

2. Mgonjwa huwa na makamasi yaliyochanganywa na damu.

 

Hii ni mojawapo ya dalili ya  Dondakoo kwa watoto tukumbuke kuwa ugonjwa huu ushambulia sana sehemu za mfumo wa hewa baada ya bakteria kushambulia sehemu za mfumo wa hewa usababisha michubuko kwenye mfumo na kwa sababu ya maambukizi mafua uwepo yakiandamana na damu iliyotoka kwenye sehemu za maambukizi.

 

3. Kuwepo kwa utando kwenye Koo.

Kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria usababisha utando kwenye Koo la mtoto ambapo hali hii usababisha mtoto hashindwe kunyonya  au kumeza kitu chochote na mtoto upumua kwa shida, kwa hiyo tunaona ugonjwa huu ulivyo mbaya kwa watoto tunapaswa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili kuepusha madhara makubwa zaidi kama kuwepo kwa utando kwenye Koo. Ambao huzuia mtoto ashindwe kumeza.

 

4, Maumivu makali ya shingo.

Kwa upande wa mtoto kunakuwepo maumivu makali ya shingo kwa sababu ya kuenea kwa bakteria ambao usambaza maumivu kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye shingo na Mtoto uhisi maumivu makali na pengine kushindwa kugeuka kwa hiyo tunapaswa kuzingatia chanjo kwa ajili ya kuepuka madhara makubwa kama hayo.

 

5. Kuvimba kwa shingo na kusababisha shingo kuwa kubwa ambayo umnyima mtoto amani na kumfanya mtoto aanze kulia mda wote na kitendo Cha mgonjwa kuvimba shingo huitwa shingo ngoti Ili kuitofautisha  na matimbwitimbwi kwa hiyo jamii inabidi kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu na kuhakikisha kila mtoto anapata chanjo Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayotokea kwa mtoto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5977

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.

Soma Zaidi...
Dalili za kuvunjika kwa nyonga

Kuvunjika kwa nyonga ni jeraha kubwa, na matatizo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha. Hatari ya kupasuka kwa nyonga huongezeka na umri.

Soma Zaidi...
Vyakula Vinavyosaidia Afya ya Uzazi kwa Mwanamke: Mwongozo wa Lishe Bora

Muhtasari (Executive Summary) ​Afya ya uzazi ya mwanamke inategemea kwa kiasi kikubwa uwiano wa vichocheo mwilini (hormonal balance), afya ya mayai (oocytes), na mazingira salama ya mfuko wa uzazi. Lishe duni inaweza kusababisha matatizo kama kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi au ugumu wa kupata ujauzito. Makala haya yanachambua vyakula vya asili vinavyosaidia kuimarisha mfumo wa uzazi wa mwanamke, kuboresha ute wa uzazi, na kuongeza nafasi ya kushika ujauzito kwa njia salama.

Soma Zaidi...
Njia za kuangalia sehemu yenye maumivu

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia sehemu yenye maumivu, hili kugundua mahali mtu anaumia ushirikiano mkubwa unahitajika kati ya mgonjwa na mhudumu.

Soma Zaidi...
Namna ya Kumtunza Mtoto Njiti

​Kumtunza mtoto aliyezaliwa kabla ya muda (mtoto njiti) kunahitaji umakini mkubwa, uvumilivu, na upendo. Post hii inatoa mwongozo muhimu kuhusu huduma za msingi nyumbani, ikiwa ni pamoja na joto, lishe, na usafi, ili kuhakikisha mtoto anakua na kuwa na afya njema.

Soma Zaidi...