picha

Dalili za ugonjwa wa Donda koo

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na

Dalili za ugonjwa wa Donda Koo.

1. Kuwepo kwa vidonda kooni.

Hali hii utokea kwa mgonjwa mwenye Donda Koo kw kuwepo kwa vidonda kooni ni kwa sababu ya maambukizi ya bakteria ambao ushambulia Koo na kusababisha vidonda na kwa kiwango kikubwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wenye Chini ya umri wa miaka mitano kwa hiyo baada ya kutambua Dalili hii mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi.

 

2. Mgonjwa huwa na makamasi yaliyochanganywa na damu.

 

Hii ni mojawapo ya dalili ya  Dondakoo kwa watoto tukumbuke kuwa ugonjwa huu ushambulia sana sehemu za mfumo wa hewa baada ya bakteria kushambulia sehemu za mfumo wa hewa usababisha michubuko kwenye mfumo na kwa sababu ya maambukizi mafua uwepo yakiandamana na damu iliyotoka kwenye sehemu za maambukizi.

 

3. Kuwepo kwa utando kwenye Koo.

Kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria usababisha utando kwenye Koo la mtoto ambapo hali hii usababisha mtoto hashindwe kunyonya  au kumeza kitu chochote na mtoto upumua kwa shida, kwa hiyo tunaona ugonjwa huu ulivyo mbaya kwa watoto tunapaswa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili kuepusha madhara makubwa zaidi kama kuwepo kwa utando kwenye Koo. Ambao huzuia mtoto ashindwe kumeza.

 

4, Maumivu makali ya shingo.

Kwa upande wa mtoto kunakuwepo maumivu makali ya shingo kwa sababu ya kuenea kwa bakteria ambao usambaza maumivu kwenye sehemu mbalimbali kama vile kwenye shingo na Mtoto uhisi maumivu makali na pengine kushindwa kugeuka kwa hiyo tunapaswa kuzingatia chanjo kwa ajili ya kuepuka madhara makubwa kama hayo.

 

5. Kuvimba kwa shingo na kusababisha shingo kuwa kubwa ambayo umnyima mtoto amani na kumfanya mtoto aanze kulia mda wote na kitendo Cha mgonjwa kuvimba shingo huitwa shingo ngoti Ili kuitofautisha  na matimbwitimbwi kwa hiyo jamii inabidi kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu na kuhakikisha kila mtoto anapata chanjo Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayotokea kwa mtoto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5260

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dalili za fangasi wa kucha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili,sababu za Hatari,na namna ya kujizuia na fangasi wa kucha.

Soma Zaidi...
Ujue ugonjwa wa kuishiwa na damu

post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuishiwa damu kwa kitaalamu huitwa(Anemia) ni ugonjwa wa kuishiwa na damu mwilini na kusababisha maisha ya mtu kuwa hatarini

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuepuka minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuiepuka minyoo

Soma Zaidi...
Njia za kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi njia mbali mbali ambazo uweza kitumiwa na wataalamu ili kuweza kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Athari za kutokutibu minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya athari zinazoweza kutokea endapo minyoo haitotibiwa

Soma Zaidi...