picha

Dalili za Ugonjwa wa ini

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa inni, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye ugonjwa wa inni, Dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.

Dalili za ugonjwa wa inni

1. Macho na ngozi ya viganja,  na nyayo za miguuni kubadilika rangi na kuwa ya njano. 

Kwa mtu Mwenye maambukizi kwenda ini rangi ya viganja na nyayo za miguuni kubadilika na kuwa na rangi ya njano hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye ini maambukizi haya uenea sana kwenye sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha baadhi ya sehemu ya mwili kuwa ya njano, kwa hiyo baada ya mtu kuona dalili kama hizi zinatokea anapaswa kwenda mapema hospitalini kwa ajili ya kuchukua vipimo kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za mtu Mwenye Homa ya inni kwa kuangalia dalili ya Aina hii.

 

2. Mara nyingine na rangi ya mkojo ubadilika na kuwa na rangi ya njano.

Kwa watu walio wengi ambao wamashambuliwa na ugonjwa huu rangi ya mkojo nayo ubadilika na kuwa na rangi ya njano, hali hii ni kwa sababu ya maambukizi hasa kama yameingia sana kwenye mwili usambaa mpaka kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha rangi ya mkojo kubadilika kuwa na rangi ya njano, kwa hiyo kitu ambacho tunapaswa kufanya ni kwamba baada ya kuona dalili kama hii tunapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kujua uhakika kama ni maambukizi kwenye ini au ni magonjwa mengine na kwa wale ambao hawanywi maji  pengine wanaweza kupata na tatizo hili la rangi ya mkojo kuwa ya njano kwa hiyo tunapaswa kupima Ili kujua afya zetu mara kwa mara.

 

3. Kwa watu wenye maambukizi kwenye inni kinyesi Chao uwa na utando mweupe mweupe ambao ufanana na Ute , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi zinaambatana mtu anapaswa kumpelekwa hospitalini kwa ajili ya kupima na kuhakikisha kuwa kama ni maambukizi ya ugonjwa wa inni, kwa hiyo vipimo ni vya lazima kwa sababu kwa vipimo tunaweza kujua maambukizi ya gonjwa hili la inni na kuchukua tahadhari Ili kuepuka kuwaambukiza wengine.

 

4. Dalili nyingine ni kama vile kupoteza hamu ya chakula kwa sababu maambukizi yanakuwa yameenea sehemu mbalimbali za mwili ambapo mtu upoteza na Ile hamu ya Kawaida ya kupata chakula hali hii ya kupoteza hamu ya kula usababisha na mgonjwa wa Homa ya inni kuishiwa nguvu mara kwa Mara na pengine anapotaka kula chakula uhisi kichefuchefu na kutapika  hai hii usababishwa na kitendo Cha kuongezeka kwa maambukizi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3550

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Upungufu wa madini ya chuma mwilini: Dalili zake.

Upungufu wa madini ya chuma mwilini (Iron Deficiency) ni miongoni mwa changamoto kubwa zaidi za kilishe duniani, inayopelekea ugonjwa wa upungufu wa damu (Iron Deficiency Anemia - IDA). Makala haya ya kitaalamu yanaangazia kwa kina dalili kuu na za nadra za hali hii, ikiwa ni pamoja na uchovu sugu, kupauka kwa ngozi, na matamanio ya vitu visivyo vya chakula (pica). Aidha, yanajadili makundi yaliyo katika hatari kubwa, mbinu za kisayansi za utambuzi wa kimaabara kupitia viwango vya ferritin na hemoglobin, pamoja na mikakati ya kuzuia na kutibu tatizo hili kupitia lishe bora na virutubisho kwa mujibu wa miongozo ya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Soma Zaidi...
Vyakula Vinavyoongeza Kinga ya Mwili.

​Blogu hii inaangazia umuhimu wa lishe bora katika kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Tutajadili vyakula mahususi vyenye virutubisho muhimu, umuhimu wa vitamini na madini, pamoja na ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi lishe inavyochangia afya yako kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Je, unaweza kupata mimba siku chache baada ya hedhi kuisha?

Jibu fupi ni ndiyo, inawezekana. Ingawa watu wengi huamini kuwa huwezi kupata ujauzito mara tu baada ya hedhi, uhalisia wa kibiolojia unaonyesha kuwa dirisha la uzazi linaweza kufunguka mapema kuliko unavyotarajia. Makala hii inaelezea jinsi mzunguko wa hedhi unavyofanya kazi na kwa nini ni muhimu kuwa makini wakati wote.

Soma Zaidi...
Ute wa uzazi and uhusiano wake na kupata ujauzito.

Kuelewa mifumo ya mwili wako ni hatua muhimu kwa mwanamke anayepanga kupata ujauzito. Ute wa uzazi (cervical mucus) ni kiashirio cha asili ambacho mwanamke anaweza kukitumia kubaini siku zake za hatari (ovulation). Makala hii inaelezea umuhimu wa ute huu, jinsi ya kuutambua, na jinsi unavyomsaidia mwanamke kuongeza nafasi za kupata ujauzito.

Soma Zaidi...