picha

Dalili za Ugonjwa wa ini

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa inni, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye ugonjwa wa inni, Dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.

Dalili za ugonjwa wa inni

1. Macho na ngozi ya viganja,  na nyayo za miguuni kubadilika rangi na kuwa ya njano. 

Kwa mtu Mwenye maambukizi kwenda ini rangi ya viganja na nyayo za miguuni kubadilika na kuwa na rangi ya njano hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye ini maambukizi haya uenea sana kwenye sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha baadhi ya sehemu ya mwili kuwa ya njano, kwa hiyo baada ya mtu kuona dalili kama hizi zinatokea anapaswa kwenda mapema hospitalini kwa ajili ya kuchukua vipimo kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za mtu Mwenye Homa ya inni kwa kuangalia dalili ya Aina hii.

 

2. Mara nyingine na rangi ya mkojo ubadilika na kuwa na rangi ya njano.

Kwa watu walio wengi ambao wamashambuliwa na ugonjwa huu rangi ya mkojo nayo ubadilika na kuwa na rangi ya njano, hali hii ni kwa sababu ya maambukizi hasa kama yameingia sana kwenye mwili usambaa mpaka kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha rangi ya mkojo kubadilika kuwa na rangi ya njano, kwa hiyo kitu ambacho tunapaswa kufanya ni kwamba baada ya kuona dalili kama hii tunapaswa kwenda hospitalini kupima Ili kujua uhakika kama ni maambukizi kwenye ini au ni magonjwa mengine na kwa wale ambao hawanywi maji  pengine wanaweza kupata na tatizo hili la rangi ya mkojo kuwa ya njano kwa hiyo tunapaswa kupima Ili kujua afya zetu mara kwa mara.

 

3. Kwa watu wenye maambukizi kwenye inni kinyesi Chao uwa na utando mweupe mweupe ambao ufanana na Ute , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi zinaambatana mtu anapaswa kumpelekwa hospitalini kwa ajili ya kupima na kuhakikisha kuwa kama ni maambukizi ya ugonjwa wa inni, kwa hiyo vipimo ni vya lazima kwa sababu kwa vipimo tunaweza kujua maambukizi ya gonjwa hili la inni na kuchukua tahadhari Ili kuepuka kuwaambukiza wengine.

 

4. Dalili nyingine ni kama vile kupoteza hamu ya chakula kwa sababu maambukizi yanakuwa yameenea sehemu mbalimbali za mwili ambapo mtu upoteza na Ile hamu ya Kawaida ya kupata chakula hali hii ya kupoteza hamu ya kula usababisha na mgonjwa wa Homa ya inni kuishiwa nguvu mara kwa Mara na pengine anapotaka kula chakula uhisi kichefuchefu na kutapika  hai hii usababishwa na kitendo Cha kuongezeka kwa maambukizi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3616

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 web hosting     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu

Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu

Soma Zaidi...
Dalili za mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi dalili za mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...
Dalili zinazoonyesha joto la kupungua mwilini (hypothermia)

joto la mwili wako linapungua, moyo wako, mfumo wa neva na viungo vingine haviwezi kufanya kazi kwa kawaida. Isipopotibiwa, Hypothermia hatimaye inaweza kusababisha moyo wako na mfumo wa upumuaji kushindwa kabisa na hata kifo.

Soma Zaidi...
Tofauti ya dalili za mafua ya kawaida na COVID-19.

​Katika ulimwengu wa sasa, kuelewa tofauti kati ya mafua ya kawaida (common cold) na COVID-19 ni muhimu kwa ajili ya usalama wako na wa jamii inayokuzunguka. Ingawa magonjwa yote mawili husababishwa na virusi na kushambulia mfumo wa upumuaji, yana tofauti muhimu katika jinsi yanavyoanza, muda wake, na dalili zake mahususi. Makala haya yanakupa mwongozo wa kulinganisha dalili ili uweze kuchukua hatua sahihi za kiafya.

Soma Zaidi...
HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO

HATUA ZA KUJIKINGA NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupunguza hatari yako ya vidonda vya tumbo ikiwa unafuata mikakati sawa inayopendekezwa kama tiba ya nyumbani kutibu vidonda.

Soma Zaidi...
Tatizo la kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa.

Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa (post-coital bleeding) ni hali inayoweza kuleta hofu kwa wanawake wengi. Ingawa mara nyingi sababu zake si za kutisha, ni muhimu kuelewa visababishi mbalimbali vinavyoweza kuashiria matatizo ya kiafya yanayohitaji matibabu. Makala hii inachunguza kwa kina sababu za kibiolojia, maambukizi, na magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii, ikitoa mwongozo wa wakati wa kumwona daktari.

Soma Zaidi...