Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

DALILI ZA UKIMWI NA HIV KWENYE ULIMU NA MDOMO

 

HIV hivi ni virusi vilivyopata umaarufu sana kwa kufahamika kuwa ndio virusi pekee vinavyoweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini yaani UKIMWI. Virusi hivi anaweza kuvipata binadamu yeyote yule. Zipo njia nyingi ambazo unaweza kupata virusi hivi kama kushiriki ngono zembe, kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kijifungua, kushiriki vitu vyenye ncha kali, kupewa damu yenye virusi, na njia nyingine kibao. Dalili za HIV na UKIMWI zinatofautiana kulingana na hatua ya mgonjwa. Lanini kuna wakati Ulimi na Mdomo kuweza kuonyesha dalili hizi wazi wazi.

 

Dalili za HIV na UKIMWI kupitia mdomoni zinaweza kuwa ni dalili za mwanzoni sana za UKIMWI kwa baadhi ya watu. Ukweli ni kuwa dalili hizi zinaweza kumpata yeyote lakini kuna watu wapo hatarini zaidi kama watoto wachanga, wazee na watu wenye upungufu wa kinga yaani UKIMWI. Dalili hizi tutaziona moja hadi nyingine hapo chini.

 

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi1.Kukauka kwa mdomo na kuoza kwa meno.Virusi vya HIV vinaweza kupelekea mdomo kukauka na kukosa mate ya kutosha. Hivyo miongoni mwa kazi za mate ni kulinda meno na mdomo. Hivyo kupelekea meno kuoza. Ni vyema mgonjwa kama anatatizo hili kuonana na daktari aweze kumpa ushauri. Unaweza kutumia dawa maalumu kwa ajili ya kuchochea mate ama kutafuna bigji ambazo hazina sukari.

 

2.Kupata fangasi wa kwenye mdomo wajulikanao kama candidiasis (thrush).Fangasi hawa wanaweza kusababisha madoa mekundu kwenye ulimi, ama mdoa meupe kwenye mdomo. Pia wanaweza kusababisha kupasuka kwa kona za mdomo na kutengeneza weupe kwenye kona za mdomo. Pia mdomoni kunaweza kuta buda la nyama lisilokuwa na maumivu. Fangasi hawa wanaweza kuhamia kwenye koo na kusababisha maumivu. Fangasi hawa ni rahisi sana kuondoka baada ya matibabu ila kwa baadhi ya sababu wanaweza kuwa sugu.

 

3.Vidonda kwenye mdomo na ulimiHivi ni vijidonda vijidogo ambavyo vipo duara. Vinaweza kutokea kwenye ulimi na kwenye mashavu kwa ndani. Pia vinaweza kutokea nyuma ya koo. Vidonda hivi vinakuwa na rangi nyekunu pembeni na rangi ya kijivu katikati. Misongo ya mawzo na baadhi ya vyakula vinaweza kuwa ni sababu.

 

4.Vidonda vya homa.Kama umeshawahi kushuhudia vidonda ambavyo vinatokana na homa. Vidonda hivi kwa watu wenye UKIMWI vina tabia ya kujirudia mara kwa mara. Dawa za ART huweza kusaidia hali hii kutotokea.

 

5.Maradhi ya ufinzi ama periodontitis or gingivitisHaya ni maradhi ya ufizi ambapo ufinzi unakosa nguvu na kushindwa kuzuia meno vyema. Hal hii inaweza kupelekea kung’oka kwa meno. Hali hii inaweza tokea mapema sana miezi 18 baada ya kupata HIV. Ukavu kwenye mdomo, kuvuta sigara kunaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi.

 

6.Kuota kwa kambakamba ama vinywele vinywele kwenye ulimi na pembeni ya ulimi.Kitaalamu hivi hujulikana kama Hairy Leukoplakia. Vikambakamba ama vinyweleo nyweleo hivi havina maumivu lakini pia haviwezi kutoka hata kwa kupiga mswaki. Hii inaweza kuwa ni katika dalili za mwanzo zaidi za UKIMWI. Vyenyewe vipo na rangi nyeupe

 

7.Madoa ya rangi ya dhambarau iliyowiva ama nyekundu kwenye mafinzi, sehemu ya juu ya mdomo na nyuma ya ulimi. Kitaalamu hufahamika kama Kaposi’s Sarcoma (KS Hii inaweza kuwa ni dalili ya kwanza kwa mtu ambaye hajapima HIV. Na kwa ambaye ameshaanza kutumia dawa dalili hizi ni si rahisi kujionyesha.

 

8.Kuota chunjua kwenye mdomo,na ulimi. Hizi husababishwa na virusi vinavyojulikana kama Human Papillomavirus, HPV. Kikawaida chunjua inaweza kuota popote pale kwenye mwili hasa hasa hutokea mara nyingi kwenye mikono. Watu wenye HIV chunjia hizi huweza kuvamia ulimi na kuhama maeneo mengine kwenye mdomo. Pia baadhi ya virusi wanao;eta hali hii wanaweza kusababisha saratani.

 

Mwisho nikufahamishe tu kuwa mdomo ni katika sehemu za kwanza kuonyesha dalili za HIV na UKIMWI. Ni vyema kwenda kupima endapo utagundua una moja ya dalili hizo hapo juu

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 3914

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanaume

Posti hii inakwenda kukuletea dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanaume

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia Ugonjwa wa tauni.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka Ugonjwa wa raundi.

Soma Zaidi...
Fahamu Dalili za Ugonjwa wa Bawasiri

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Bawasiri. Bawasiri ni mishipa iliyovimba kwenye njia yako ya haja kubwa na sehemu ya chini ya puru. Bawasiri inaweza kutokana na kukaza mwendo wakati wa kwenda haja ndogo au kutokana na shinikizo la kuongeze

Soma Zaidi...
SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE

Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala

Soma Zaidi...
Elimu kuhusu HIV na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jipu la Jino

Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.

Soma Zaidi...
Fahamu ugonjwa wa Varicose vein

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa vericose veini, hili ni tatizo ambalo utokea katika mzunguko wa damu hasa kwenye miguu.

Soma Zaidi...
Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

Soma Zaidi...
AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.

Soma Zaidi...