picha

Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3729

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 ai web app     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu

Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu

Soma Zaidi...
Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.

Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe.

Soma Zaidi...
Dalili na namna ya kujizuia na malaria

Postii hii inshusiana na dalili na ishara za kujikinga au kuzuia malaria kwa Njia mbalimbali.

Soma Zaidi...
Dalili za tonsillitis (mafindo mafindo)

Tonsillitis kwa kiswahili hujulikana kama mafundomafundo ambayo hutokea pande mbili karibu na Koo na huwa na uvimbe na zikikaa kwa muda bila matibabu hutoa usaha.Dalili na dalili za ugonjwa wa tonsillitis ni pamoja na

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa yanayosababisha madhara kwenye mapafu na kitaalamu hujulikana Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake

Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.

Soma Zaidi...