picha

Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3890

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰2 web hosting     ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi ya sikio kwa watoto

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za maambukizi ya sikio kwa watoto.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Mwenye Kikohozi

Kikohozi ni njia ya asili ya mwili kujisafisha, lakini kwa mtoto, inaweza kuwa chanzo cha usumbufu mkubwa na wasiwasi kwa wazazi. Post hii inatoa mbinu salama na za nyumbani za kumsaidia mtoto kupata nafuu, huku ikielekeza dalili za hatari zinazohitaji msaada wa kitabibu haraka.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya magonjwa ya ngono

Posti hii inahusu athari za maambukizi ya magonjwa ya ngonoย  ambapo magonjwa ya ngono isipokuwa UKIMWIย  yanatibika .mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitali au kituo chochote cha afya kupata matibabu mara anapoona dalili za magonjwa haya.

Soma Zaidi...
Njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Soma Zaidi...
Kuumwa na mgongo: Matatizo ya disc na jinsi ya kuepuka upasuaji.

โ€‹Maumivu ya mgongo ni mojawapo ya changamoto kubwa za kiafya zinazomkabili binadamu wa karne ya 21. Kati ya visababishi vikuu, matatizo ya diski za mgongo (spinal disc issues) yanashika nafasi ya juu. Makala hii inatoa mwongozo wa kina kuhusu namna diski zinavyofanya kazi, nini kinatokea zinapoharibika, na muhimu zaidi, mikakati ya kitabibu na mazoezi yanayoweza kukusaidia kuepuka njia ya upasuaji na kurejesha ubora wa maisha yako.

Soma Zaidi...
Dondoo muhimu ya ki afya.

Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu ya ki afya, ni maelekezo ambayo utolewa ili kuweza kuzifanya afya zetu ziwe bora zaidi na kuepuka madhara yoyote ya ki afya

Soma Zaidi...