picha

Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3852

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 ai web app     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Madhara ya Tiba kemikali kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba kemikali, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wa saratani, madhara haya yanayoweza kuwa ni kwa Sababu mbalimbali kama vile kuaribika kwa seli zinazoendelea kufanya kazi kwenye mwili.

Soma Zaidi...
Matibabu ya vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.

Soma Zaidi...
Maradhi ya macho

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake

Soma Zaidi...
Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dadili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu ambao kitaalamu hujulikana Kama multiple sclerosis.

Soma Zaidi...
AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.

Soma Zaidi...
Madhara ya minyoo

Somo hili linakwenda kukuletea madhara ya minyoo

Soma Zaidi...