picha

Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-11-05 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 3348

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?

Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi Mdomoni.

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za fangasi Mdomoni kwa watoto, vijana, watu wazima na mama wanaonyonyeshwa.

Soma Zaidi...
Masharti ya vidonda vya tumbo

Haya ni masharti ya mwenye vidonda vya tumbo. Mgojwa wa vidonda vya hatumbo hatakiwi kufanya yafuatayo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono, sababu zake nanjia za kujilinda.

Kisonono husababishwa na bakteria. Bakteria ya kisonono mara nyingi hupitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati wa kujamiiana, ikiwa ni pamoja na kujamiiana kwa mdomo, mkundu au uke.

Soma Zaidi...
Dalili za kipindupindu na njia za kujilinda na kipindupindu.

Post hii inazungumzia zaidi kuhusiana na ugonjwa wa kipindupindu.kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu anaitwa vibrio cholera.mdudu huyu hushambulia utumbo mdogo na kusababisha madhara mengi.

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa mapafu.

posti hii inahusu dalili za ugonjwa wa mapafu.ambapo kitaalamu hujulikana Kama Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu yako. Majimaji mengi kw

Soma Zaidi...
Ni Nini husababisha kukosa choo? (Constipation)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazopelekea kukosa choo ,yaani kinyesi kuwa kigumu au kukosa kabisa choo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea.

Soma Zaidi...
Tahadhari za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI

Soma Zaidi...